Home Page
Maisha Ya Shekh
Vitabu Vyake
Hukumu Na Fat’wa
Wito na fikra za shekh
Vitabu Vya Mwanae
Maktaba Ya Kituo
Picha
Wasiliana Nasi


Affiliate Websites
Affiliate Websites

   E-Mail Listing:


 

AL-AHKAAMUL WAADHIHA 

HIZI NI FAT’WA ZA KIONGOZI WA KIDINI AYATULLAHI AL-UDHMA ALHAJI SHEKH MOHAMMAD FAADHIL LANKARAANIY

( Mundu amrefushie umri)

TAQLIID

Mas’ala 1: Ni wajibu kwa kila mukallafu ambae hajafikia daraja ya ijtihadi imma kuwa muqallid (kumfua mujitahidi Fulani katika mas’ala ya kisheria) au kufanya ihtiyaati katika ibada zake zote na utendaji kazi wake (kama biashara) na mengineyo na katika matendo yake mengine anayo paswa kuyafanya au kuyaacha.

Mas’ala 2: Matendo ya mtu wa kawaida ayafanyayo bila kufanya taqliid au ihtiyaat hayatoshelezi  kisheria maadamu haijulikani ya kuwa yako sambamba na ukweli au uhakika wa kisheria au yako sambamba na fat’wa za Mujitahid ambae ilikuwa ni wajibu kwake kumfuata katika utendaji wake.

Mas’ala 3: Taqliidi ni kazi au tendo lifanyikalo kwa kutegemea kauli ya Mujitahidi Fulani. Kwa hivyo basi haijuzu na haifai kumfuata au kufanya taqliid ya mtu asie kuwa Mujtahidi. Na niwajibu kwa mtu asie kuwa Mujtahidi kufanya taqliid ikiwa hakuweza kufanya ihtiyaat.

Mas’ala 4: Kauli yenye nguvu ni kwamba inawezekana kutosheka tu na kufanya ihtiyaati katika uwanja wa utendaji au katika matendo hata kama kufanya hivyo italazimu kurudia tendo hilo au mukallaf akaweza kufanya ijtihadi au taqliid.

Mas’ala 5: Ni wajibu kufanya uchunguzi na kumtafuata Mujtahidi alie kuwa Aalam (mwenye elimu zaidi kati ya Mamujtahidi) ikiwa kuna uwezekano wa kufanya hivyo, kutokana na wajibu wa kumfuata yeye au kufanya taqlidi yake mahala ambamo kuna ihtimali ya kutofautiana Mamujitahidi kutokana na kauli iliyo na nguvu zaidi.

Na makusudio ya Aaalam ni mwenye maarifa zaidi ya kanuni na dalili za mas’ala na mwenye kufahamu na kuelewa zaidi kuliko wenziwe na mwenye kufahamu vyema habari, na mzuri zaidi katika kufahamu hadithi, na kwa ufupi ni kuwa Aalam ni yule ambae ni mwenye uwezo mzuri zaidi wa kufanya istinbaat ( uchambuzi na utungaji wa sheria). Na Marejeo ya kumuainisha na kumthibitisha pia kumfahamu ni kwa ahlul khibrah wataalam wa mambo hayo na wenye ujuzi wa istimbati na utungaji wa sheria.

Mas’ala 6: Hufahamika kuwa huyu ni mjuzi zaidi kutokana na elimu ya kimaumbile au kitu chochote chenye nafasi kama hiyo kati ya elimu za kawaida au vitu vya kawaida viwezavyo kujulisha hali hiyo, au kwa kutumia vithibitisho na dalili zisizo pingika au kupingwa, au kwa kuenea habari ziletazo matumaini na yakini.

Mas’ala 7: Ikiwa kutakuwa na Mamujitahidi wawili na haikuwezekana kupata ujuzu au dalili (uthibitisho) wa yupi alie mjuzi zaidi kati yao wawili, ikiwa kutakuwa na ihtimali ya kuwa mmoja wapo ambae ni maalum ni mjuzi zaidi  basi hapo itawajibika kumfuata yeye (kufanya taqlidi yake).

Mas’ala 8: Ni sharti Mujtahidi awe na masharti yafuatayo, awe baaligh (balee) mwenye akili timamu, awe muumini na muadilifu na awe mwanaume na awe hai, kwa hivyo basi haijuzu kufanya taqliidi ya maiti kwa mara ya kwanza, na awe amezaliwa kwanjia ya ndoa halali (Twaharatul mawlid), na awe ni mwenye ujuzi zaidi, na kauli ya ahwat ni kuwa asiwe ni mwenye kuipenda dunia (asiwe mwenye kufuata mambo ya kidunia)

Mas’ala 9: Makusudio ya uadilifu ni kuwa awe na uwezo wa kinafsi wa kutekeleza mambo ya wajibu na kuacha madhambi  hasa mambo makubwa yaliyo haramishwa, na  utendaji wa mambo ya wajibu na kuacha ya haramu nje huthibiti kwa kuwepo uwezo wa kinafsi na kupitia murua wa mtu. Na uadilifu hujulikana na kufahamika kwa husnudh- dhaahir ( kuwa na dhahiri nzuri asie sifika kwa maovu), na huthibiti kwa ushahidi wa watu wawili waadilifu na kwa kuenea habari zitoazo ujuzi au yakini na matumaini.

Mas’ala 10: Ikiwa Mujtahidi atatokewa na jambo ambalo litamfanya akose sharti moja wapo kati ya masharti hayo  yaliyo tangulia itakuwa no wajibu kwa muqallid kuhamia kwa Mijtahidi mwingione.

Mas’ala 11: Ikiwa mukallaf atafanya taqliid na kumfuata mtu ambae hakuwa ametimiza masharti  na ukapita muda Fulani akifanya taqlidi yake atakuwa kama yule ambae hakufanya taqlidi asilan, ama ikiwa matendo yake aliyo yafanya yatakuwa sambamba na uhakika na ukweli wa kisheria au yako sambamba na fat’wa za Mujtahidi ambae ilikuwa ni wajibu kufanya taqlidi yake (ilikuwa ni wajibu kumfuata) wakati akifanya matendo hayo basi matendo hayo ni sahihi, laa sivyo matendo yake sio  sahihi.

Mas’ala 12: Ikiwa mukallaf atamuqallid Mujtahidi ambae anaruhusu na kujuzisha kubakia kwenye taqliid ya  Mujtahidi alie kufa, kisha Mujtahidi huyo akafa haijuzu kubakia kwenye taqlidi yake hasa kwenye mas’ala haya, bali ni wajibu kurudi na kurejea kwa alie hai ambae ni Aaalam (mjuzi zaidi) katika mas’ala ya kujuzu kubakia kwa alie kufa au hapana.

Mas’ala 13: Haijuzu kufanya taqliidi ya maiti (kumfuata Mujtahidi alie kufa) kwa mara ya kwanza, lau kama mukallaf atamfuata Mujtahidi alie hai kisha akafariki inajuzu kubakia kwenye taqlidi yake moja kwa moja bila pingamizi ikiwa watalingana kielimu kati ya alie kufa na yule alie hai, na lau kama alie kufa ni mjuzi zaidi itajuzu kubakia kwake, na katika mas’ala hayo hakuna tofauto kati ya mtu alie fanya matendo kwa mujibu wa fat’wa zake au mwingine.

Mas’ala 14: Ikiwa kutakuwa na Mamujitahidi wawili walio lingana kwenye elimu inajuzu kwa mukallaf kumfuata yeyote kati ya wawili hao na inajuzu kwake baadhi ya mas’ala kuchukua kwa Mujtahidi huyo na mengine kwa Mujtahidi mwingine. Ama ikiwa mmoja wao ni mwenye bora zaidi kuliko mwingine katika uadilifu au uchamungu au mfano wa hayo kauli ya ahwat ya wajibu ni kuwa atamchagua huyo.

Mas’ala 15: Inajuzu kuhama baada ya kuwa mukallaf amefanya taqliid kutoka kwa Mujtahidi alie hai kwenda kwa Mujtahidi mwingine alie hai na ambae analingana nae kielimu na ni wajibu kuhama ikiwa wa pili ni mjuzi zaidi.

Mas’ala 16: Njia za kufahamu fat’wa za Mujtahidi ni kama zifuatazo:

1- Kusikia kwa Mujitahidi akisema yeye mwenyewe.

2- Kuambiwa na watu wawili waadilifu, na haitoshi kutosheka na habari za mtu mmoja muadilifu (yaani kutosheka na habari za mtu mmoja kuna ishkaali), isipokuwa ikiwa habari yake itatupa matumaini na yakini.

3- Kuwepo kwa fat’wa kwenye risalatul amaliyyah (kitabu chake cha fat’wa) ikiwa kimeandikwa na yeye mwenyewe au kwa khati yake, au kuzielewa fat’wa zake zote.

Mas’ala 17: Ikiwa mtu atanukuu kimakosa fat’wa ya Mujtahidi ni wajibu kwake kuwatangazia walio jifunza kwake,  vilevile  ni wajibu juu ya Mujtahid kutangaza ikiwa atakosea katika kuibainisha fat’wa yake.

Mas’ala 18: Ikiwa mtu atanukuu fat’wa ya Mujtahidi ikiwa sahihi, kisha rai ya Mujtahidi ikabadilika kuhusiana na fat’wa hiyo au katika mas’ala hayo kutokana na kauli ya ahwati ni kuwa niwajibu kwa mtu alie nukuu kumtangazia alie sikia kutoka kwake fat’wa ya mwamzao.

Mas’ala 19: Ikiwa watu wawili walio nukuu fat’wa watapingana au dalili mbili zikapingana katika kunukuu fat’wa ya Mujtahidi, mwenye kunukuu na dalili hizo zitaporomoka yaani hazitakuwa na maana. Na ikiwa alienukuu atapingana na alie sikia kutoka kwa Mujtahidi mwenyewe atatangulizwa na kupewa kipaumbele alie sikia.Ama ikiwa atapingana alie sikia au alie nukuu kwa kutoa kitabu cha fat’wa za Mujtahi yule hapo kitatangulizwa kitabu chake cha fat’wa ikiwa kitabu hicho kimeandikwa kwa hati yake au ikiwa ni mwenye kuyajua yote yaliyomo kwenye kitabu hicho kiukamilifu.

Mas’ala 20: Muqallid (mwenye kumfuata Mujtahidi) anayo hiari kati ya kufanya matendo kulingana na ihtiyaati ya Mujtahidi ambae ni Aalam (mjuzi zaidi)- ikiwa hakuwa na fat’wa kwenye mas’ala fulani- na kati ya kurejea kwa mwingine, na hapo ata angaliwa mjuzi zidi kuliko mwingine.

Mas’ala 21: Ikiwa Muqallid atakuwa na shaka juu ya kufariki kwa Mujtahidi au kubadilika rai yake au kutokea mambo ambayo hayajuzishi kumfuata au kumfanyia taqliid inajuzu kwa mtu huyo kubakia kwa Mujtahidi huyo mpaka hali yake ibainike vizuri.

Mas’ala 22: Hukumu ya Al-haakim alie timiza masharti haijuzu kuipinga hata kama ni Mujtahidi mwingine, ispokuwa ikiwa litabainika kosa lake kwenye hukumu hiyo.

Mas’ala 23: Ni wajibu kwa mtu wa kawaida katika muda mbao bado anafanya uchunguzi wa kumtafuta Mujtahidi au aliekuwa Aalam kufanya ihtiyaati kwenye matendo yake.

Mas’ala 24: Ikiwa mukallaf atafahamu ya kuwa yeye alikuwa akifanya ibada zake bila kufuata fat’wa za Mujtahidi yaani hakuwa akifanya taqliid kwa muda kadhaa na hakuweza kufahamu kiasi cha muda huo, ikiwa atafahamu namna zilivyo kuwa zikifanyika ibada zile na akafahamu ya kuwa zilikuwa sambamba na uhakika wa kisheria au fat’wa za Mujtahidi ambae ndie aliepewa jukumu la kurejelewa, hapo hakutakuwa na jukumu lolote juu yake, laa sivyo itamuwajibikia kufanya kadhaa au kulipa kiwango ambacho anayakini nacho ikiwa kukhalifu huko kunamlazimu kulipa kadhaa kulingana na mtizamo au rai ya Mujtahid, na kauli ya ahwat ya sunna ni kuwa atalipa  na kufanya kadhaa kiwango ambacho anafahamu yakuwa kwa kufanya hivyo jukumu lake litakuwa limemuondokea (baraa atudhimmah).

Mas’ala 25: Ikiwa utapita muda tangu muqallid awe baaligh ( balee), na akaingiwa na shaka baadae ya kuwa matendo yake alikuwa akiyafanya kwa kumfuata Mujtahidi au kwa kufanya taqliid sahihi au laa,  inajuzu kwake kuyajengea matendo yake yaliyo tangulia  kuwa ni sahihi, ama matendo yake yafuatayo ni wajibu juu yake kuyasahihisha kwa wakati huo kwa kufanya taqliid.

Mas’ala 26: Ikiwa rai ya Mujtahidi itabadilika  wakati huo haijuzu kwa muqallid kubakia kwenye rai yake ya mwanzo ikiwa rai hiyo haiwafikiani na ihtiyaat, laa sivyo itajuzu kubakia kwake kwa anwani ya kuwa inawafikiana na ihtiyaat si kwa anwani ya taqliid.

Mas’ala 27: Ikiwa mukallaf atamfuata mtu ambae si mwenye uwezo wa kutoa fat’wa kisha akalifahamu hilo ni wajibu juu yake kuhama, na matendo yake aliyoyafanya mwanzo ni sawa na matendo ya jaahili alie fanya matendo yake bila ya taqliid. Na pia itakuwa ni wajibu kutokana na kauli yenye nguzu zaidi kuhamia kwa alie kuwa Aalam kwa yule ambae alikuwa akimfuata asie kuwa Aalam, au alikuwa akimfuata Aalam kisha baadae mwingine akawa ni Aalam zaidi yake.

Mas’ala 28: Ikiwa suala la Aalamiyya (Mjuzi zaidi) litafungika kwa watu wawili na haikuwezekana kumuainisha mmoja wapo kuwa ni Aalam zaidi- kwa sababu kwa kila mmojawapo kunaihtimali ya kuwa ni Aalam- hapa hukumu yake ni kumfuata yeyote kati yao bila kipingamizi, sawa iwezekane kufanya ihtiyaat kati ya kauli mbili za watu hao au laa.

Mas’ala 29: Alie chukuwa uwakala wa kufanya matendo badala ya mtu mwingine atafanya matendo yale kwa mujibu wa taqliid ya alie mchukulia uwakala na si kwa mujibu wa taqliid yake ikiwa wanatofautiana katika Mujtahidi, ama alie usiwa (Wasii) kwa mfano lau kama atakuwa ni mwenye kuusiwa kukodisha watu wa kusali sala kwa niaba yake hapo ni wajibu matendoyake yawe sawa au kwa mujibu wa fat’wa za Mujtahidi wake.

 Mas’ala 30: Mtu alie idhinishwa na kupewa uwakala na  Mujtahidi wa kutumia au kusimamia  mali ya waqfu au mali ya watoto wasio na walii humalizika idhini hiyo au uwakala huo kwa kufariki Mujtahidi yule, tofauti na mtu alie teuliwa na kupewa jukumu na Mujtahidi la kusimamia vitu vya waqfu au usimamizi wa watoto au wendawazimu wasio kuwa na msimamizi( walii), hakika  yeye usimamizi wake na uangalizi wake  haubatiliki kwa kauli iliyo dhahiri.

Mas’ala 31: Ni wajibu kwa mukallaf kufahamu sehemu zote za ibada na masharti yake na vizuizi vyake na vitangulizi vyake hata kama ni kwa sura ya ujumla, kiasi kwamba awe anafahamu yakuwa ibada yake imetimiza sehemu zote na masharti yote na haina vizuizi.

Mas’ala 32: Ikiwa yatamtokea mukallaf  mas’ala fulani ambayo hajui hukumu yake na  akiwa katikakati ya sala inajuzu kwake kufanya tendo lake kwa kufuata upande mmoja wapo kati ya pande mbili za mas’ala hayo, akikusudia kuuliza hukumu yake baada ya sala na akiwa ameazimia kuirudia sala hiyo ikiwa haikuwafikiana na ukweli ulivyo wa kisheria, na lau kama tendo lake litakuwa sambamba na hukumu ya kisheria haitakuwa ni wajibu kwake kuirudia.

Mas’ala 33: Kama ambavyo ni wajibu kufanya taqliid katika mambo ya wajibu na haraam, pia ni wajibu katika mambo ya sunna ambayo kunaihtimali ya kuwa ni wajibu, na katika mambo ya makruuh na mubaha ( si wajibu wala haram) yenye ihtimali ya kuwa yanaulazima wa kutekelezwa.

Mas’ala 34: Tamko ( Ahwat) lililo tajwa katika  kitabu hiki linakusudiwa kwa maana ya ihtiyaat ya sunna ikiwa limetanguliwa na limefuatiwa na fat’wa, laa sivyo  lina maana ya ihtiyati ya wajibu, na maana yake ni kuwa mukallaf wakati huo anahiari  kati ya kufanya tendo hilo na kati ya kurejea kwa Mujtahidi mwingine pamoja na kuchunga suala la alie kuwa Aalam (mjuzi zaidi), tofauti na ihtiyaati ya sunna, haijuzu katika ihtiyaati hiyo kurejea kwa mwinginewe, bali mukallaf ana hiari kati ya kufanya kwa mujibu wa ihtiyaati hiyo au kufanya kwa mujibu wa fat’wa iliyo tangulia au ifuatayo.

Mas’ala 35: Ikiwa mukallaf atafunga mkataba au kufanya  makubaliano na mtu fulani au akafanya tendo fulani kwa mijibu wa taqliidi ya Mujtadi anae hukumu ya kuwa mkataba huo na matendo hayo ni sahihi kisha Mujtahidi huyo akafa, na akamfuata anae sema ya kuwa mkataba huo ni batili inajuzu kwa mukallaf huyo kujengea kuwa  matendo yake yaliyo tangulia ni sahihi.

 KITABU TWAHARA (MLANGO WA TWAHARA)

 KATIKA MLANGO HUU KUNA SEHEMU TOFAUTI

 SEHEMU YA KWANZA

 MGAWANYIKO WA MAJI NA HUKUMU ZAKE 

NA KATIKA SEHEMU HII KUNA VIFUNGU KADHAA

KIFUNGU CHA KWANZA

MAJI  YAMEGAWANYIKA SEHEMU MBILI

SEHEMU YA KWANZA:

 Maji Mutlaq, hiki ni kitu chenye kutiririka na ambacho huitwa kwa jina la (Maji) bila kuongeza kitu, kama maji yaliyopo kwenye kisima au mto au bahari. Na tusemapo maji ya bahari au maji ya mto au maji ya kisima husema hivyo kwa ajili ya kuyapambanua, si kwa sababu ya kusahihisha matumizi.

SEHEMU YA PILI:

Maji mudhaaf,  ni kitu chenye kutiririka ambacho haifai kuitwa kwa jina la (maji) pekee,  bali huongezewa neno lingine kama ifuatavyo: Maji ya komamanga kwa mfano, au maji ya waridi kwa kutaja jina lililo dhifiwa kwenye tamko maji. Na pengine huitwa (Maji) kwa majazi, kwa sababu hii inafaa kuto tumia neno maji kwenye neno hilo.

KIFUNGU CHA PILI:

 MAJI MUTLAQ (Maji halisi) NA HUKUMU ZAKE

Maji mutlaq yamegawanyika sehemu zifuatazo: 1-Maji yenye kutiririka.  2- Maji ya chemchem yasiyo tiririka. 3- Maji ya kisima. 4- Maji ya mvua.  5- Maji ya kuri moja 6- Maji kidogo (yasiyo fikia kiwango cha kuri moja).

Mas'alal 36: Maji mutlaq na mgawanyiko wake wote kama hayakuingiwa na najisi ni twahara na ni yenye kutwahirisha hadathi na khabathi.

Mas'ala 37:Maji mutlaq na mgawanyiko wake wote  hata maji yenye kutiririka ikiwa yatabadilika na kugeuka moja ya sifa zake tatu kwa kuingiwa na najisi hunajisika, Na sifa hizo ni rangi ladha na harufu. Na maji kidogo yananajisika tu kwa kuingiwa  na najisi.

Mas'ala 38: Ikiwa maji yatabadilika  na ubadilikaji huo haukuwa ni katika moja kati ya sifa zake tatu, rangi ladha na harufu, kama yakibadilika uzito wake  na mfano wa hayo, maji hayo hayata najisika ikiwa hayakubadilika na kuwa maji mudhaafu.

Mas'ala 39: Ikiwa rangi ya maji itabadilika au ladha yake au harufu yake kwa kukaribiana na najisi, kama  mzoga ukiangukia karibu na maji hayo na mzoga huo ukawa ukingoni mwa maji hayo hayatanajisika vile vile.

Mas'ala 40: Ikiwa maji hayakubadilika kwa najisi  maji hayo si najisi, kama yakibadilika kwa kitu kilicho najisika, kama ikiwa  yatabadilika na kuwa ya njano au mekundu kwa kuingiwa na juisi iliyo najisika.

Mas'ala 41: maji hayanajisiki tu kwa kuingiwa na najisi au kubadilika kwa kuingiwa na najisi yenyewe, bali  ikiwa yataingiwa na kitu chenye najisi au kilicho beba sehemu na chembe chembe za najisi, au kitu hicho kina chembe chembe za najisi na maji yale yakabadilika na kugeuka kwa najisi ile, maji hayo yatanajisika pia.

Mas'ala 42: Inatosha kunajisika kwa maji kubadilika kwake kwa sababu ya kuingiwa na najisi hata kama hayakubadilika sifa zake zote, kwa mfano lau kama  maji hayo yatabadilika rangi yake na kuwa rangi ya njano au nyekundu kwa kuingiwa na damu, au yakawa na harufu iliyo kinyume na harufu ya mkojo na haja kubwa kwa kuangukia najisi hizo kwenye maji hayo, maji hayo yatakuwa yamenajisika pia.

KIFUNGU CHA TATU

MAJI  YENYE KUTIRIRIKA  NA HUKUMU ZAKE

Haya ni maji yenye kutiririka na yaliyo ungana na mada ya ardhini au nyingineyo hata kama hayatoki na kuchimbuka ardhini.

Mas'ala 43: Maaul jaariy (maji yenye kutiririka) sawa yawe ni kiasi cha kuri moja au yawe ni kiasi kidogo kuliko kuri, na sawa utiririkaji wake uwe ni wa kuchupa au kunyunyiza,. hayanajisiki kwa kuingiwa na najisi kama hayajabadilika sifa zake.

Na huambatanishwa na maji yenye kutiririka katika hukumu ya kuto najisika kwa kuingiwa na najisi bila kubadilika, maji yote yachimbukayo ardhini hata kama hayatiririki.

Mas'ala 44: Ikiwa maji yenye kutiririka juu ya ardhi bila ya kuwa na asili ichimbukayo ardhini au  yenye kunyunyiza, ikiwa majio hayo yatakuwa ni machache zaidi kuliko kuri ya maji,  hakika maji hayo hunajisika kwa kuingiwa tu na najisi.

Ama ikiwa mukallaf atatia shaka ya kuwa maji hayo yana chimbuko  (mada) au laa kauli yenye nguvu inasema kuwa hayata najisika  maji hayo kwa kuingiwa au kukutana na najisi ikiwa hapo kabla hayakutanguliwa na hali ya kuto kuwa na mada.

Mas'ala 45: Kizingatiwacho katika kuto najisika maji yatiririkayo ni kuungana kwake na mada (asili kama chemchem au kuungana na bomba), kwa mfano lau kama mada au asili ya kutiririka kwa  maji hayo iko juu, na mada  yenye kutiririsha au kunyunyiza maji hayo itakuwa  ni chini ya kuri moja maji hayo yatanajisika, ndio ikiwa sehemu inayo nyunyiza au asili ya maji hayo itagusana na najisi maji hayo hayatanajisika.

Mas'ala 46: Maji yaliyo tuwama na yaliyo ungana na maji yenye kutiririka hukumu yake ni sawa na maji yenye kutiririka katika  hukumu ya kuto najisika kwake kwa kugusana au kuingiwa na najisi au kitu kilicho najisika, kwa mfano hodhi lililo ungana na mto kwa ajili ya umwagiliaji, maji yake hayanajisiki kwa kugusana na najisi, vile vile kingo za mto hata kama maji yake yametuwama na hayatiririki.

Mas'ala 57: Ikiwa baadhi ya sehemu ya maji yenye kutiririka itabadilika na sehemu nyingine isibadilike, sehemu ya maji hayo iliyo ungana na mada hainajisiki kwa kuungana  au kuingiwa na najisi hata kama maji yake ni machache, na upande mwingine hukumu yake ni sawa na hukumu ya maji yaliyo tuwama ikiwa maji ya sehemu hiyo yatabadilika, laa sivyo yatahesabiwa yamenajisika kiwango kilicho badilika pekee, kwa kuungana  yale mengine na mada.

  KIFUNGU CHA NNE

  MAJI  YALIYO  TUWAMA  NA HUKUMU ZAKE

Mas'ala 48: Maji yaliyo tuwama bila kuungana na mada ikiwa kiwango chake hakifikii kuri moja hakika maji hayo yananajisika kwa kuingiwa na najisi, tofauti na ikiwa yanafikia kuri moja, hakika yakiwa ni kuri moja hayanajisiki kwa kuingiwa au kukutana  na najisi isipokuwa yatakapo badilika moja kati ya sifa zake tatu.

Mas'ala 49: Kiwango cha kuri kwa uzito ni sawa na huqqa ya istambuli 280, ama ukubwa wake ni sawa na shibiri 34 kasoro moja ya tatu, na kwa lita ni sawa na lita 377 takriiban.

Mas'ala 50: Maji yakiwa ni chini ya kuri moja hata kama ni kwa kiasi kichache hukumu yake ni sawa na hukumu ya ya maji kidogo.

Mas'ala 51:Ikiwa najisi itaangukia kwenye kuri na haikujulikana ya kuwa imeangukia humo kabla ya kufika kuri au baada ya kukamilika kuri, maji hayo yatahukumiwa kuwa ni twahara, isipokuwa ikiwa itafahamika tarehe ya kuangukia kwake humo na tarehe ya kufikia kwake kuri haikujulikana.

 Mas'ala 52: Ikiwa imefikia kuri lakini haikujulikana ya kuwa ni maji mutlaq (ni maji halisi) au mudhaaf, na yakaingiwa na najisi,  maji hayo hayata hukumiwa kuwa ni najisi, isipokuwa itakapo kuwa  hali yake ya mwanzo ilikuwa ni mudhaaf na kukawa na shaka ya kuwa bado ni mudhafu.

 Na ikiwa kunakuri mbili moja ni mutlaq na nyingine ni mudhaaf, na ikafahamika kuingiwa na najisi moja kati ya kuri hizo mbili  lakini haijulikani kuwa ni ipi kati ya kuri hizo,  zote mbili zitahukumiwa kuwa ni twahara pia.

KIFUNGU CHA TANO

  MAJI YA MVUA NA HUKUMU ZAKE

 Mas'ala 53: Hukumu ya maji ya mvua wakati ikinyesha ni sawa na hukumu ya maji yenye kutiririka, hayata najisika kwa kugusana na najisi ikiwa hayajabadilika moja kati ya sifa zake,  hata kama  mvua hiyo ni kidogo, sawa maji hayo yatiririke kwenye mifereji au juu ya ardhi au laa, la muhimu ni kuthibiti kuwa ni maji ya mvua, na ikiwa yatakusanyika sehemu moja na kikaoshewa ndani  yake kitu kilicho najisika  kitu hicho kitatwahirika hata kama maji yale yatakuwa ni madogo.

Haya yote ni wakati mvua ikiendelea kunyesha, na ikiwa mvua itakatika na kuacha  kunyesha hukumu yake ni sawa na hukumu ya maji yaliyo tuwama.

Mas'ala 54: Nguo iliyo najisika  na zulia lililo najisika ikiwa vitu viwili hivi vitanyeshewa na mvua na maji kuingia ndani ya vitu hivyo basi vitu  hivyo vyote vitatwahirika, na haihitaji kukamua au kuosha kwa mara kadhaa, na ikiwa  maji yatafika kwenye baadhi ya sehemu na hayakuenea sehemu zote itatwahirika sehemu zilizo fikiwa na mvua hiyo  na si vinginevyo. Na hukumu hii inahusika tu ikiwa hakuna najisi yenyewe kwenye vitu hivyo, laa sivyo havitwahiriki isipokuwa vitakapo nyeshewa tena baada ya kuondoka najisi yenyewe kwenye vitu  hivyo.

Mas'ala 55: Ardhi iliyo najisika hutwahirika kwa kunyeshewa na mvua kwa sharti kwamba mvua hiyo iinyeshee moja kwa moja kutoka mawinguni  hata kama ni kwa kupeperushwa na upepo,  ama ikiwa mvua hiyo itanyeshea juu ya kitu kingine – kama ambavyo maji hayo yatatiririkia juu ya ardhi baada ya kuangukia mahali pengine na kuingiwa na najisi- katika hali kama hii haita twahirika.

Ndio  ikiwa mvua hiyo itanyesha juu ya ardhi kisha maji yake yakatiririkia juu ya paa basi sehemu hiyo itatwahirika.

Mas'ala 56: Ikiwa maji ya mvua yataangukia kwenye najisi yenyewe kisha yakadondokea kwenye kitu kingine, kitu hicho hakita najisika ikiwa maji hayo hayakuwa na chembe chembe za najisi ndani yake na hayakubadilika kwa najisi.

Mas'ala 57: Mchanga ulio najisika hutwahirika kwa kunyeshewa na mvua ikiwa mvua hiyo itaingia hadi ndani ya mchanga huo na kubadilika kuwa udongo.

Mas'ala 58: Jamvi lililo najisika linatwahirika kwa kunyeshewa na mvua, vilevile zulia lililo tandikwa juu ya ardhi, na ardhi iliyopo chini ya zulia hilo ikiwa ni najisi hutwahirika  ikifikiwa na maji ya mvua. Ndio ikiwa jamvi au zulia havikuwa juu ya ardhi au kukawa na utengano, hapo kuna ishkaali katika hukumu ya kutwahirika kwake kwa kunyeshewa na mvua, kwanza kwa kunyeshea mvua juu ya jamvi au zulia kisha maji hayo yakadondokea juu ya ardhi.

Mas'ala 59: Chombo ambaacho nbi  najisi kinatwahirika ikiwa maji ya mvua yatafika sehemu zote zenye najisi katika chombo hicho isipokuwa ikiwa kimenajisika kwa kuliwa na mbwa ndani yake, katika hali kama hiyo kutwahirika chombo hicho kwa kunyeshewa na mvua tu bila ya kukisugua au kukiosha kwa mchanga kuna ishkaali, lakini ikiwa kitanyeshewe na mvua baada ya kukisugua au kukiosha kwa mchanga wakati huo kitatwahirika bila ya kuhitajia kuosha mara kadhaa.

KIFUNGU CHA SITA

MAJI YA BAFUNI NA HUKUMU YAKE

Mas'ala 60: Maji ya bafuni ni sawa na maji yenye kutiririka kwa sharti kuwa yawe yameungana na mada, kwa mfano maji yaliyoko kwenye mahodhi madogo ikiwa yataungana na mada hayanajisiki kwa kuingiwa na najisi ikiwa maji yaliyoko kwenye hodhi pekee au kwa kuyaunganisha na yaliyomo kwewnye mada yanafikia kuri.

Mas'ala 61:Ikiwa maji yaliyomo kwenye mahodhi madogo yatanajisika yanatwahirika kwa kuungana na mada kwa sharti kwamba maji ya mada yawe ni kuri na yachanganyike pia.

KIFUNGU CHA SABA

 MAJI YA KISIMA NA  HUKUMU  ZAKE

Mas'ala 62: Hukumu ya maji ya kisima yenye kuchimbuka ardhini ni sawa na hukumu ya maji yenye kutiririka katika hukumu ya kuto najisika isipokuwa kwa kubadilika moja kati ya sifa zake, sawa yawe ni kiasi cha kuri moja au chini ya hapo, na ikiwa yatabadilika  kisha ubadilikaji huo ukaondoka na kutoweka wenyewe maji hayo yatatwahirika kwa sababu yana mada na yamechanganyika na maji yatokayo kwenye mada kama chemchem. Ama yakiwa hayana mada yenye kuchimbuka basi itazingatiwa kiasi cha kuri katika hali ya  kutonajisika kwake hata kama kitaitwa kisima, kama mfano wa visima ambavyo hukusanyika ndani yake maji yasiyo chimbuka  ardhini.

Mas'ala 63: Maji  najisi yaliyo tuwama sawa maji hayo yawe ni kuri au  kidogo  yanatwahirika kwa kuungana na maji ya kuri yaliyo twahara au kwa kuungana na maji yenye kutiririka au maji yenye kuchimbuka ardhini hata kama hayatiririki na kuchanganyika na maji hayo, na pia hutwahirika kwa kukutana na kuchanganyika na maji ya mvua,  na kauli ya ahwat ni kuwa kutazingatiwa kuchanganyika kwa maji hayo.

Mas'ala 64: Birika lililo jazwa maji yaliyo najisika ikiwa litazamishwa kwenye hodhi  hutwahirika baada ya kuchanganyika maji hayo, na si wajibu kuyamwaga maji yake na kuliosha birika hilo.

KIFUNGU CHA NANE

MAJI YALIYO TUMIKA YAKIWA NI MACHACHE

Mas'ala 65: Maji yaliyo tumika  kutawadhia ni twahara na yanatwahirisha hadathi na khabathi, vile vile maji yaliyo tumika katika ghusli ya sunna, ama maji yaliyo tumika katika ghusli ya hadathi kubwa pamoja na kuwa mwili hutwahirika hakuna ishkaali katika utwahara wa maji hayo na juu  uwezekano wa kuyatumia kuondolea khabathi, na kauli yenye nguvu zaidi ni kuwa inajuzu kuyatumia kuondolea hadathi pia japokuwa kauli ya ahwati ni kuwa nivema kujiepusha na maji hayo.

Ama maji yaliyo tumika kuondoa khabathi tofauti na maji yaliyo tumika kustanji haijuzu kuyatumia katika udhu na ghusli, na kauli yenye nguvu zaidi ni kuwa maji yatumikayo kuondolea najisi yenyewe ni najisi, bali hata maji yaliyo tumiwa kuoshea yasiyo ondoa najisi, ama  maji ya kustanjia  hukumu yake itafuatia.

Mas'ala 66: Hakuna ishkaali katika matone ambayo hudondokea kwenye chombo wakati wa kuosha hatakama tutasema ya kuwa haijuzu kutumia maji yaliyo oshewa hadathi kubwa. Na maji yanayo bakia kwenye nguo baada ya kukamuliwa nguo hiyo ni twahara, ikiwa maji hayo yatatoka baada ya nguo hiyo kukamuliwa hayata ambatanishwa na hukumu ya maji yaliyo oshewa.

 Na mkono hutwahirika kwa kufuata kitu kinacho twahirishwa baada ya kukitwahirisha kitu hicho, kwa hivyo hakuna haja ya kuiosha mikono hiyo, pia chombo ambacho hutumika kuoshea nguo na mfano wa hivyo.

KIFUNGU CHA TISA

  HUKUMU YA MAJI  YENYE  KUTILIWA  SHAKA

Mas'ala 67: Maji ambayo hutiliwa shaka ya kuwa ni najisi au twahara maji hayo ni twahara ikiwa haikujulikana ya kuwa hapo kabla yalikuwa ni najisi, ama maji ambayo hutiliwa shaka ya kuwa ni mutlaq au hapana hayahukumiwi maji hayo kuwa ni mutlaq isipokuwa ikiwa hapo kabla yalikuwa ni mutlaq.

Ndio, ikiwa maji hayo ni kuri moja na yakaingiwa na najisi hayatahukumiwa kuwa ni najisi isipokuwa ikiwa hapo kabla yalikuwa ni maji mudhaaf, ama maji ambayo yanatiliwa shaka ya kuwa ni mubaha au hapana (maji halali) maji hayo hukumu yake ni kuwa ni mubaha, aisipokuwa ikiwa hapo kabla yalikuwa ni milki ya mtu mwingine au yalikuwa katika milki ya mtu mwingine ambae kuna ihtimali kuwa ni maji yake.

Mas'ala 68: Ikiwa mukallaf atafahamu kwa sura ya ujumla ya kuwa mojawapo  kati ya vyombo viwili ni najisi  na kingine ni twahara haitajuzu kutumia chombo moja wapo kuondolea khabathi au hadathi.

Mas'ala 69: Chombo kinacho shukiwa kuwa sehemu moja wapo ya chombo hicho imenajisika  hakita hukumiwa kuwa ni najisi isipokuwa  hali ya sehemu  hiyo ya hapo kabla itajulikana kuwa ilikuwa ni najisi, lakini kauli ya ahwat inasema kuwa ni bora kujiepusha na utumiaji wa chombo hicho.

Mas'ala 70: Ikiwa maji mutlaq yatafanana na mudhaaf itajuzu kuyatumia maji hayo kuondolea khabathi kwa kutumia moja wapo kati ya maji hayo na kuoshea kwa kutumia maji mengine, vile vile katika kuondoa hadathi.

Mas'ala 71: Ikiwa itafahamika kwa sura ya ujumla ya kuwa maji haya ima ni najisi au

ni mudhaaf inajuzu kuyanywa maji hayo, lakini haijuzu kuyatumia kutawadhia, vile vile ikiwa itajulikana ya kuwa ima maji hayo ni mudhaaf au ni maghsuub (ya kunyang'anya).

Ama ikiwa itajulkikana ya kuwa maji hayo ni najisi au ni ya kunyang'anya haitajuzu kuyanywa, kama ambavyo  haitajuzu kuyatumia kutawadhia.

Mas'ala 72: Ikiwa sehemu au pande zitiliwazo shaka au zenye shubha hazijulikani kidhati, katika hali kama hii inajuzu kuyatumia maji hayo bila kipingamizi.

KIFUNGU CHA KUMI
HUKUMU ZA  MAJI  MUDHAAF

Mmas'ala 73: Maji mudhaaf, kama maji ya uwa waridi ni twahara ikiwa hayakuingiwa na najisi, lakini maji hayo si yenye kutwahirisha hadathi,  vilevile si yenye kutwahirisha khabathi hata katika hali ya dharura.

Mas'ala 74: Maji mudhaaf yana najisika kwa kuingiwa tu na najisi sawa yawe mengi au kidogo, isipokuwa yakiwa ni yenye kuchupa  kwa nguvu juu ya najisi, hata kama yanatoka chini kwenda juu kama maji yatokayo kwenye bomba lenye kunyunyizia  na mfano wa hiyo, katika hali kama hii itahukumiwa kuwa ni najisi sehemu ile tu iliyo gusana na najisi, na haivuki na kuelekea juu.

Mas'ala 75: Ikiwa maji mudhaaf yatanajisika hayatatwahirika isipokuwa kwa kuyaweka kwenye kuri  au kwenye maji yenye kutiririka na kutoweka hali ya kuwa kwake maji mudhafu. Na kutwahirika  kwa maji mudhaaf  yaliyo najisi kwa kuyachemsha ( au kuongeza kiwango cha maji hayo) kuna ishkaali.

 

KIFUNGU CHA KUMI NA MOJA
MABAKI YA CHAKULA

Mas'ala 76: Mabaki ya chakula yote ni twahara isipokuwa mabaki ya mnyama alie najisi (najisul aini) kama mbwa Nguruwe na mushrik (kafir) , hakika mabaki yao ni najisi.

Mas'ala 77: Nimakuruhu kula mabaki ya mnyama asie liwa isipokuwa mabaki ya Muumini na paka kutokana na kauli ya baadhi ya mujtahidiin.

SEHEMU YA PILI: HUKUMU ZA CHOONI

 

 

PIA KUNA VIFUNGU KADHAA

  KIFUNGU CHA KWANZA

   

  HUKUMU ZA KWENDA CHOONI

Mas'ala 78: Ni wajibu wakatio mtu anapokwenda chooni au katika hali ya kujisaidia haja kubwa bali hata katika hali nyingine tofauti kusitiri uchi (sehemu za siri) – nazo ni sehemu ya mbele na nyuma na peke mbili- kwa muonaji mwenye kuheshimiwa, isipokuwa mtoto na mwenda wazimu wasio weza kupambanua, na mke na mume na alie milikiwa kwa mmiliki wake na alie halalishwa kwa alie halalishiwa, hakika kwa watu hawa inajuzu kwa kila mmoja wao kuangalia uchi wa mwenziwe.

Mas'ala 79: Hakuna tofauti katika uharamu wa kuangali kati ya uchi wa  Muislaam au kafiri kutokana na kauli ya ahwat.

Mas'ala 80: Si wajibu kusitiri mapaja mawili wala matako wala nywele ziotazo pembezoni mwa sehemu za siri (mavuzi). Ndio, ni sunna kusitiri sehemu zilizoko kati ya kitovu na magoti.

Mas'ala 81: Haijuzu kuangalia uchi wa mtu mwingine kwa kutumia kioo na mfano wa hicho, wala kwa kutumia kioo cha kujitizamia  na wala haijuzu kuangalia kwa kutumia maji yaliyo safi. 

Mas'ala 82: Ikiwa mtu itamlazimu kuangalia uchi wa mtu mwingine kama katika hali ya kumtibu mgonjwa, kauli ya ahwat ni kuwa ataangalia kupitia kioo kilicho wekwa mbele yake ikiwa kufanya hivyo kutatosheleza na kuondoa dharura hiyo, laa sivyo hakuna tatizo  kuangalia.

Mas'ala 83: Ni haramu kwa mwenye kujisaidia haja kubwa – wakati wa kujisaidia- kuelekea Qibla na kukipa mgongo Qibla kwa kuielekeza sehemu ya mbele ya mwili wake  kwenye Qibla hata kama uchi wake atauelekeza sehemu au upande mwingine tofauti na sehemu hizo mbili, na kauli ya ahwat ni kuwa ataacha  kukielekezea  uchi wake pekee hata kama sehemu za mbele za mwili wake zitaelekea  sehemu hizo mbili, na makusudio ya sehemu za mbele za mwili ni kifua tumbo na magoti mawili, na ikiwa italazimika kufanya moja wapo atakuwa na hiari japokuwa kauli ya ahwat ni kuwa atakipa mgongo, na akiwa itamlazimu kufanya kitendo kimoja wapo  kati ya mambo mawili hayo na kuto jisitiri pamoja na kuwepo muangaliaji mwenye kuheshimiwa itawajibika kwake kujisitiri.

Mas'ala 84: Kauli yenye nguvu ni kuwa si haramu kukielekea au kukipa mgongo kibla katika hali ya kufanya istibraa na katika hali ya kustanji japo kuwa kutofanya hivyo ni ahwat (bora zaidi). Ndio ikiwa atafahamu ya kuwa mkojo utatoka  kwa kufanya istibraa kauli ya ahwat ni kuwa itawajibika kuacha kukielekea au kukipa mgongo Qibla.

Mas'ala 85: Lau kama mukallaf atapatwa na shubha katika kukipambanua Qibla hukumu ya kutumia dhanna haiko mbali pamoja na kuto kuwepo uwezekano wa kukitafuta na kufanya uchunguzi wa sehemu ya Qibla, na ikiwa kuichelewesha sala kutamsababishia matatizo.

Mas'ala 86: Ni haramu kujisaidia haja kubwa kwenye milki ya mtu mwingine isipokuwa kwa idhini yake, vile vile ni haramu kujisaidia kwenye makaburi ya waumini ikiwa kufanya hivyo ni kuvunja heshima yao.

Mas'ala 87: Ni haramu kujisaidia haja kubwa kwenye mashule na mfano wa hayo ikiwa haikufahamika kuwa sehemu hizo zimewekwa waqfu kwa ajili ya watu wote, na inatosha idhini ya msimamizi wa waqfu hizo, na kauli iliyo dhahiri ni kutosheka na ada ya watu  ikiwa kufanya kwao kutakupa matumaini ya kuwa ni sehemu ya matumizi ya watu wote, vile vile hali ni hiyo hiyo kwenye matumizi mengine ya vitu hivyo vya waqfu.


KIFUNGU CHA PILI

KUSTANJI

Ni wajibu kuosha sehemu ya kutokea mkojo kwa maji, na inatosha kuosha mara moja japo kuwa kauli ya ahwat ya sunna ni kuosha mara kadhaa, na haitoshelezi kitu kingine tofauti na maji, na sehemu ya haja kubwa ikiwa haja itavuka mahali pake na kutapakaa hapo italazimika kutumia maji pekee kama najisi nyingine, na ikiwa hakikuvuka mahali pake mukallaf anahiari ya kuosha kwa maji hadi kusafike mahali hapo, na kati ya kupangusa kwa  kutumia mawe au kitambaa au mfano wa hivyo kati ya vitu vyenye kuondoa najisi, na maji ni bora zaidi, na kutumia vyote  ndio ukamilifu wa twahara.

Mas'ala 88: Je kupangusa kwa mawe na mfano wa hilo inasababisha kutwahirika mahala hapo au kusamehewa kwenye sala pekee? Katika kupangusa kuna ishkaali, na kauli ya ahwti ni ya pili (  yaani ni sababu ya kusamehewa kwenye sala)

Mas'ala 89: Katika kupangusa huzingatiwa kutumia mawe matatu au mfano wa hayo, au kutumia pande tatu za jiwe moja na mfano wa hilo japo kuwa kuna uwezekano wa kusafika kwa kutumia chini ya mawe matatu, na kama hapakusafika mahala hapo kwa mawe matatu ataongeza mpaka pasafike mahali hapo.

Mas'ala 90: Ni wajibu mawe yatumikayo au mfano wake yawe twahara.

Mas'ala 91: Ni haramu kustanji kwa kutumia vitu vyenye kuheshimiwa, vile vile ni haramu kutumia mifupa na kinyesi. Na lau kama mtu atastanji kwa  kutumia vitu hivyo atazingatiwa kuwa ameasi, na kutwahirika au kusameheka kwa kutumia vitu hivyo kuna ishkaal.

Mas;ala 92: Ni wajibu katika hali ya  kuosha kwa maji kuondoa najisi yenyewe na athari zake kwa maana kuwa kuondoa chembe chembe ndogo ambazo hazionekani na kwa kawaida haziondoki isipokuwa kwa kutumia maji, na si wajibu kuondoa rangi na harufu, na inatosha katika upangusaji  kuondoa najisi yenyewe, na si wajibu kuondoa athari za najisi, na ikiwa haja kubwa itatoka ikiwa na najisi nyingine isiyo kuwa hiyo kama damu au mahali pa haja kubwa pakagusana na najisi nyingine kutoka nje  haitatosheleza kuitwahirisha sehemu hiyo ispokuwa kwa kutumia maji, na lau kama atatia shaka ya kuwa imetwahirika sehemu hiyo au laa atajengea ya kuwa haikutwahirika na hapa atakuwa na hiayari kati ya kutumia maji  mawe na mfano wa vitu viwili hivyo.

KIFUNGU CHA TATU

ADABU ZA KWENDA CHOONI

Ni sunna kwa mwenye kujisaidia haja kubwa kujitenga na watu au kwenda sehemu ya mbali ambayo hatoweza kuonekana, na katika haja ndogo atafute sehemu yenye muinuko, kama ambavyo ni sunna kwake kufunika kichwa na kufunga kitambaa shingoni, na kufunika kicha na nyingo kwa kilemba au kitambaa  kunatosheleza kufunika kichwa, na ni sunna kutanguliza mguu wa kulia wakati wa kutoka, na kufanya istibraa, na kujitegemeza kwenye  mguu wake wa kushoto – wkati wa kukaa- na kupanua mguu wa kulia, na ni makruuhu kujisaidia barabarani, njiani,  chini yamiti ya matunda, na sehemu za kulaaniwa, kama kwenye milango ya majumba na mfano wa sehemu hizo kati ya sehemu ambazo mwenye kujisaidia sehemu hizo anakuwa amejisababishia watu kumlaani, na sehemu zilizo andaliwa kwa ajili ya vituo vya misafara, na kulielekea jua au mwezi kwa utupu wake, na kula na kunywa katika hali ya kujisaidia, na mengineyo kati ya mambo yaliyo tajwa na maulamaa radhi za mwenyezi mungu ziwe juu yao, japo kuthibiti kwa baadhi ya mambo yaliyo tajwa kuwa ni ya sunna au makruuhu kuna ishkaali.

Mas'ala 93: Maji ya kustanjia ni twahara hata kama yamestanjiwa sehemu ya kutokea mkojo ikiwa yatatimia masharti haya yafuatayo:

1- Kuto badilika rangi, ladha na harufu ya maji hayo kwa najisi.

2- Kuto ingiwa na najisi nyingine kutoka nje tofauti na mkojo.

3- Kuto vuka najisi itokayo kwenye sehemu yake ya kawaida.

4- Haja kubwa na ndogo isitoke pamoja na najisi nyingine  kama damu, isipokuwa ikiwa itatoka lakini si yenye kuonekana katika hali hiyo hakuna tatizo.

5- Kusiwe na chembe chembe za haja kubwa zenye kuonekana kwa kauli ya ahwat.

Kwa kukamilika masharti haya maji ya kustanjia yanakuwa ni twahara na yanaweza kutumika kuondolea khabathi, lakini haijuzu kuyatumia kuondolea hadathi wala  kuyatumia kwenye udhu wa sunna na ghusli ya sunna.

KIFUNGU CHA NNE ISTIBRAA

Namna ya kufanya istibraa ya mkojo ni kama ifuatavyo, kwanza uta pangusa kuanzia kwenye makalio (yaani mwanzoni mwa sehemu itokeapo haja kubwa) hadi mwanzoni mwa kiungo cha kiume mara tatu, kisha uta anzia mwanzoni mwa kiungo cha kiume hadi kwenye kichwa cha uume mara tatu, na mwisho utakikamua kichwa mara tatu.

Na faida ya istibraa huonekana pale utakapo  kuhukumiwa kuwa ni twahara unyevu nyevu utokao baada ya kufanya istibraa unao shukiwa kuwa ni mkojo au laa, na umaji maji huo ukitoka si wajibu kutawadha, na lau kama utatoka umaji maji unao shukiwa kuwa ni mkojo kabla ya kufanya istibraa – hata kama mukallaf aliacha kufanya istibraa kutokana na dharura na kutoweza kufanya hivyo- atajengea kuwa ni mkojo, na itawajibika kujitwahirisha kwa kutoka umaji maji huo na  kumlazimu kutawadha.

Na huambatanishwa na istibraa katika faida zilizo tajwa muda wote ambao anayakini kuwa hakuna chembe chembe zilizo bakia kwenye mirija itoayo mkojo, na mwanamke hafanyi istibraa, na umaji maji utokao kwenye sehemu zake za siri unahukumiwa kuwa ni twahara na kuwa hautengui twahara ikiwa haikutambulika kuwa ni mkojo. Ndio ni bora zaidi kwa mwanamke kusubiri kidogo- baada ya kukojoa – na kukohoa kohoa na kujikamua utupu wake (sehemu zake za siri) kwa upana kisha kuiosha kwa maji.

Mas'ala 94: Faida za kufanya istibraa hupatikana katika istibraa hata kama ni kwa kufanywa na mtu mwingine kama mkewe au mtu alie milikiwa (mjakazi au mtumwa).

Mas'ala 95: Ikiwa mukallaf atatia shaka ya kuwa amefanya istibraa au amestanji atajengea kuwa hakufanya hata kama ni kawaida yake kufanya, na ikiwa atatia shaka mtu ambae hakufanya istibraa ya kuwa umetoka umajimaji atajengea kuwa haukutoka hata kama atakuwa anadhania kuwa umetoka umajimaji.

Mas'ala 96: Ikiwa atafahamu ya kuwa amefanya istibraa au amestanji na akatia shaka ya kuwa amefanya istibraa au amestanji sawa sawa au laa atajengea kuwa ni sahihi.

Mas'ala 97: Ikiwa mukallaf atafahamu ya kuwa ametokwa na madhii na hakufahamu ya kuwa madhii hayo yalifuatana na chembe chembve za  mkojo au hapana atajengea kuwa ni twahara hata kama hakufanya istibraa, isipokuwa ikithibiti kuwa ni umajimaji unao tiliwa shaka, na shaka yenyewe iwe katika hali ifuatayo ya kuwa umaji maji huu uliodhihiri je yote ni madhii au  ni mchanganyiko  kati ya madhii na mkojo.

  KITABU TWAHARA (MLANGO WA TWAHARA)

  KATIKA MLANGO HUU KUNA SEHEMU TOFAUTI

  SEHEMU YA KWANZA

  MGAWANYIKO WA MAJI NA HUKUMU ZAKE 

 

NA KATIKA SEHEMU HII KUNA VIFUNGU KADHAA

KIFUNGU CHA KWANZA

MAJI  YAMEGAWANYIKA SEHEMU MBILI

SEHEMU YA KWANZA:

 Maji Mutlaq, hiki ni kitu chenye kutiririka na ambacho huitwa kwa jina la (Maji) bila kuongeza kitu, kama maji yaliyopo kwenye kisima au mto au bahari. Na tusemapo maji ya bahari au maji ya mto au maji ya kisima husema hivyo kwa ajili ya kuyapambanua, si kwa sababu ya kusahihisha matumizi.

SEHEMU YA PILI:

Maji mudhaaf,  ni kitu chenye kutiririka ambacho haifai kuitwa kwa jina la (maji) pekee,  bali huongezewa neno lingine kama ifuatavyo: Maji ya komamanga kwa mfano, au maji ya waridi kwa kutaja jina lililo dhifiwa kwenye tamko maji. Na pengine huitwa (Maji) kwa majazi, kwa sababu hii inafaa kuto tumia neno maji kwenye neno hilo.

KIFUNGU CHA PILI:

 MAJI MUTLAQ (Maji halisi) NA HUKUMU ZAKE

Maji mutlaq yamegawanyika sehemu zifuatazo: 1-Maji yenye kutiririka.  2- Maji ya chemchem yasiyo tiririka. 3- Maji ya kisima. 4- Maji ya mvua.  5- Maji ya kuri moja 6- Maji kidogo (yasiyo fikia kiwango cha kuri moja).

Mas'alal 36: Maji mutlaq na mgawanyiko wake wote kama hayakuingiwa na najisi ni twahara na ni yenye kutwahirisha hadathi na khabathi.

Mas'ala 37:Maji mutlaq na mgawanyiko wake wote  hata maji yenye kutiririka ikiwa yatabadilika na kugeuka moja ya sifa zake tatu kwa kuingiwa na najisi hunajisika, Na sifa hizo ni rangi ladha na harufu. Na maji kidogo yananajisika tu kwa kuingiwa  na najisi.

Mas'ala 38: Ikiwa maji yatabadilika  na ubadilikaji huo haukuwa ni katika moja kati ya sifa zake tatu, rangi ladha na harufu, kama yakibadilika uzito wake  na mfano wa hayo, maji hayo hayata najisika ikiwa hayakubadilika na kuwa maji mudhaafu.

Mas'ala 39: Ikiwa rangi ya maji itabadilika au ladha yake au harufu yake kwa kukaribiana na najisi, kama  mzoga ukiangukia karibu na maji hayo na mzoga huo ukawa ukingoni mwa maji hayo hayatanajisika vile vile.

Mas'ala 40: Ikiwa maji hayakubadilika kwa najisi  maji hayo si najisi, kama yakibadilika kwa kitu kilicho najisika, kama ikiwa  yatabadilika na kuwa ya njano au mekundu kwa kuingiwa na juisi iliyo najisika.

Mas'ala 41: maji hayanajisiki tu kwa kuingiwa na najisi au kubadilika kwa kuingiwa na najisi yenyewe, bali  ikiwa yataingiwa na kitu chenye najisi au kilicho beba sehemu na chembe chembe za najisi, au kitu hicho kina chembe chembe za najisi na maji yale yakabadilika na kugeuka kwa najisi ile, maji hayo yatanajisika pia.

Mas'ala 42: Inatosha kunajisika kwa maji kubadilika kwake kwa sababu ya kuingiwa na najisi hata kama hayakubadilika sifa zake zote, kwa mfano lau kama  maji hayo yatabadilika rangi yake na kuwa rangi ya njano au nyekundu kwa kuingiwa na damu, au yakawa na harufu iliyo kinyume na harufu ya mkojo na haja kubwa kwa kuangukia najisi hizo kwenye maji hayo, maji hayo yatakuwa yamenajisika pia.

KIFUNGU CHA TATU

MAJI  YENYE KUTIRIRIKA  NA HUKUMU ZAKE

Haya ni maji yenye kutiririka na yaliyo ungana na mada ya ardhini au nyingineyo hata kama hayatoki na kuchimbuka ardhini.

Mas'ala 43: Maaul jaariy (maji yenye kutiririka) sawa yawe ni kiasi cha kuri moja au yawe ni kiasi kidogo kuliko kuri, na sawa utiririkaji wake uwe ni wa kuchupa au kunyunyiza,. hayanajisiki kwa kuingiwa na najisi kama hayajabadilika sifa zake.

Na huambatanishwa na maji yenye kutiririka katika hukumu ya kuto najisika kwa kuingiwa na najisi bila kubadilika, maji yote yachimbukayo ardhini hata kama hayatiririki.

Mas'ala 44: Ikiwa maji yenye kutiririka juu ya ardhi bila ya kuwa na asili ichimbukayo ardhini au  yenye kunyunyiza, ikiwa majio hayo yatakuwa ni machache zaidi kuliko kuri ya maji,  hakika maji hayo hunajisika kwa kuingiwa tu na najisi.

Ama ikiwa mukallaf atatia shaka ya kuwa maji hayo yana chimbuko  (mada) au laa kauli yenye nguvu inasema kuwa hayata najisika  maji hayo kwa kuingiwa au kukutana na najisi ikiwa hapo kabla hayakutanguliwa na hali ya kuto kuwa na mada.

Mas'ala 45: Kizingatiwacho katika kuto najisika maji yatiririkayo ni kuungana kwake na mada (asili kama chemchem au kuungana na bomba), kwa mfano lau kama mada au asili ya kutiririka kwa  maji hayo iko juu, na mada  yenye kutiririsha au kunyunyiza maji hayo itakuwa  ni chini ya kuri moja maji hayo yatanajisika, ndio ikiwa sehemu inayo nyunyiza au asili ya maji hayo itagusana na najisi maji hayo hayatanajisika.

Mas'ala 46: Maji yaliyo tuwama na yaliyo ungana na maji yenye kutiririka hukumu yake ni sawa na maji yenye kutiririka katika  hukumu ya kuto najisika kwake kwa kugusana au kuingiwa na najisi au kitu kilicho najisika, kwa mfano hodhi lililo ungana na mto kwa ajili ya umwagiliaji, maji yake hayanajisiki kwa kugusana na najisi, vile vile kingo za mto hata kama maji yake yametuwama na hayatiririki.

Mas'ala 57: Ikiwa baadhi ya sehemu ya maji yenye kutiririka itabadilika na sehemu nyingine isibadilike, sehemu ya maji hayo iliyo ungana na mada hainajisiki kwa kuungana  au kuingiwa na najisi hata kama maji yake ni machache, na upande mwingine hukumu yake ni sawa na hukumu ya maji yaliyo tuwama ikiwa maji ya sehemu hiyo yatabadilika, laa sivyo yatahesabiwa yamenajisika kiwango kilicho badilika pekee, kwa kuungana  yale mengine na mada.

 KIFUNGU CHA NNE

  MAJI  YALIYO  TUWAMA  NA HUKUMU ZAKE

Mas'ala 48: Maji yaliyo tuwama bila kuungana na mada ikiwa kiwango chake hakifikii kuri moja hakika maji hayo yananajisika kwa kuingiwa na najisi, tofauti na ikiwa yanafikia kuri moja, hakika yakiwa ni kuri moja hayanajisiki kwa kuingiwa au kukutana  na najisi isipokuwa yatakapo badilika moja kati ya sifa zake tatu.

Mas'ala 49: Kiwango cha kuri kwa uzito ni sawa na huqqa ya istambuli 280, ama ukubwa wake ni sawa na shibiri 34 kasoro moja ya tatu, na kwa lita ni sawa na lita 377 takriiban.

Mas'ala 50: Maji yakiwa ni chini ya kuri moja hata kama ni kwa kiasi kichache hukumu yake ni sawa na hukumu ya ya maji kidogo.

Mas'ala 51:Ikiwa najisi itaangukia kwenye kuri na haikujulikana ya kuwa imeangukia humo kabla ya kufika kuri au baada ya kukamilika kuri, maji hayo yatahukumiwa kuwa ni twahara, isipokuwa ikiwa itafahamika tarehe ya kuangukia kwake humo na tarehe ya kufikia kwake kuri haikujulikana.

 Mas'ala 52: Ikiwa imefikia kuri lakini haikujulikana ya kuwa ni maji mutlaq (ni maji halisi) au mudhaaf, na yakaingiwa na najisi,  maji hayo hayata hukumiwa kuwa ni najisi, isipokuwa itakapo kuwa  hali yake ya mwanzo ilikuwa ni mudhaaf na kukawa na shaka ya kuwa bado ni mudhafu.

 Na ikiwa kunakuri mbili moja ni mutlaq na nyingine ni mudhaaf, na ikafahamika kuingiwa na najisi moja kati ya kuri hizo mbili  lakini haijulikani kuwa ni ipi kati ya kuri hizo,  zote mbili zitahukumiwa kuwa ni twahara pia.

KIFUNGU CHA TANO

  MAJI YA MVUA NA HUKUMU ZAKE

 Mas'ala 53: Hukumu ya maji ya mvua wakati ikinyesha ni sawa na hukumu ya maji yenye kutiririka, hayata najisika kwa kugusana na najisi ikiwa hayajabadilika moja kati ya sifa zake,  hata kama  mvua hiyo ni kidogo, sawa maji hayo yatiririke kwenye mifereji au juu ya ardhi au laa, la muhimu ni kuthibiti kuwa ni maji ya mvua, na ikiwa yatakusanyika sehemu moja na kikaoshewa ndani  yake kitu kilicho najisika  kitu hicho kitatwahirika hata kama maji yale yatakuwa ni madogo.

Haya yote ni wakati mvua ikiendelea kunyesha, na ikiwa mvua itakatika na kuacha  kunyesha hukumu yake ni sawa na hukumu ya maji yaliyo tuwama.

Mas'ala 54: Nguo iliyo najisika  na zulia lililo najisika ikiwa vitu viwili hivi vitanyeshewa na mvua na maji kuingia ndani ya vitu hivyo basi vitu  hivyo vyote vitatwahirika, na haihitaji kukamua au kuosha kwa mara kadhaa, na ikiwa  maji yatafika kwenye baadhi ya sehemu na hayakuenea sehemu zote itatwahirika sehemu zilizo fikiwa na mvua hiyo  na si vinginevyo. Na hukumu hii inahusika tu ikiwa hakuna najisi yenyewe kwenye vitu hivyo, laa sivyo havitwahiriki isipokuwa vitakapo nyeshewa tena baada ya kuondoka najisi yenyewe kwenye vitu  hivyo.

Mas'ala 55: Ardhi iliyo najisika hutwahirika kwa kunyeshewa na mvua kwa sharti kwamba mvua hiyo iinyeshee moja kwa moja kutoka mawinguni  hata kama ni kwa kupeperushwa na upepo,  ama ikiwa mvua hiyo itanyeshea juu ya kitu kingine – kama ambavyo maji hayo yatatiririkia juu ya ardhi baada ya kuangukia mahali pengine na kuingiwa na najisi- katika hali kama hii haita twahirika.

Ndio  ikiwa mvua hiyo itanyesha juu ya ardhi kisha maji yake yakatiririkia juu ya paa basi sehemu hiyo itatwahirika.

Mas'ala 56: Ikiwa maji ya mvua yataangukia kwenye najisi yenyewe kisha yakadondokea kwenye kitu kingine, kitu hicho hakita najisika ikiwa maji hayo hayakuwa na chembe chembe za najisi ndani yake na hayakubadilika kwa najisi.

Mas'ala 57: Mchanga ulio najisika hutwahirika kwa kunyeshewa na mvua ikiwa mvua hiyo itaingia hadi ndani ya mchanga huo na kubadilika kuwa udongo.

Mas'ala 58: Jamvi lililo najisika linatwahirika kwa kunyeshewa na mvua, vilevile zulia lililo tandikwa juu ya ardhi, na ardhi iliyopo chini ya zulia hilo ikiwa ni najisi hutwahirika  ikifikiwa na maji ya mvua. Ndio ikiwa jamvi au zulia havikuwa juu ya ardhi au kukawa na utengano, hapo kuna ishkaali katika hukumu ya kutwahirika kwake kwa kunyeshewa na mvua, kwanza kwa kunyeshea mvua juu ya jamvi au zulia kisha maji hayo yakadondokea juu ya ardhi.

Mas'ala 59: Chombo ambaacho nbi  najisi kinatwahirika ikiwa maji ya mvua yatafika sehemu zote zenye najisi katika chombo hicho isipokuwa ikiwa kimenajisika kwa kuliwa na mbwa ndani yake, katika hali kama hiyo kutwahirika chombo hicho kwa kunyeshewa na mvua tu bila ya kukisugua au kukiosha kwa mchanga kuna ishkaali, lakini ikiwa kitanyeshewe na mvua baada ya kukisugua au kukiosha kwa mchanga wakati huo kitatwahirika bila ya kuhitajia kuosha mara kadhaa.

   KIFUNGU CHA SITA

MAJI YA BAFUNI NA HUKUMU YAKE

Mas'ala 60: Maji ya bafuni ni sawa na maji yenye kutiririka kwa sharti kuwa yawe yameungana na mada, kwa mfano maji yaliyoko kwenye mahodhi madogo ikiwa yataungana na mada hayanajisiki kwa kuingiwa na najisi ikiwa maji yaliyoko kwenye hodhi pekee au kwa kuyaunganisha na yaliyomo kwewnye mada yanafikia kuri.

Mas'ala 61:Ikiwa maji yaliyomo kwenye mahodhi madogo yatanajisika yanatwahirika kwa kuungana na mada kwa sharti kwamba maji ya mada yawe ni kuri na yachanganyike pia.

KIFUNGU CHA SABA

  MAJI YA KISIMA NA  HUKUMU  ZAKE

Mas'ala 62: Hukumu ya maji ya kisima yenye kuchimbuka ardhini ni sawa na hukumu ya maji yenye kutiririka katika hukumu ya kuto najisika isipokuwa kwa kubadilika moja kati ya sifa zake, sawa yawe ni kiasi cha kuri moja au chini ya hapo, na ikiwa yatabadilika  kisha ubadilikaji huo ukaondoka na kutoweka wenyewe maji hayo yatatwahirika kwa sababu yana mada na yamechanganyika na maji yatokayo kwenye mada kama chemchem. Ama yakiwa hayana mada yenye kuchimbuka basi itazingatiwa kiasi cha kuri katika hali ya  kutonajisika kwake hata kama kitaitwa kisima, kama mfano wa visima ambavyo hukusanyika ndani yake maji yasiyo chimbuka  ardhini.

Mas'ala 63: Maji  najisi yaliyo tuwama sawa maji hayo yawe ni kuri au  kidogo  yanatwahirika kwa kuungana na maji ya kuri yaliyo twahara au kwa kuungana na maji yenye kutiririka au maji yenye kuchimbuka ardhini hata kama hayatiririki na kuchanganyika na maji hayo, na pia hutwahirika kwa kukutana na kuchanganyika na maji ya mvua,  na kauli ya ahwat ni kuwa kutazingatiwa kuchanganyika kwa maji hayo.

Mas'ala 64: Birika lililo jazwa maji yaliyo najisika ikiwa litazamishwa kwenye hodhi  hutwahirika baada ya kuchanganyika maji hayo, na si wajibu kuyamwaga maji yake na kuliosha birika hilo.

KIFUNGU CHA NANE

MAJI YALIYO TUMIKA YAKIWA NI MACHACHE

Mas'ala 65: Maji yaliyo tumika  kutawadhia ni twahara na yanatwahirisha hadathi na khabathi, vile vile maji yaliyo tumika katika ghusli ya sunna, ama maji yaliyo tumika katika ghusli ya hadathi kubwa pamoja na kuwa mwili hutwahirika hakuna ishkaali katika utwahara wa maji hayo na juu  uwezekano wa kuyatumia kuondolea khabathi, na kauli yenye nguvu zaidi ni kuwa inajuzu kuyatumia kuondolea hadathi pia japokuwa kauli ya ahwati ni kuwa nivema kujiepusha na maji hayo.

Ama maji yaliyo tumika kuondoa khabathi tofauti na maji yaliyo tumika kustanji haijuzu kuyatumia katika udhu na ghusli, na kauli yenye nguvu zaidi ni kuwa maji yatumikayo kuondolea najisi yenyewe ni najisi, bali hata maji yaliyo tumiwa kuoshea yasiyo ondoa najisi, ama  maji ya kustanjia  hukumu yake itafuatia.

Mas'ala 66: Hakuna ishkaali katika matone ambayo hudondokea kwenye chombo wakati wa kuosha hatakama tutasema ya kuwa haijuzu kutumia maji yaliyo oshewa hadathi kubwa. Na maji yanayo bakia kwenye nguo baada ya kukamuliwa nguo hiyo ni twahara, ikiwa maji hayo yatatoka baada ya nguo hiyo kukamuliwa hayata ambatanishwa na hukumu ya maji yaliyo oshewa.

 Na mkono hutwahirika kwa kufuata kitu kinacho twahirishwa baada ya kukitwahirisha kitu hicho, kwa hivyo hakuna haja ya kuiosha mikono hiyo, pia chombo ambacho hutumika kuoshea nguo na mfano wa hivyo.

KIFUNGU CHA TISA

  HUKUMU YA MAJI  YENYE  KUTILIWA  SHAKA

Mas'ala 67: Maji ambayo hutiliwa shaka ya kuwa ni najisi au twahara maji hayo ni twahara ikiwa haikujulikana ya kuwa hapo kabla yalikuwa ni najisi, ama maji ambayo hutiliwa shaka ya kuwa ni mutlaq au hapana hayahukumiwi maji hayo kuwa ni mutlaq isipokuwa ikiwa hapo kabla yalikuwa ni mutlaq.

Ndio, ikiwa maji hayo ni kuri moja na yakaingiwa na najisi hayatahukumiwa kuwa ni najisi isipokuwa ikiwa hapo kabla yalikuwa ni maji mudhaaf, ama maji ambayo yanatiliwa shaka ya kuwa ni mubaha au hapana (maji halali) maji hayo hukumu yake ni kuwa ni mubaha, aisipokuwa ikiwa hapo kabla yalikuwa ni milki ya mtu mwingine au yalikuwa katika milki ya mtu mwingine ambae kuna ihtimali kuwa ni maji yake.

Mas'ala 68: Ikiwa mukallaf atafahamu kwa sura ya ujumla ya kuwa mojawapo  kati ya vyombo viwili ni najisi  na kingine ni twahara haitajuzu kutumia chombo moja wapo kuondolea khabathi au hadathi.

Mas'ala 69: Chombo kinacho shukiwa kuwa sehemu moja wapo ya chombo hicho imenajisika  hakita hukumiwa kuwa ni najisi isipokuwa  hali ya sehemu  hiyo ya hapo kabla itajulikana kuwa ilikuwa ni najisi, lakini kauli ya ahwat inasema kuwa ni bora kujiepusha na utumiaji wa chombo hicho.

Mas'ala 70: Ikiwa maji mutlaq yatafanana na mudhaaf itajuzu kuyatumia maji hayo kuondolea khabathi kwa kutumia moja wapo kati ya maji hayo na kuoshea kwa kutumia maji mengine, vile vile katika kuondoa hadathi.

Mas'ala 71: Ikiwa itafahamika kwa sura ya ujumla ya kuwa maji haya ima ni najisi au

ni mudhaaf inajuzu kuyanywa maji hayo, lakini haijuzu kuyatumia kutawadhia, vile vile ikiwa itajulikana ya kuwa ima maji hayo ni mudhaaf au ni maghsuub (ya kunyang'anya).

Ama ikiwa itajulkikana ya kuwa maji hayo ni najisi au ni ya kunyang'anya haitajuzu kuyanywa, kama ambavyo  haitajuzu kuyatumia kutawadhia.

Mas'ala 72: Ikiwa sehemu au pande zitiliwazo shaka au zenye shubha hazijulikani kidhati, katika hali kama hii inajuzu kuyatumia maji hayo bila kipingamizi.

KIFUNGU CHA KUMI

HUKUMU ZA  MAJI  MUDHAAF

Mmas'ala 73: Maji mudhaaf, kama maji ya uwa waridi ni twahara ikiwa hayakuingiwa na najisi, lakini maji hayo si yenye kutwahirisha hadathi,  vilevile si yenye kutwahirisha khabathi hata katika hali ya dharura.

Mas'ala 74: Maji mudhaaf yana najisika kwa kuingiwa tu na najisi sawa yawe mengi au kidogo, isipokuwa yakiwa ni yenye kuchupa  kwa nguvu juu ya najisi, hata kama yanatoka chini kwenda juu kama maji yatokayo kwenye bomba lenye kunyunyizia  na mfano wa hiyo, katika hali kama hii itahukumiwa kuwa ni najisi sehemu ile tu iliyo gusana na najisi, na haivuki na kuelekea juu.

Mas'ala 75: Ikiwa maji mudhaaf yatanajisika hayatatwahirika isipokuwa kwa kuyaweka kwenye kuri  au kwenye maji yenye kutiririka na kutoweka hali ya kuwa kwake maji mudhafu. Na kutwahirika  kwa maji mudhaaf  yaliyo najisi kwa kuyachemsha ( au kuongeza kiwango cha maji hayo) kuna ishkaali.

 

 KIFUNGU CHA KUMI NA MOJA

MABAKI YA CHAKULA

Mas'ala 76: Mabaki ya chakula yote ni twahara isipokuwa mabaki ya mnyama alie najisi (najisul aini) kama mbwa Nguruwe na mushrik (kafir) , hakika mabaki yao ni najisi.

Mas'ala 77: Nimakuruhu kula mabaki ya mnyama asie liwa isipokuwa mabaki ya Muumini na paka kutokana na kauli ya baadhi ya mujtahidiin.

SEHEMU YA PILI: HUKUMU ZA CHOONI

  PIA KUNA VIFUNGU KADHAA

  KIFUNGU CHA KWANZA

  HUKUMU ZA KWENDA CHOONI

Mas'ala 78: Ni wajibu wakatio mtu anapokwenda chooni au katika hali ya kujisaidia haja kubwa bali hata katika hali nyingine tofauti kusitiri uchi (sehemu za siri) – nazo ni sehemu ya mbele na nyuma na peke mbili- kwa muonaji mwenye kuheshimiwa, isipokuwa mtoto na mwenda wazimu wasio weza kupambanua, na mke na mume na alie milikiwa kwa mmiliki wake na alie halalishwa kwa alie halalishiwa, hakika kwa watu hawa inajuzu kwa kila mmoja wao kuangalia uchi wa mwenziwe.

Mas'ala 79: Hakuna tofauti katika uharamu wa kuangali kati ya uchi wa  Muislaam au kafiri kutokana na kauli ya ahwat.

Mas'ala 80: Si wajibu kusitiri mapaja mawili wala matako wala nywele ziotazo pembezoni mwa sehemu za siri (mavuzi). Ndio, ni sunna kusitiri sehemu zilizoko kati ya kitovu na magoti.

Mas'ala 81: Haijuzu kuangalia uchi wa mtu mwingine kwa kutumia kioo na mfano wa hicho, wala kwa kutumia kioo cha kujitizamia  na wala haijuzu kuangalia kwa kutumia maji yaliyo safi. 

Mas'ala 82: Ikiwa mtu itamlazimu kuangalia uchi wa mtu mwingine kama katika hali ya kumtibu mgonjwa, kauli ya ahwat ni kuwa ataangalia kupitia kioo kilicho wekwa mbele yake ikiwa kufanya hivyo kutatosheleza na kuondoa dharura hiyo, laa sivyo hakuna tatizo  kuangalia.

Mas'ala 83: Ni haramu kwa mwenye kujisaidia haja kubwa – wakati wa kujisaidia- kuelekea Qibla na kukipa mgongo Qibla kwa kuielekeza sehemu ya mbele ya mwili wake  kwenye Qibla hata kama uchi wake atauelekeza sehemu au upande mwingine tofauti na sehemu hizo mbili, na kauli ya ahwat ni kuwa ataacha  kukielekezea  uchi wake pekee hata kama sehemu za mbele za mwili wake zitaelekea  sehemu hizo mbili, na makusudio ya sehemu za mbele za mwili ni kifua tumbo na magoti mawili, na ikiwa italazimika kufanya moja wapo atakuwa na hiari japokuwa kauli ya ahwat ni kuwa atakipa mgongo, na akiwa itamlazimu kufanya kitendo kimoja wapo  kati ya mambo mawili hayo na kuto jisitiri pamoja na kuwepo muangaliaji mwenye kuheshimiwa itawajibika kwake kujisitiri.

Mas'ala 84: Kauli yenye nguvu ni kuwa si haramu kukielekea au kukipa mgongo kibla katika hali ya kufanya istibraa na katika hali ya kustanji japo kuwa kutofanya hivyo ni ahwat (bora zaidi). Ndio ikiwa atafahamu ya kuwa mkojo utatoka  kwa kufanya istibraa kauli ya ahwat ni kuwa itawajibika kuacha kukielekea au kukipa mgongo Qibla.

Mas'ala 85: Lau kama mukallaf atapatwa na shubha katika kukipambanua Qibla hukumu ya kutumia dhanna haiko mbali pamoja na kuto kuwepo uwezekano wa kukitafuta na kufanya uchunguzi wa sehemu ya Qibla, na ikiwa kuichelewesha sala kutamsababishia matatizo.

Mas'ala 86: Ni haramu kujisaidia haja kubwa kwenye milki ya mtu mwingine isipokuwa kwa idhini yake, vile vile ni haramu kujisaidia kwenye makaburi ya waumini ikiwa kufanya hivyo ni kuvunja heshima yao.

Mas'ala 87: Ni haramu kujisaidia haja kubwa kwenye mashule na mfano wa hayo ikiwa haikufahamika kuwa sehemu hizo zimewekwa waqfu kwa ajili ya watu wote, na inatosha idhini ya msimamizi wa waqfu hizo, na kauli iliyo dhahiri ni kutosheka na ada ya watu  ikiwa kufanya kwao kutakupa matumaini ya kuwa ni sehemu ya matumizi ya watu wote, vile vile hali ni hiyo hiyo kwenye matumizi mengine ya vitu hivyo vya waqfu.

KIFUNGU CHA PILI

KUSTANJI

Ni wajibu kuosha sehemu ya kutokea mkojo kwa maji, na inatosha kuosha mara moja japo kuwa kauli ya ahwat ya sunna ni kuosha mara kadhaa, na haitoshelezi kitu kingine tofauti na maji, na sehemu ya haja kubwa ikiwa haja itavuka mahali pake na kutapakaa hapo italazimika kutumia maji pekee kama najisi nyingine, na ikiwa hakikuvuka mahali pake mukallaf anahiari ya kuosha kwa maji hadi kusafike mahali hapo, na kati ya kupangusa kwa  kutumia mawe au kitambaa au mfano wa hivyo kati ya vitu vyenye kuondoa najisi, na maji ni bora zaidi, na kutumia vyote  ndio ukamilifu wa twahara.

Mas'ala 88: Je kupangusa kwa mawe na mfano wa hilo inasababisha kutwahirika mahala hapo au kusamehewa kwenye sala pekee? Katika kupangusa kuna ishkaali, na kauli ya ahwti ni ya pili (  yaani ni sababu ya kusamehewa kwenye sala)

Mas'ala 89: Katika kupangusa huzingatiwa kutumia mawe matatu au mfano wa hayo, au kutumia pande tatu za jiwe moja na mfano wa hilo japo kuwa kuna uwezekano wa kusafika kwa kutumia chini ya mawe matatu, na kama hapakusafika mahala hapo kwa mawe matatu ataongeza mpaka pasafike mahali hapo.

Mas'ala 90: Ni wajibu mawe yatumikayo au mfano wake yawe twahara.

Mas'ala 91: Ni haramu kustanji kwa kutumia vitu vyenye kuheshimiwa, vile vile ni haramu kutumia mifupa na kinyesi. Na lau kama mtu atastanji kwa  kutumia vitu hivyo atazingatiwa kuwa ameasi, na kutwahirika au kusameheka kwa kutumia vitu hivyo kuna ishkaal.

Mas;ala 92: Ni wajibu katika hali ya  kuosha kwa maji kuondoa najisi yenyewe na athari zake kwa maana kuwa kuondoa chembe chembe ndogo ambazo hazionekani na kwa kawaida haziondoki isipokuwa kwa kutumia maji, na si wajibu kuondoa rangi na harufu, na inatosha katika upangusaji  kuondoa najisi yenyewe, na si wajibu kuondoa athari za najisi, na ikiwa haja kubwa itatoka ikiwa na najisi nyingine isiyo kuwa hiyo kama damu au mahali pa haja kubwa pakagusana na najisi nyingine kutoka nje  haitatosheleza kuitwahirisha sehemu hiyo ispokuwa kwa kutumia maji, na lau kama atatia shaka ya kuwa imetwahirika sehemu hiyo au laa atajengea ya kuwa haikutwahirika na hapa atakuwa na hiayari kati ya kutumia maji  mawe na mfano wa vitu viwili hivyo.

KIFUNGU CHA TATU

ADABU ZA KWENDA CHOONI

Ni sunna kwa mwenye kujisaidia haja kubwa kujitenga na watu au kwenda sehemu ya mbali ambayo hatoweza kuonekana, na katika haja ndogo atafute sehemu yenye muinuko, kama ambavyo ni sunna kwake kufunika kichwa na kufunga kitambaa shingoni, na kufunika kicha na nyingo kwa kilemba au kitambaa  kunatosheleza kufunika kichwa, na ni sunna kutanguliza mguu wa kulia wakati wa kutoka, na kufanya istibraa, na kujitegemeza kwenye  mguu wake wa kushoto – wkati wa kukaa- na kupanua mguu wa kulia, na ni makruuhu kujisaidia barabarani, njiani,  chini yamiti ya matunda, na sehemu za kulaaniwa, kama kwenye milango ya majumba na mfano wa sehemu hizo kati ya sehemu ambazo mwenye kujisaidia sehemu hizo anakuwa amejisababishia watu kumlaani, na sehemu zilizo andaliwa kwa ajili ya vituo vya misafara, na kulielekea jua au mwezi kwa utupu wake, na kula na kunywa katika hali ya kujisaidia, na mengineyo kati ya mambo yaliyo tajwa na maulamaa radhi za mwenyezi mungu ziwe juu yao, japo kuthibiti kwa baadhi ya mambo yaliyo tajwa kuwa ni ya sunna au makruuhu kuna ishkaali.

Mas'ala 93: Maji ya kustanjia ni twahara hata kama yamestanjiwa sehemu ya kutokea mkojo ikiwa yatatimia masharti haya yafuatayo:

1- Kuto badilika rangi, ladha na harufu ya maji hayo kwa najisi.

2- Kuto ingiwa na najisi nyingine kutoka nje tofauti na mkojo.

3- Kuto vuka najisi itokayo kwenye sehemu yake ya kawaida.

4- Haja kubwa na ndogo isitoke pamoja na najisi nyingine  kama damu, isipokuwa ikiwa itatoka lakini si yenye kuonekana katika hali hiyo hakuna tatizo.

5- Kusiwe na chembe chembe za haja kubwa zenye kuonekana kwa kauli ya ahwat.

Kwa kukamilika masharti haya maji ya kustanjia yanakuwa ni twahara na yanaweza kutumika kuondolea khabathi, lakini haijuzu kuyatumia kuondolea hadathi wala  kuyatumia kwenye udhu wa sunna na ghusli ya sunna.

KIFUNGU CHA NNE

 ISTIBRAA

Namna ya kufanya istibraa ya mkojo ni kama ifuatavyo, kwanza uta pangusa kuanzia kwenye makalio (yaani mwanzoni mwa sehemu itokeapo haja kubwa) hadi mwanzoni mwa kiungo cha kiume mara tatu, kisha uta anzia mwanzoni mwa kiungo cha kiume hadi kwenye kichwa cha uume mara tatu, na mwisho utakikamua kichwa mara tatu.

Na faida ya istibraa huonekana pale utakapo  kuhukumiwa kuwa ni twahara unyevu nyevu utokao baada ya kufanya istibraa unao shukiwa kuwa ni mkojo au laa, na umaji maji huo ukitoka si wajibu kutawadha, na lau kama utatoka umaji maji unao shukiwa kuwa ni mkojo kabla ya kufanya istibraa – hata kama mukallaf aliacha kufanya istibraa kutokana na dharura na kutoweza kufanya hivyo- atajengea kuwa ni mkojo, na itawajibika kujitwahirisha kwa kutoka umaji maji huo na  kumlazimu kutawadha.

Na huambatanishwa na istibraa katika faida zilizo tajwa muda wote ambao anayakini kuwa hakuna chembe chembe zilizo bakia kwenye mirija itoayo mkojo, na mwanamke hafanyi istibraa, na umaji maji utokao kwenye sehemu zake za siri unahukumiwa kuwa ni twahara na kuwa hautengui twahara ikiwa haikutambulika kuwa ni mkojo. Ndio ni bora zaidi kwa mwanamke kusubiri kidogo- baada ya kukojoa – na kukohoa kohoa na kujikamua utupu wake (sehemu zake za siri) kwa upana kisha kuiosha kwa maji.

Mas'ala 94: Faida za kufanya istibraa hupatikana katika istibraa hata kama ni kwa kufanywa na mtu mwingine kama mkewe au mtu alie milikiwa (mjakazi au mtumwa).

Mas'ala 95: Ikiwa mukallaf atatia shaka ya kuwa amefanya istibraa au amestanji atajengea kuwa hakufanya hata kama ni kawaida yake kufanya, na ikiwa atatia shaka mtu ambae hakufanya istibraa ya kuwa umetoka umajimaji atajengea kuwa haukutoka hata kama atakuwa anadhania kuwa umetoka umajimaji.

Mas'ala 96: Ikiwa atafahamu ya kuwa amefanya istibraa au amestanji na akatia shaka ya kuwa amefanya istibraa au amestanji sawa sawa au laa atajengea kuwa ni sahihi.

Mas'ala 97: Ikiwa mukallaf atafahamu ya kuwa ametokwa na madhii na hakufahamu ya kuwa madhii hayo yalifuatana na chembe chembve za  mkojo au hapana atajengea kuwa ni twahara hata kama hakufanya istibraa, isipokuwa ikithibiti kuwa ni umajimaji unao tiliwa shaka, na shaka yenyewe iwe katika hali ifuatayo ya kuwa umaji maji huu uliodhihiri je yote ni madhii au  ni mchanganyiko  kati ya madhii na mkojo.