AL-AHKAAMUL WAADHIHA  
HIZI NI FAT’WA ZA KIONGOZI WA
KIDINI AYATULLAHI AL-UDHMA ALHAJI SHEKH MOHAMMAD FAADHIL LANKARAANIY
 ( Mundu amrefushie umri) 
 TAQLIID
Mas’ala 1: Ni wajibu kwa kila
mukallafu ambae hajafikia daraja ya ijtihadi imma kuwa muqallid (kumfua
mujitahidi Fulani katika mas’ala ya kisheria) au kufanya ihtiyaati katika ibada
zake zote na utendaji kazi wake (kama biashara) na mengineyo na katika matendo
yake mengine anayo paswa kuyafanya au kuyaacha. Mas’ala 2: Matendo ya mtu wa
kawaida ayafanyayo bila kufanya taqliid au ihtiyaat hayatoshelezi  kisheria
maadamu haijulikani ya kuwa yako sambamba na ukweli au uhakika wa kisheria au
yako sambamba na fat’wa za Mujitahid ambae ilikuwa ni wajibu kwake kumfuata
katika utendaji wake. Mas’ala 3: Taqliidi ni kazi au
tendo lifanyikalo kwa kutegemea kauli ya Mujitahidi Fulani. Kwa hivyo basi
haijuzu na haifai kumfuata au kufanya taqliid ya mtu asie kuwa Mujtahidi. Na
niwajibu kwa mtu asie kuwa Mujtahidi kufanya taqliid ikiwa hakuweza kufanya
ihtiyaat. Mas’ala 4: Kauli yenye nguvu ni
kwamba inawezekana kutosheka tu na kufanya ihtiyaati katika uwanja wa utendaji
au katika matendo hata kama kufanya hivyo italazimu kurudia tendo hilo au mukallaf akaweza kufanya ijtihadi au taqliid. Mas’ala 5: Ni wajibu kufanya
uchunguzi na kumtafuata Mujtahidi alie kuwa Aalam (mwenye elimu zaidi kati ya
Mamujtahidi) ikiwa kuna uwezekano wa kufanya hivyo, kutokana na wajibu wa
kumfuata yeye au kufanya taqlidi yake mahala ambamo kuna ihtimali ya
kutofautiana Mamujitahidi kutokana na kauli iliyo na nguvu zaidi.  Na makusudio ya Aaalam ni mwenye
maarifa zaidi ya kanuni na dalili za mas’ala na mwenye kufahamu na kuelewa
zaidi kuliko wenziwe na mwenye kufahamu vyema habari, na mzuri zaidi katika
kufahamu hadithi, na kwa ufupi ni kuwa Aalam ni yule ambae ni mwenye uwezo
mzuri zaidi wa kufanya istinbaat ( uchambuzi na utungaji wa sheria). Na Marejeo
ya kumuainisha na kumthibitisha pia kumfahamu ni kwa ahlul khibrah wataalam wa
mambo hayo na wenye ujuzi wa istimbati na utungaji wa sheria. Mas’ala 6: Hufahamika kuwa huyu
ni mjuzi zaidi kutokana na elimu ya kimaumbile au kitu chochote chenye nafasi kama hiyo kati ya elimu za kawaida au vitu vya kawaida viwezavyo kujulisha hali hiyo, au
kwa kutumia vithibitisho na dalili zisizo pingika au kupingwa, au kwa kuenea
habari ziletazo matumaini na yakini. Mas’ala 7: Ikiwa kutakuwa na
Mamujitahidi wawili na haikuwezekana kupata ujuzu au dalili (uthibitisho) wa
yupi alie mjuzi zaidi kati yao wawili, ikiwa kutakuwa na ihtimali ya kuwa mmoja
wapo ambae ni maalum ni mjuzi zaidi  basi hapo itawajibika kumfuata yeye
(kufanya taqlidi yake). Mas’ala 8: Ni sharti Mujtahidi
awe na masharti yafuatayo, awe baaligh (balee) mwenye akili timamu, awe muumini
na muadilifu na awe mwanaume na awe hai, kwa hivyo basi haijuzu kufanya
taqliidi ya maiti kwa mara ya kwanza, na awe amezaliwa kwanjia ya ndoa halali
(Twaharatul mawlid), na awe ni mwenye ujuzi zaidi, na kauli ya ahwat ni kuwa
asiwe ni mwenye kuipenda dunia (asiwe mwenye kufuata mambo ya kidunia)  
Mas’ala 9: Makusudio ya uadilifu
ni kuwa awe na uwezo wa kinafsi wa kutekeleza mambo ya wajibu na kuacha
madhambi  hasa mambo makubwa yaliyo haramishwa, na  utendaji wa mambo ya wajibu
na kuacha ya haramu nje huthibiti kwa kuwepo uwezo wa kinafsi na kupitia murua
wa mtu. Na uadilifu hujulikana na kufahamika kwa husnudh- dhaahir ( kuwa na
dhahiri nzuri asie sifika kwa maovu), na huthibiti kwa ushahidi wa watu wawili
waadilifu na kwa kuenea habari zitoazo ujuzi au yakini na matumaini. Mas’ala 10: Ikiwa Mujtahidi
atatokewa na jambo ambalo litamfanya akose sharti moja wapo kati ya masharti
hayo  yaliyo tangulia itakuwa no wajibu kwa muqallid kuhamia kwa Mijtahidi
mwingione. Mas’ala 11: Ikiwa mukallaf
atafanya taqliid na kumfuata mtu ambae hakuwa ametimiza masharti  na ukapita
muda Fulani akifanya taqlidi yake atakuwa kama yule ambae hakufanya taqlidi
asilan, ama ikiwa matendo yake aliyo yafanya yatakuwa sambamba na uhakika na
ukweli wa kisheria au yako sambamba na fat’wa za Mujtahidi ambae ilikuwa ni
wajibu kufanya taqlidi yake (ilikuwa ni wajibu kumfuata) wakati akifanya
matendo hayo basi matendo hayo ni sahihi, laa sivyo matendo yake sio  sahihi.  Mas’ala 12: Ikiwa mukallaf
atamuqallid Mujtahidi ambae anaruhusu na kujuzisha kubakia kwenye taqliid ya 
Mujtahidi alie kufa, kisha Mujtahidi huyo akafa haijuzu kubakia kwenye taqlidi
yake hasa kwenye mas’ala haya, bali ni wajibu kurudi na kurejea kwa alie hai
ambae ni Aaalam (mjuzi zaidi) katika mas’ala ya kujuzu kubakia kwa alie kufa au
hapana. Mas’ala 13: Haijuzu kufanya
taqliidi ya maiti (kumfuata Mujtahidi alie kufa) kwa mara ya kwanza, lau kama
mukallaf atamfuata Mujtahidi alie hai kisha akafariki inajuzu kubakia kwenye
taqlidi yake moja kwa moja bila pingamizi ikiwa watalingana kielimu kati ya
alie kufa na yule alie hai, na lau kama alie kufa ni mjuzi zaidi itajuzu
kubakia kwake, na katika mas’ala hayo hakuna tofauto kati ya mtu alie fanya
matendo kwa mujibu wa fat’wa zake au mwingine. Mas’ala 14: Ikiwa kutakuwa na
Mamujitahidi wawili walio lingana kwenye elimu inajuzu kwa mukallaf kumfuata
yeyote kati ya wawili hao na inajuzu kwake baadhi ya mas’ala kuchukua kwa
Mujtahidi huyo na mengine kwa Mujtahidi mwingine. Ama ikiwa mmoja wao ni mwenye
bora zaidi kuliko mwingine katika uadilifu au uchamungu au mfano wa hayo kauli
ya ahwat ya wajibu ni kuwa atamchagua huyo. Mas’ala 15: Inajuzu kuhama baada
ya kuwa mukallaf amefanya taqliid kutoka kwa Mujtahidi alie hai kwenda kwa
Mujtahidi mwingine alie hai na ambae analingana nae kielimu na ni wajibu kuhama
ikiwa wa pili ni mjuzi zaidi.  Mas’ala 16: Njia za kufahamu
fat’wa za Mujtahidi ni kama zifuatazo: 
1- Kusikia kwa Mujitahidi akisema yeye mwenyewe. 
2- Kuambiwa na watu wawili waadilifu, na haitoshi kutosheka na habari za
mtu mmoja muadilifu (yaani kutosheka na habari za mtu mmoja kuna ishkaali),
isipokuwa ikiwa habari yake itatupa matumaini na yakini. 
3- Kuwepo kwa fat’wa kwenye risalatul amaliyyah (kitabu chake cha fat’wa)
ikiwa kimeandikwa na yeye mwenyewe au kwa khati yake, au kuzielewa fat’wa zake
zote. Mas’ala 17: Ikiwa mtu atanukuu kimakosa fat’wa ya
Mujtahidi ni wajibu kwake kuwatangazia walio jifunza kwake,  vilevile  ni
wajibu juu ya Mujtahid kutangaza ikiwa atakosea katika kuibainisha fat’wa yake. Mas’ala 18: Ikiwa mtu atanukuu
fat’wa ya Mujtahidi ikiwa sahihi, kisha rai ya Mujtahidi ikabadilika kuhusiana
na fat’wa hiyo au katika mas’ala hayo kutokana na kauli ya ahwati ni kuwa
niwajibu kwa mtu alie nukuu kumtangazia alie sikia kutoka kwake fat’wa ya
mwamzao.  Mas’ala 19: Ikiwa watu wawili
walio nukuu fat’wa watapingana au dalili mbili zikapingana katika kunukuu
fat’wa ya Mujtahidi, mwenye kunukuu na dalili hizo zitaporomoka yaani
hazitakuwa na maana. Na ikiwa alienukuu atapingana na alie sikia kutoka kwa
Mujtahidi mwenyewe atatangulizwa na kupewa kipaumbele alie sikia.Ama ikiwa
atapingana alie sikia au alie nukuu kwa kutoa kitabu cha fat’wa za Mujtahi yule
hapo kitatangulizwa kitabu chake cha fat’wa ikiwa kitabu hicho kimeandikwa kwa
hati yake au ikiwa ni mwenye kuyajua yote yaliyomo kwenye kitabu hicho
kiukamilifu. Mas’ala 20: Muqallid (mwenye
kumfuata Mujtahidi) anayo hiari kati ya kufanya matendo kulingana na ihtiyaati
ya Mujtahidi ambae ni Aalam (mjuzi zaidi)- ikiwa hakuwa na fat’wa kwenye
mas’ala fulani- na kati ya kurejea kwa mwingine, na hapo ata angaliwa mjuzi
zidi kuliko mwingine. Mas’ala 21: Ikiwa Muqallid
atakuwa na shaka juu ya kufariki kwa Mujtahidi au kubadilika rai yake au
kutokea mambo ambayo hayajuzishi kumfuata au kumfanyia taqliid inajuzu kwa mtu
huyo kubakia kwa Mujtahidi huyo mpaka hali yake ibainike vizuri. Mas’ala 22: Hukumu ya Al-haakim
alie timiza masharti haijuzu kuipinga hata kama ni Mujtahidi mwingine, ispokuwa
ikiwa litabainika kosa lake kwenye hukumu hiyo. Mas’ala 23: Ni wajibu kwa mtu wa
kawaida katika muda mbao bado anafanya uchunguzi wa kumtafuta Mujtahidi au
aliekuwa Aalam kufanya ihtiyaati kwenye matendo yake. Mas’ala 24: Ikiwa mukallaf
atafahamu ya kuwa yeye alikuwa akifanya ibada zake bila kufuata fat’wa za
Mujtahidi yaani hakuwa akifanya taqliid kwa muda kadhaa na hakuweza kufahamu
kiasi cha muda huo, ikiwa atafahamu namna zilivyo kuwa zikifanyika ibada zile
na akafahamu ya kuwa zilikuwa sambamba na uhakika wa kisheria au fat’wa za
Mujtahidi ambae ndie aliepewa jukumu la kurejelewa, hapo hakutakuwa na jukumu
lolote juu yake, laa sivyo itamuwajibikia kufanya kadhaa au kulipa kiwango
ambacho anayakini nacho ikiwa kukhalifu huko kunamlazimu kulipa kadhaa
kulingana na mtizamo au rai ya Mujtahid, na kauli ya ahwat ya sunna ni kuwa
atalipa  na kufanya kadhaa kiwango ambacho anafahamu yakuwa kwa kufanya hivyo
jukumu lake litakuwa limemuondokea (baraa atudhimmah). Mas’ala 25: Ikiwa utapita muda
tangu muqallid awe baaligh ( balee), na akaingiwa na shaka baadae ya kuwa
matendo yake alikuwa akiyafanya kwa kumfuata Mujtahidi au kwa kufanya taqliid
sahihi au laa,  inajuzu kwake kuyajengea matendo yake yaliyo tangulia  kuwa ni
sahihi, ama matendo yake yafuatayo ni wajibu juu yake kuyasahihisha kwa wakati
huo kwa kufanya taqliid. Mas’ala 26: Ikiwa rai ya
Mujtahidi itabadilika  wakati huo haijuzu kwa muqallid kubakia kwenye rai yake
ya mwanzo ikiwa rai hiyo haiwafikiani na ihtiyaat, laa sivyo itajuzu kubakia
kwake kwa anwani ya kuwa inawafikiana na ihtiyaat si kwa anwani ya taqliid. Mas’ala 27: Ikiwa mukallaf
atamfuata mtu ambae si mwenye uwezo wa kutoa fat’wa kisha akalifahamu hilo ni wajibu juu yake kuhama, na matendo yake aliyoyafanya mwanzo ni sawa na matendo ya
jaahili alie fanya matendo yake bila ya taqliid. Na pia itakuwa ni wajibu
kutokana na kauli yenye nguzu zaidi kuhamia kwa alie kuwa Aalam kwa yule ambae
alikuwa akimfuata asie kuwa Aalam, au alikuwa akimfuata Aalam kisha baadae
mwingine akawa ni Aalam zaidi yake. Mas’ala 28: Ikiwa suala la
Aalamiyya (Mjuzi zaidi) litafungika kwa watu wawili na haikuwezekana
kumuainisha mmoja wapo kuwa ni Aalam zaidi- kwa sababu kwa kila mmojawapo
kunaihtimali ya kuwa ni Aalam- hapa hukumu yake ni kumfuata yeyote kati yao bila kipingamizi, sawa iwezekane kufanya ihtiyaat kati ya kauli mbili za watu hao au
laa. Mas’ala 29: Alie chukuwa uwakala
wa kufanya matendo badala ya mtu mwingine atafanya matendo yale kwa mujibu wa
taqliid ya alie mchukulia uwakala na si kwa mujibu wa taqliid yake ikiwa wanatofautiana
katika Mujtahidi, ama alie usiwa (Wasii) kwa mfano lau kama atakuwa ni mwenye
kuusiwa kukodisha watu wa kusali sala kwa niaba yake hapo ni wajibu matendoyake
yawe sawa au kwa mujibu wa fat’wa za Mujtahidi wake.  Mas’ala 30: Mtu alie idhinishwa na
kupewa uwakala na  Mujtahidi wa kutumia au kusimamia  mali ya waqfu au mali ya
watoto wasio na walii humalizika idhini hiyo au uwakala huo kwa kufariki
Mujtahidi yule, tofauti na mtu alie teuliwa na kupewa jukumu na Mujtahidi la
kusimamia vitu vya waqfu au usimamizi wa watoto au wendawazimu wasio kuwa na
msimamizi( walii), hakika  yeye usimamizi wake na uangalizi wake  haubatiliki
kwa kauli iliyo dhahiri. Mas’ala 31: Ni wajibu kwa
mukallaf kufahamu sehemu zote za ibada na masharti yake na vizuizi vyake na
vitangulizi vyake hata kama ni kwa sura ya ujumla, kiasi kwamba awe anafahamu
yakuwa ibada yake imetimiza sehemu zote na masharti yote na haina vizuizi. Mas’ala 32: Ikiwa yatamtokea
mukallaf  mas’ala fulani ambayo hajui hukumu yake na  akiwa katikakati ya sala
inajuzu kwake kufanya tendo lake kwa kufuata upande mmoja wapo kati ya pande
mbili za mas’ala hayo, akikusudia kuuliza hukumu yake baada ya sala na akiwa
ameazimia kuirudia sala hiyo ikiwa haikuwafikiana na ukweli ulivyo wa kisheria,
na lau kama tendo lake litakuwa sambamba na hukumu ya kisheria haitakuwa ni
wajibu kwake kuirudia.  Mas’ala 33: Kama ambavyo ni
wajibu kufanya taqliid katika mambo ya wajibu na haraam, pia ni wajibu katika
mambo ya sunna ambayo kunaihtimali ya kuwa ni wajibu, na katika mambo ya
makruuh na mubaha ( si wajibu wala haram) yenye ihtimali ya kuwa yanaulazima wa
kutekelezwa. Mas’ala 34: Tamko ( Ahwat) lililo
tajwa katika  kitabu hiki linakusudiwa kwa maana ya ihtiyaat ya sunna ikiwa
limetanguliwa na limefuatiwa na fat’wa, laa sivyo  lina maana ya ihtiyati ya
wajibu, na maana yake ni kuwa mukallaf wakati huo anahiari  kati ya kufanya
tendo hilo na kati ya kurejea kwa Mujtahidi mwingine pamoja na kuchunga suala
la alie kuwa Aalam (mjuzi zaidi), tofauti na ihtiyaati ya sunna, haijuzu katika
ihtiyaati hiyo kurejea kwa mwinginewe, bali mukallaf ana hiari kati ya kufanya
kwa mujibu wa ihtiyaati hiyo au kufanya kwa mujibu wa fat’wa iliyo tangulia au
ifuatayo. Mas’ala 35: Ikiwa mukallaf
atafunga mkataba au kufanya  makubaliano na mtu fulani au akafanya tendo fulani
kwa mijibu wa taqliidi ya Mujtadi anae hukumu ya kuwa mkataba huo na matendo
hayo ni sahihi kisha Mujtahidi huyo akafa, na akamfuata anae sema ya kuwa
mkataba huo ni batili inajuzu kwa mukallaf huyo kujengea kuwa  matendo yake
yaliyo tangulia ni sahihi.  
 KITABU TWAHARA (MLANGO WA TWAHARA) 
 KATIKA MLANGO HUU KUNA SEHEMU TOFAUTI 
 SEHEMU YA KWANZA 
 MGAWANYIKO WA MAJI NA HUKUMU ZAKE   
NA KATIKA SEHEMU HII KUNA VIFUNGU KADHAA 
KIFUNGU CHA KWANZA 
MAJI  YAMEGAWANYIKA SEHEMU MBILI 
SEHEMU YA KWANZA:  
 Maji Mutlaq,
hiki ni kitu chenye kutiririka na ambacho huitwa kwa jina la (Maji) bila
kuongeza kitu, kama maji yaliyopo kwenye kisima au mto au bahari. Na tusemapo
maji ya bahari au maji ya mto au maji ya kisima husema hivyo kwa ajili ya
kuyapambanua, si kwa sababu ya kusahihisha matumizi. 
SEHEMU YA PILI:  
Maji mudhaaf, 
ni kitu chenye kutiririka ambacho haifai kuitwa kwa jina la (maji) pekee,  bali
huongezewa neno lingine kama ifuatavyo: Maji ya komamanga kwa mfano, au maji ya
waridi kwa kutaja jina lililo dhifiwa kwenye tamko maji. Na pengine huitwa (Maji)
kwa majazi, kwa sababu hii inafaa kuto tumia neno maji kwenye neno hilo. 
KIFUNGU CHA 
PILI: 
 MAJI MUTLAQ 
(Maji halisi) NA HUKUMU ZAKE 
Maji mutlaq 
yamegawanyika sehemu zifuatazo: 1-Maji yenye kutiririka.  2- Maji ya 
chemchem yasiyo tiririka. 3- Maji ya kisima. 4- Maji ya mvua.  5- Maji ya 
kuri moja 6- Maji kidogo (yasiyo fikia kiwango cha kuri moja).  
Mas'alal 36: Maji 
mutlaq na mgawanyiko wake wote kama hayakuingiwa na najisi ni twahara na ni 
yenye kutwahirisha hadathi na khabathi. 
Mas'ala 37:Maji 
mutlaq na mgawanyiko wake wote  hata maji yenye kutiririka ikiwa 
yatabadilika na kugeuka moja ya sifa zake tatu kwa kuingiwa na najisi 
hunajisika, Na sifa hizo ni rangi ladha na harufu. Na maji kidogo 
yananajisika tu kwa kuingiwa  na najisi. 
Mas'ala 38: Ikiwa 
maji yatabadilika  na ubadilikaji huo haukuwa ni katika moja kati ya sifa 
zake tatu, rangi ladha na harufu, kama yakibadilika uzito wake  na mfano wa 
hayo, maji hayo hayata najisika ikiwa hayakubadilika na kuwa maji 
mudhaafu. 
Mas'ala 39: Ikiwa 
rangi ya maji itabadilika au ladha yake au harufu yake kwa kukaribiana na 
najisi, kama  mzoga ukiangukia karibu na maji hayo na mzoga huo ukawa 
ukingoni mwa maji hayo hayatanajisika vile vile. 
Mas'ala 40: Ikiwa 
maji hayakubadilika kwa najisi  maji hayo si najisi, kama yakibadilika kwa 
kitu kilicho najisika, kama ikiwa  yatabadilika na kuwa ya njano au mekundu 
kwa kuingiwa na juisi iliyo najisika.  
Mas'ala 41: maji 
hayanajisiki tu kwa kuingiwa na najisi au kubadilika kwa kuingiwa na najisi 
yenyewe, bali  ikiwa yataingiwa na kitu chenye najisi au kilicho beba 
sehemu na chembe chembe za najisi, au kitu hicho kina chembe chembe za najisi na 
maji yale yakabadilika na kugeuka kwa najisi ile, maji hayo yatanajisika 
pia. 
Mas'ala 42: Inatosha 
kunajisika kwa maji kubadilika kwake kwa sababu ya kuingiwa na najisi hata kama 
hayakubadilika sifa zake zote, kwa mfano lau kama  maji hayo yatabadilika 
rangi yake na kuwa rangi ya njano au nyekundu kwa kuingiwa na damu, au yakawa na 
harufu iliyo kinyume na harufu ya mkojo na haja kubwa kwa kuangukia najisi hizo 
kwenye maji hayo, maji hayo yatakuwa yamenajisika pia.  
 KIFUNGU CHA TATU 
 MAJI  YENYE KUTIRIRIKA  NA HUKUMU ZAKE 
Haya ni maji yenye 
kutiririka na yaliyo ungana na mada ya ardhini au nyingineyo hata kama hayatoki 
na kuchimbuka ardhini. 
Mas'ala 43: Maaul 
jaariy (maji yenye kutiririka) sawa yawe ni kiasi cha kuri moja au yawe ni kiasi 
kidogo kuliko kuri, na sawa utiririkaji wake uwe ni wa kuchupa au kunyunyiza,. 
hayanajisiki kwa kuingiwa na najisi kama hayajabadilika sifa zake.  
Na huambatanishwa na 
maji yenye kutiririka katika hukumu ya kuto najisika kwa kuingiwa na najisi bila 
kubadilika, maji yote yachimbukayo ardhini hata kama hayatiririki.  
Mas'ala 44: Ikiwa 
maji yenye kutiririka juu ya ardhi bila ya kuwa na asili ichimbukayo ardhini 
au  yenye kunyunyiza, ikiwa majio hayo yatakuwa ni machache zaidi kuliko 
kuri ya maji,  hakika maji hayo hunajisika kwa kuingiwa tu na najisi. 
 
Ama ikiwa mukallaf 
atatia shaka ya kuwa maji hayo yana chimbuko  (mada) au laa kauli yenye 
nguvu inasema kuwa hayata najisika  maji hayo kwa kuingiwa au kukutana na 
najisi ikiwa hapo kabla hayakutanguliwa na hali ya kuto kuwa na mada. 
Mas'ala 45: 
Kizingatiwacho katika kuto najisika maji yatiririkayo ni kuungana kwake na mada 
(asili kama chemchem au kuungana na bomba), kwa mfano lau kama mada au asili ya 
kutiririka kwa  maji hayo iko juu, na mada  yenye kutiririsha au 
kunyunyiza maji hayo itakuwa  ni chini ya kuri moja maji hayo yatanajisika, 
ndio ikiwa sehemu inayo nyunyiza au asili ya maji hayo itagusana na najisi maji 
hayo hayatanajisika. 
Mas'ala 46: Maji 
yaliyo tuwama na yaliyo ungana na maji yenye kutiririka hukumu yake ni sawa na 
maji yenye kutiririka katika  hukumu ya kuto najisika kwake kwa kugusana au 
kuingiwa na najisi au kitu kilicho najisika, kwa mfano hodhi lililo ungana na 
mto kwa ajili ya umwagiliaji, maji yake hayanajisiki kwa kugusana na najisi, 
vile vile kingo za mto hata kama maji yake yametuwama na 
hayatiririki. 
Mas'ala 57: Ikiwa 
baadhi ya sehemu ya maji yenye kutiririka itabadilika na sehemu nyingine 
isibadilike, sehemu ya maji hayo iliyo ungana na mada hainajisiki kwa 
kuungana  au kuingiwa na najisi hata kama maji yake ni machache, na upande 
mwingine hukumu yake ni sawa na hukumu ya maji yaliyo tuwama ikiwa maji ya 
sehemu hiyo yatabadilika, laa sivyo yatahesabiwa yamenajisika kiwango kilicho 
badilika pekee, kwa kuungana  yale mengine na mada. 
  KIFUNGU CHA NNE  
  MAJI  YALIYO  TUWAMA  NA HUKUMU ZAKE 
Mas'ala 48: Maji 
yaliyo tuwama bila kuungana na mada ikiwa kiwango chake hakifikii kuri moja 
hakika maji hayo yananajisika kwa kuingiwa na najisi, tofauti na ikiwa yanafikia 
kuri moja, hakika yakiwa ni kuri moja hayanajisiki kwa kuingiwa au 
kukutana  na najisi isipokuwa yatakapo badilika moja kati ya sifa zake 
tatu. 
Mas'ala 49: Kiwango 
cha kuri kwa uzito ni sawa na huqqa ya istambuli 280, ama ukubwa wake ni sawa na 
shibiri 34 kasoro moja ya tatu, na kwa lita ni sawa na lita 377 
takriiban. 
Mas'ala 50: Maji 
yakiwa ni chini ya kuri moja hata kama ni kwa kiasi kichache hukumu yake ni sawa 
na hukumu ya ya maji kidogo. 
Mas'ala 51:Ikiwa 
najisi itaangukia kwenye kuri na haikujulikana ya kuwa imeangukia humo kabla ya 
kufika kuri au baada ya kukamilika kuri, maji hayo yatahukumiwa kuwa ni twahara, 
isipokuwa ikiwa itafahamika tarehe ya kuangukia kwake humo na tarehe ya kufikia 
kwake kuri haikujulikana. 
 Mas'ala 52: 
Ikiwa imefikia kuri lakini haikujulikana ya kuwa ni maji mutlaq (ni maji halisi) 
au mudhaaf, na yakaingiwa na najisi,  maji hayo hayata hukumiwa kuwa ni 
najisi, isipokuwa itakapo kuwa  hali yake ya mwanzo ilikuwa ni mudhaaf na 
kukawa na shaka ya kuwa bado ni mudhafu. 
 Na ikiwa 
kunakuri mbili moja ni mutlaq na nyingine ni mudhaaf, na ikafahamika kuingiwa na 
najisi moja kati ya kuri hizo mbili  lakini haijulikani kuwa ni ipi kati ya 
kuri hizo,  zote mbili zitahukumiwa kuwa ni twahara pia.  
 
KIFUNGU CHA TANO 
  
MAJI YA MVUA NA HUKUMU ZAKE 
 Mas'ala 53: 
Hukumu ya maji ya mvua wakati ikinyesha ni sawa na hukumu ya maji yenye 
kutiririka, hayata najisika kwa kugusana na najisi ikiwa hayajabadilika moja 
kati ya sifa zake,  hata kama  mvua hiyo ni kidogo, sawa maji hayo 
yatiririke kwenye mifereji au juu ya ardhi au laa, la muhimu ni kuthibiti kuwa 
ni maji ya mvua, na ikiwa yatakusanyika sehemu moja na kikaoshewa ndani  
yake kitu kilicho najisika  kitu hicho kitatwahirika hata kama maji yale 
yatakuwa ni madogo.  
Haya yote ni wakati 
mvua ikiendelea kunyesha, na ikiwa mvua itakatika na kuacha  kunyesha 
hukumu yake ni sawa na hukumu ya maji yaliyo tuwama.  
Mas'ala 54: Nguo 
iliyo najisika  na zulia lililo najisika ikiwa vitu viwili hivi 
vitanyeshewa na mvua na maji kuingia ndani ya vitu hivyo basi vitu  hivyo 
vyote vitatwahirika, na haihitaji kukamua au kuosha kwa mara kadhaa, na 
ikiwa  maji yatafika kwenye baadhi ya sehemu na hayakuenea sehemu zote 
itatwahirika sehemu zilizo fikiwa na mvua hiyo  na si vinginevyo. Na hukumu 
hii inahusika tu ikiwa hakuna najisi yenyewe kwenye vitu hivyo, laa sivyo 
havitwahiriki isipokuwa vitakapo nyeshewa tena baada ya kuondoka najisi yenyewe 
kwenye vitu  hivyo. 
Mas'ala 55: Ardhi 
iliyo najisika hutwahirika kwa kunyeshewa na mvua kwa sharti kwamba mvua hiyo 
iinyeshee moja kwa moja kutoka mawinguni  hata kama ni kwa kupeperushwa na 
upepo,  ama ikiwa mvua hiyo itanyeshea juu ya kitu kingine – kama ambavyo 
maji hayo yatatiririkia juu ya ardhi baada ya kuangukia mahali pengine na 
kuingiwa na najisi- katika hali kama hii haita twahirika.  
Ndio  ikiwa mvua 
hiyo itanyesha juu ya ardhi kisha maji yake yakatiririkia juu ya paa basi sehemu 
hiyo itatwahirika. 
Mas'ala 56: Ikiwa 
maji ya mvua yataangukia kwenye najisi yenyewe kisha yakadondokea kwenye kitu 
kingine, kitu hicho hakita najisika ikiwa maji hayo hayakuwa na chembe chembe za 
najisi ndani yake na hayakubadilika kwa najisi. 
Mas'ala 57: Mchanga 
ulio najisika hutwahirika kwa kunyeshewa na mvua ikiwa mvua hiyo itaingia hadi 
ndani ya mchanga huo na kubadilika kuwa udongo. 
Mas'ala 58: Jamvi 
lililo najisika linatwahirika kwa kunyeshewa na mvua, vilevile zulia lililo 
tandikwa juu ya ardhi, na ardhi iliyopo chini ya zulia hilo ikiwa ni najisi 
hutwahirika  ikifikiwa na maji ya mvua. Ndio ikiwa jamvi au zulia havikuwa 
juu ya ardhi au kukawa na utengano, hapo kuna ishkaali katika hukumu ya 
kutwahirika kwake kwa kunyeshewa na mvua, kwanza kwa kunyeshea mvua juu ya jamvi 
au zulia kisha maji hayo yakadondokea juu ya ardhi.  
Mas'ala 59: Chombo 
ambaacho nbi  najisi kinatwahirika ikiwa maji ya mvua yatafika sehemu zote 
zenye najisi katika chombo hicho isipokuwa ikiwa kimenajisika kwa kuliwa na mbwa 
ndani yake, katika hali kama hiyo kutwahirika chombo hicho kwa kunyeshewa na 
mvua tu bila ya kukisugua au kukiosha kwa mchanga kuna ishkaali, lakini ikiwa 
kitanyeshewe na mvua baada ya kukisugua au kukiosha kwa mchanga wakati huo 
kitatwahirika bila ya kuhitajia kuosha mara kadhaa. 
 
KIFUNGU CHA SITA 
 
 
 
MAJI YA BAFUNI NA HUKUMU YAKE 
Mas'ala 60: Maji ya 
bafuni ni sawa na maji yenye kutiririka kwa sharti kuwa yawe yameungana na mada, 
kwa mfano maji yaliyoko kwenye mahodhi madogo ikiwa yataungana na mada 
hayanajisiki kwa kuingiwa na najisi ikiwa maji yaliyoko kwenye hodhi pekee au 
kwa kuyaunganisha na yaliyomo kwewnye mada yanafikia kuri. 
Mas'ala 61:Ikiwa maji 
yaliyomo kwenye mahodhi madogo yatanajisika yanatwahirika kwa kuungana na mada 
kwa sharti kwamba maji ya mada yawe ni kuri na yachanganyike pia. 
  
 
KIFUNGU CHA SABA 
 
 MAJI YA KISIMA NA  
HUKUMU  ZAKE 
Mas'ala 62: Hukumu ya 
maji ya kisima yenye kuchimbuka ardhini ni sawa na hukumu ya maji yenye 
kutiririka katika hukumu ya kuto najisika isipokuwa kwa kubadilika moja kati ya 
sifa zake, sawa yawe ni kiasi cha kuri moja au chini ya hapo, na ikiwa 
yatabadilika  kisha ubadilikaji huo ukaondoka na kutoweka wenyewe maji hayo 
yatatwahirika kwa sababu yana mada na yamechanganyika na maji yatokayo kwenye 
mada kama chemchem. Ama yakiwa hayana mada yenye kuchimbuka basi itazingatiwa 
kiasi cha kuri katika hali ya  kutonajisika kwake hata kama kitaitwa 
kisima, kama mfano wa visima ambavyo hukusanyika ndani yake maji yasiyo 
chimbuka  ardhini. 
Mas'ala 63: 
Maji  najisi yaliyo tuwama sawa maji hayo yawe ni kuri au  
kidogo  yanatwahirika kwa kuungana na maji ya kuri yaliyo twahara au kwa 
kuungana na maji yenye kutiririka au maji yenye kuchimbuka ardhini hata kama 
hayatiririki na kuchanganyika na maji hayo, na pia hutwahirika kwa kukutana na 
kuchanganyika na maji ya mvua,  na kauli ya ahwat ni kuwa kutazingatiwa 
kuchanganyika kwa maji hayo. 
Mas'ala 64: Birika 
lililo jazwa maji yaliyo najisika ikiwa litazamishwa kwenye hodhi  
hutwahirika baada ya kuchanganyika maji hayo, na si wajibu kuyamwaga maji yake 
na kuliosha birika hilo. 
 
KIFUNGU CHA NANE  
 
MAJI YALIYO TUMIKA YAKIWA NI MACHACHE 
Mas'ala 65: Maji 
yaliyo tumika  kutawadhia ni twahara na yanatwahirisha hadathi na khabathi, 
vile vile maji yaliyo tumika katika ghusli ya sunna, ama maji yaliyo tumika 
katika ghusli ya hadathi kubwa pamoja na kuwa mwili hutwahirika hakuna ishkaali 
katika utwahara wa maji hayo na juu  uwezekano wa kuyatumia kuondolea 
khabathi, na kauli yenye nguvu zaidi ni kuwa inajuzu kuyatumia kuondolea hadathi 
pia japokuwa kauli ya ahwati ni kuwa nivema kujiepusha na maji hayo.  
Ama maji yaliyo 
tumika kuondoa khabathi tofauti na maji yaliyo tumika kustanji haijuzu kuyatumia 
katika udhu na ghusli, na kauli yenye nguvu zaidi ni kuwa maji yatumikayo 
kuondolea najisi yenyewe ni najisi, bali hata maji yaliyo tumiwa kuoshea yasiyo 
ondoa najisi, ama  maji ya kustanjia  hukumu yake itafuatia. 
 
Mas'ala 66: Hakuna 
ishkaali katika matone ambayo hudondokea kwenye chombo wakati wa kuosha hatakama 
tutasema ya kuwa haijuzu kutumia maji yaliyo oshewa hadathi kubwa. Na maji 
yanayo bakia kwenye nguo baada ya kukamuliwa nguo hiyo ni twahara, ikiwa maji 
hayo yatatoka baada ya nguo hiyo kukamuliwa hayata ambatanishwa na hukumu ya 
maji yaliyo oshewa. 
 Na mkono 
hutwahirika kwa kufuata kitu kinacho twahirishwa baada ya kukitwahirisha kitu 
hicho, kwa hivyo hakuna haja ya kuiosha mikono hiyo, pia chombo ambacho hutumika 
kuoshea nguo na mfano wa hivyo. 
 
KIFUNGU CHA TISA 
 
 
  
HUKUMU YA MAJI  YENYE  KUTILIWA  SHAKA 
Mas'ala 67: Maji 
ambayo hutiliwa shaka ya kuwa ni najisi au twahara maji hayo ni twahara ikiwa 
haikujulikana ya kuwa hapo kabla yalikuwa ni najisi, ama maji ambayo hutiliwa 
shaka ya kuwa ni mutlaq au hapana hayahukumiwi maji hayo kuwa ni mutlaq 
isipokuwa ikiwa hapo kabla yalikuwa ni mutlaq.  
Ndio, ikiwa maji hayo 
ni kuri moja na yakaingiwa na najisi hayatahukumiwa kuwa ni najisi isipokuwa 
ikiwa hapo kabla yalikuwa ni maji mudhaaf, ama maji ambayo yanatiliwa shaka ya 
kuwa ni mubaha au hapana (maji halali) maji hayo hukumu yake ni kuwa ni mubaha, 
aisipokuwa ikiwa hapo kabla yalikuwa ni milki ya mtu mwingine au yalikuwa katika 
milki ya mtu mwingine ambae kuna ihtimali kuwa ni maji yake. 
Mas'ala 68: Ikiwa 
mukallaf atafahamu kwa sura ya ujumla ya kuwa mojawapo  kati ya vyombo 
viwili ni najisi  na kingine ni twahara haitajuzu kutumia chombo moja wapo 
kuondolea khabathi au hadathi. 
Mas'ala 69: Chombo 
kinacho shukiwa kuwa sehemu moja wapo ya chombo hicho imenajisika  hakita 
hukumiwa kuwa ni najisi isipokuwa  hali ya sehemu  hiyo ya hapo kabla 
itajulikana kuwa ilikuwa ni najisi, lakini kauli ya ahwat inasema kuwa ni bora 
kujiepusha na utumiaji wa chombo hicho. 
Mas'ala 70: Ikiwa 
maji mutlaq yatafanana na mudhaaf itajuzu kuyatumia maji hayo kuondolea khabathi 
kwa kutumia moja wapo kati ya maji hayo na kuoshea kwa kutumia maji mengine, 
vile vile katika kuondoa hadathi. 
Mas'ala 71: Ikiwa 
itafahamika kwa sura ya ujumla ya kuwa maji haya ima ni najisi au  
ni mudhaaf inajuzu 
kuyanywa maji hayo, lakini haijuzu kuyatumia kutawadhia, vile vile ikiwa 
itajulikana ya kuwa ima maji hayo ni mudhaaf au ni maghsuub (ya kunyang'anya). 
 
Ama ikiwa 
itajulkikana ya kuwa maji hayo ni najisi au ni ya kunyang'anya haitajuzu 
kuyanywa, kama ambavyo  haitajuzu kuyatumia kutawadhia. 
Mas'ala 72: Ikiwa 
sehemu au pande zitiliwazo shaka au zenye shubha hazijulikani kidhati, katika 
hali kama hii inajuzu kuyatumia maji hayo bila kipingamizi. 
 
 
KIFUNGU CHA KUMI  HUKUMU ZA  MAJI  MUDHAAF 
Mmas'ala 73: Maji 
mudhaaf, kama maji ya uwa waridi ni twahara ikiwa hayakuingiwa na najisi, lakini 
maji hayo si yenye kutwahirisha hadathi,  vilevile si yenye kutwahirisha 
khabathi hata katika hali ya dharura. 
Mas'ala 74: Maji 
mudhaaf yana najisika kwa kuingiwa tu na najisi sawa yawe mengi au kidogo, 
isipokuwa yakiwa ni yenye kuchupa  kwa nguvu juu ya najisi, hata kama 
yanatoka chini kwenda juu kama maji yatokayo kwenye bomba lenye 
kunyunyizia  na mfano wa hiyo, katika hali kama hii itahukumiwa kuwa ni 
najisi sehemu ile tu iliyo gusana na najisi, na haivuki na kuelekea 
juu. 
Mas'ala 75: Ikiwa 
maji mudhaaf yatanajisika hayatatwahirika isipokuwa kwa kuyaweka kwenye 
kuri  au kwenye maji yenye kutiririka na kutoweka hali ya kuwa kwake maji 
mudhafu. Na kutwahirika  kwa maji mudhaaf  yaliyo najisi kwa 
kuyachemsha ( au kuongeza kiwango cha maji hayo) kuna ishkaali. 
  
 
KIFUNGU CHA KUMI NA 
MOJA MABAKI YA CHAKULA 
Mas'ala 76: Mabaki ya 
chakula yote ni twahara isipokuwa mabaki ya mnyama alie najisi (najisul aini) 
kama mbwa Nguruwe na mushrik (kafir) , hakika mabaki yao ni najisi. 
Mas'ala 77: 
Nimakuruhu kula mabaki ya mnyama asie liwa isipokuwa mabaki ya Muumini na paka 
kutokana na kauli ya baadhi ya mujtahidiin. 
 
SEHEMU YA PILI: HUKUMU ZA CHOONI 
  
 
  
 
 
PIA KUNA VIFUNGU KADHAA 
  
  
KIFUNGU CHA KWANZA 
  
  
  
HUKUMU ZA KWENDA CHOONI 
Mas'ala 78: Ni wajibu 
wakatio mtu anapokwenda chooni au katika hali ya kujisaidia haja kubwa bali hata 
katika hali nyingine tofauti kusitiri uchi (sehemu za siri) – nazo ni sehemu ya 
mbele na nyuma na peke mbili- kwa muonaji mwenye kuheshimiwa, isipokuwa mtoto na 
mwenda wazimu wasio weza kupambanua, na mke na mume na alie milikiwa kwa mmiliki 
wake na alie halalishwa kwa alie halalishiwa, hakika kwa watu hawa inajuzu kwa 
kila mmoja wao kuangalia uchi wa mwenziwe.  
Mas'ala 79: Hakuna 
tofauti katika uharamu wa kuangali kati ya uchi wa  Muislaam au kafiri 
kutokana na kauli ya ahwat. 
Mas'ala 80: Si wajibu 
kusitiri mapaja mawili wala matako wala nywele ziotazo pembezoni mwa sehemu za 
siri (mavuzi). Ndio, ni sunna kusitiri sehemu zilizoko kati ya kitovu na 
magoti. 
Mas'ala 81: Haijuzu 
kuangalia uchi wa mtu mwingine kwa kutumia kioo na mfano wa hicho, wala kwa 
kutumia kioo cha kujitizamia  na wala haijuzu kuangalia kwa kutumia maji 
yaliyo safi.   
Mas'ala 82: Ikiwa mtu 
itamlazimu kuangalia uchi wa mtu mwingine kama katika hali ya kumtibu mgonjwa, 
kauli ya ahwat ni kuwa ataangalia kupitia kioo kilicho wekwa mbele yake ikiwa 
kufanya hivyo kutatosheleza na kuondoa dharura hiyo, laa sivyo hakuna 
tatizo  kuangalia. 
Mas'ala 83: Ni haramu 
kwa mwenye kujisaidia haja kubwa – wakati wa kujisaidia- kuelekea Qibla na 
kukipa mgongo Qibla kwa kuielekeza sehemu ya mbele ya mwili wake  kwenye 
Qibla hata kama uchi wake atauelekeza sehemu au upande mwingine tofauti na 
sehemu hizo mbili, na kauli ya ahwat ni kuwa ataacha  kukielekezea  
uchi wake pekee hata kama sehemu za mbele za mwili wake zitaelekea  sehemu 
hizo mbili, na makusudio ya sehemu za mbele za mwili ni kifua tumbo na magoti 
mawili, na ikiwa italazimika kufanya moja wapo atakuwa na hiari japokuwa kauli 
ya ahwat ni kuwa atakipa mgongo, na akiwa itamlazimu kufanya kitendo kimoja 
wapo  kati ya mambo mawili hayo na kuto jisitiri pamoja na kuwepo 
muangaliaji mwenye kuheshimiwa itawajibika kwake kujisitiri. 
Mas'ala 84: Kauli 
yenye nguvu ni kuwa si haramu kukielekea au kukipa mgongo kibla katika hali ya 
kufanya istibraa na katika hali ya kustanji japo kuwa kutofanya hivyo ni ahwat 
(bora zaidi). Ndio ikiwa atafahamu ya kuwa mkojo utatoka  kwa kufanya 
istibraa kauli ya ahwat ni kuwa itawajibika kuacha kukielekea au kukipa mgongo 
Qibla. 
Mas'ala 85: Lau kama 
mukallaf atapatwa na shubha katika kukipambanua Qibla hukumu ya kutumia dhanna 
haiko mbali pamoja na kuto kuwepo uwezekano wa kukitafuta na kufanya uchunguzi 
wa sehemu ya Qibla, na ikiwa kuichelewesha sala kutamsababishia 
matatizo. 
Mas'ala 86: Ni haramu 
kujisaidia haja kubwa kwenye milki ya mtu mwingine isipokuwa kwa idhini yake, 
vile vile ni haramu kujisaidia kwenye makaburi ya waumini ikiwa kufanya hivyo ni 
kuvunja heshima yao. 
Mas'ala 87: Ni haramu 
kujisaidia haja kubwa kwenye mashule na mfano wa hayo ikiwa haikufahamika kuwa 
sehemu hizo zimewekwa waqfu kwa ajili ya watu wote, na inatosha idhini ya 
msimamizi wa waqfu hizo, na kauli iliyo dhahiri ni kutosheka na ada ya 
watu  ikiwa kufanya kwao kutakupa matumaini ya kuwa ni sehemu ya matumizi 
ya watu wote, vile vile hali ni hiyo hiyo kwenye matumizi mengine ya vitu hivyo 
vya waqfu.  
KIFUNGU CHA PILI
KUSTANJI
Ni wajibu kuosha 
sehemu ya kutokea mkojo kwa maji, na inatosha kuosha mara moja japo kuwa kauli 
ya ahwat ya sunna ni kuosha mara kadhaa, na haitoshelezi kitu kingine tofauti na 
maji, na sehemu ya haja kubwa ikiwa haja itavuka mahali pake na kutapakaa hapo 
italazimika kutumia maji pekee kama najisi nyingine, na ikiwa hakikuvuka mahali 
pake mukallaf anahiari ya kuosha kwa maji hadi kusafike mahali hapo, na kati ya 
kupangusa kwa  kutumia mawe au kitambaa au mfano wa hivyo kati ya vitu 
vyenye kuondoa najisi, na maji ni bora zaidi, na kutumia vyote  ndio 
ukamilifu wa twahara. 
Mas'ala 88: Je 
kupangusa kwa mawe na mfano wa hilo inasababisha kutwahirika mahala hapo au 
kusamehewa kwenye sala pekee? Katika kupangusa kuna ishkaali, na kauli ya ahwti 
ni ya pili (  yaani ni sababu ya kusamehewa kwenye sala) 
Mas'ala 89: Katika 
kupangusa huzingatiwa kutumia mawe matatu au mfano wa hayo, au kutumia pande 
tatu za jiwe moja na mfano wa hilo japo kuwa kuna uwezekano wa kusafika kwa 
kutumia chini ya mawe matatu, na kama hapakusafika mahala hapo kwa mawe matatu 
ataongeza mpaka pasafike mahali hapo. 
Mas'ala 90: Ni wajibu 
mawe yatumikayo au mfano wake yawe twahara. 
Mas'ala 91: Ni haramu 
kustanji kwa kutumia vitu vyenye kuheshimiwa, vile vile ni haramu kutumia mifupa 
na kinyesi. Na lau kama mtu atastanji kwa  kutumia vitu hivyo atazingatiwa 
kuwa ameasi, na kutwahirika au kusameheka kwa kutumia vitu hivyo kuna 
ishkaal. 
Mas;ala 92: Ni wajibu 
katika hali ya  kuosha kwa maji kuondoa najisi yenyewe na athari zake kwa 
maana kuwa kuondoa chembe chembe ndogo ambazo hazionekani na kwa kawaida 
haziondoki isipokuwa kwa kutumia maji, na si wajibu kuondoa rangi na harufu, na 
inatosha katika upangusaji  kuondoa najisi yenyewe, na si wajibu kuondoa 
athari za najisi, na ikiwa haja kubwa itatoka ikiwa na najisi nyingine isiyo 
kuwa hiyo kama damu au mahali pa haja kubwa pakagusana na najisi nyingine kutoka 
nje  haitatosheleza kuitwahirisha sehemu hiyo ispokuwa kwa kutumia maji, na 
lau kama atatia shaka ya kuwa imetwahirika sehemu hiyo au laa atajengea ya kuwa 
haikutwahirika na hapa atakuwa na hiayari kati ya kutumia maji  mawe na 
mfano wa vitu viwili hivyo. 
KIFUNGU CHA TATU
ADABU ZA KWENDA CHOONI
Ni sunna kwa mwenye 
kujisaidia haja kubwa kujitenga na watu au kwenda sehemu ya mbali ambayo 
hatoweza kuonekana, na katika haja ndogo atafute sehemu yenye muinuko, kama 
ambavyo ni sunna kwake kufunika kichwa na kufunga kitambaa shingoni, na kufunika 
kicha na nyingo kwa kilemba au kitambaa  kunatosheleza kufunika kichwa, na 
ni sunna kutanguliza mguu wa kulia wakati wa kutoka, na kufanya istibraa, na 
kujitegemeza kwenye  mguu wake wa kushoto – wkati wa kukaa- na kupanua mguu 
wa kulia, na ni makruuhu kujisaidia barabarani, njiani,  chini yamiti ya 
matunda, na sehemu za kulaaniwa, kama kwenye milango ya majumba na mfano wa 
sehemu hizo kati ya sehemu ambazo mwenye kujisaidia sehemu hizo anakuwa 
amejisababishia watu kumlaani, na sehemu zilizo andaliwa kwa ajili ya vituo vya 
misafara, na kulielekea jua au mwezi kwa utupu wake, na kula na kunywa katika 
hali ya kujisaidia, na mengineyo kati ya mambo yaliyo tajwa na maulamaa radhi za 
mwenyezi mungu ziwe juu yao, japo kuthibiti kwa baadhi ya mambo yaliyo tajwa 
kuwa ni ya sunna au makruuhu kuna ishkaali. 
Mas'ala 93: Maji ya 
kustanjia ni twahara hata kama yamestanjiwa sehemu ya kutokea mkojo ikiwa 
yatatimia masharti haya yafuatayo:  
1- Kuto badilika rangi, 
ladha na harufu ya maji hayo kwa najisi. 
2- Kuto ingiwa na najisi 
nyingine kutoka nje tofauti na mkojo. 
3- Kuto vuka najisi 
itokayo kwenye sehemu yake ya kawaida. 
4- Haja kubwa na ndogo 
isitoke pamoja na najisi nyingine  kama damu, isipokuwa ikiwa itatoka 
lakini si yenye kuonekana katika hali hiyo hakuna tatizo. 
5- Kusiwe na chembe 
chembe za haja kubwa zenye kuonekana kwa kauli ya ahwat. 
Kwa kukamilika 
masharti haya maji ya kustanjia yanakuwa ni twahara na yanaweza kutumika 
kuondolea khabathi, lakini haijuzu kuyatumia kuondolea hadathi wala  
kuyatumia kwenye udhu wa sunna na ghusli ya sunna. 
 
 
KIFUNGU CHA NNE ISTIBRAA
Namna ya kufanya 
istibraa ya mkojo ni kama ifuatavyo, kwanza uta pangusa kuanzia kwenye makalio 
(yaani mwanzoni mwa sehemu itokeapo haja kubwa) hadi mwanzoni mwa kiungo cha 
kiume mara tatu, kisha uta anzia mwanzoni mwa kiungo cha kiume hadi kwenye 
kichwa cha uume mara tatu, na mwisho utakikamua kichwa mara tatu. 
Na faida ya istibraa 
huonekana pale utakapo  kuhukumiwa kuwa ni twahara unyevu nyevu 
utokao baada ya kufanya istibraa unao shukiwa kuwa ni mkojo au laa, na umaji 
maji huo ukitoka si wajibu kutawadha, na lau kama utatoka umaji maji unao 
shukiwa kuwa ni mkojo kabla ya kufanya istibraa – hata kama mukallaf aliacha 
kufanya istibraa kutokana na dharura na kutoweza kufanya hivyo- atajengea kuwa 
ni mkojo, na itawajibika kujitwahirisha kwa kutoka umaji maji huo na  
kumlazimu kutawadha. 
Na huambatanishwa na 
istibraa katika faida zilizo tajwa muda wote ambao anayakini kuwa hakuna chembe 
chembe zilizo bakia kwenye mirija itoayo mkojo, na mwanamke hafanyi istibraa, na 
umaji maji utokao kwenye sehemu zake za siri unahukumiwa kuwa ni twahara na kuwa 
hautengui twahara ikiwa haikutambulika kuwa ni mkojo. Ndio ni bora zaidi kwa 
mwanamke kusubiri kidogo- baada ya kukojoa – na kukohoa kohoa na kujikamua utupu 
wake (sehemu zake za siri) kwa upana kisha kuiosha kwa maji. 
Mas'ala 94: Faida za 
kufanya istibraa hupatikana katika istibraa hata kama ni kwa kufanywa na mtu 
mwingine kama mkewe au mtu alie milikiwa (mjakazi au mtumwa). 
Mas'ala 95: Ikiwa 
mukallaf atatia shaka ya kuwa amefanya istibraa au amestanji atajengea kuwa 
hakufanya hata kama ni kawaida yake kufanya, na ikiwa atatia shaka mtu ambae 
hakufanya istibraa ya kuwa umetoka umajimaji atajengea kuwa haukutoka hata kama 
atakuwa anadhania kuwa umetoka umajimaji. 
Mas'ala 96: Ikiwa 
atafahamu ya kuwa amefanya istibraa au amestanji na akatia shaka ya kuwa 
amefanya istibraa au amestanji sawa sawa au laa atajengea kuwa ni 
sahihi. 
Mas'ala 97: Ikiwa 
mukallaf atafahamu ya kuwa ametokwa na madhii na hakufahamu ya kuwa madhii hayo 
yalifuatana na chembe chembve za  mkojo au hapana atajengea kuwa ni twahara 
hata kama hakufanya istibraa, isipokuwa ikithibiti kuwa ni umajimaji unao tiliwa 
shaka, na shaka yenyewe iwe katika hali ifuatayo ya kuwa umaji maji huu 
uliodhihiri je yote ni madhii au  ni mchanganyiko  kati ya madhii na 
mkojo.  
  
KITABU TWAHARA (MLANGO WA TWAHARA) 
 
 
  
KATIKA 
MLANGO HUU KUNA SEHEMU TOFAUTI 
 
 
  
SEHEMU YA KWANZA 
  
MGAWANYIKO WA MAJI NA HUKUMU ZAKE   
  
 
 
NA KATIKA SEHEMU HII KUNA VIFUNGU KADHAA 
 
KIFUNGU CHA KWANZA 
 
MAJI  YAMEGAWANYIKA SEHEMU MBILI 
SEHEMU YA KWANZA: 
 
 Maji Mutlaq, 
hiki ni kitu chenye kutiririka na ambacho huitwa kwa jina la (Maji) bila 
kuongeza kitu, kama maji yaliyopo kwenye kisima au mto au bahari. Na tusemapo 
maji ya bahari au maji ya mto au maji ya kisima husema hivyo kwa ajili ya 
kuyapambanua, si kwa sababu ya kusahihisha matumizi. 
SEHEMU YA PILI: 
 
Maji mudhaaf,  
ni kitu chenye kutiririka ambacho haifai kuitwa kwa jina la (maji) pekee,  
bali huongezewa neno lingine kama ifuatavyo: Maji ya komamanga kwa mfano, au 
maji ya waridi kwa kutaja jina lililo dhifiwa kwenye tamko maji. Na pengine 
huitwa (Maji) kwa majazi, kwa sababu hii inafaa kuto tumia neno maji kwenye neno 
hilo. 
KIFUNGU CHA 
PILI: 
 MAJI MUTLAQ 
(Maji halisi) NA HUKUMU ZAKE 
Maji mutlaq 
yamegawanyika sehemu zifuatazo: 1-Maji yenye kutiririka.  2- Maji ya 
chemchem yasiyo tiririka. 3- Maji ya kisima. 4- Maji ya mvua.  5- Maji ya 
kuri moja 6- Maji kidogo (yasiyo fikia kiwango cha kuri moja).  
Mas'alal 36: Maji 
mutlaq na mgawanyiko wake wote kama hayakuingiwa na najisi ni twahara na ni 
yenye kutwahirisha hadathi na khabathi. 
Mas'ala 37:Maji 
mutlaq na mgawanyiko wake wote  hata maji yenye kutiririka ikiwa 
yatabadilika na kugeuka moja ya sifa zake tatu kwa kuingiwa na najisi 
hunajisika, Na sifa hizo ni rangi ladha na harufu. Na maji kidogo 
yananajisika tu kwa kuingiwa  na najisi. 
Mas'ala 38: Ikiwa 
maji yatabadilika  na ubadilikaji huo haukuwa ni katika moja kati ya sifa 
zake tatu, rangi ladha na harufu, kama yakibadilika uzito wake  na mfano wa 
hayo, maji hayo hayata najisika ikiwa hayakubadilika na kuwa maji 
mudhaafu. 
Mas'ala 39: Ikiwa 
rangi ya maji itabadilika au ladha yake au harufu yake kwa kukaribiana na 
najisi, kama  mzoga ukiangukia karibu na maji hayo na mzoga huo ukawa 
ukingoni mwa maji hayo hayatanajisika vile vile. 
Mas'ala 40: Ikiwa 
maji hayakubadilika kwa najisi  maji hayo si najisi, kama yakibadilika kwa 
kitu kilicho najisika, kama ikiwa  yatabadilika na kuwa ya njano au mekundu 
kwa kuingiwa na juisi iliyo najisika.  
Mas'ala 41: maji 
hayanajisiki tu kwa kuingiwa na najisi au kubadilika kwa kuingiwa na najisi 
yenyewe, bali  ikiwa yataingiwa na kitu chenye najisi au kilicho beba 
sehemu na chembe chembe za najisi, au kitu hicho kina chembe chembe za najisi na 
maji yale yakabadilika na kugeuka kwa najisi ile, maji hayo yatanajisika 
pia. 
Mas'ala 42: Inatosha 
kunajisika kwa maji kubadilika kwake kwa sababu ya kuingiwa na najisi hata kama 
hayakubadilika sifa zake zote, kwa mfano lau kama  maji hayo yatabadilika 
rangi yake na kuwa rangi ya njano au nyekundu kwa kuingiwa na damu, au yakawa na 
harufu iliyo kinyume na harufu ya mkojo na haja kubwa kwa kuangukia najisi hizo 
kwenye maji hayo, maji hayo yatakuwa yamenajisika pia.  
 
KIFUNGU CHA TATU 
 
MAJI  YENYE KUTIRIRIKA  NA HUKUMU ZAKE 
Haya ni maji yenye 
kutiririka na yaliyo ungana na mada ya ardhini au nyingineyo hata kama hayatoki 
na kuchimbuka ardhini. 
Mas'ala 43: Maaul 
jaariy (maji yenye kutiririka) sawa yawe ni kiasi cha kuri moja au yawe ni kiasi 
kidogo kuliko kuri, na sawa utiririkaji wake uwe ni wa kuchupa au kunyunyiza,. 
hayanajisiki kwa kuingiwa na najisi kama hayajabadilika sifa zake.  
Na huambatanishwa na 
maji yenye kutiririka katika hukumu ya kuto najisika kwa kuingiwa na najisi bila 
kubadilika, maji yote yachimbukayo ardhini hata kama hayatiririki.  
Mas'ala 44: Ikiwa 
maji yenye kutiririka juu ya ardhi bila ya kuwa na asili ichimbukayo ardhini 
au  yenye kunyunyiza, ikiwa majio hayo yatakuwa ni machache zaidi kuliko 
kuri ya maji,  hakika maji hayo hunajisika kwa kuingiwa tu na najisi. 
 
Ama ikiwa mukallaf 
atatia shaka ya kuwa maji hayo yana chimbuko  (mada) au laa kauli yenye 
nguvu inasema kuwa hayata najisika  maji hayo kwa kuingiwa au kukutana na 
najisi ikiwa hapo kabla hayakutanguliwa na hali ya kuto kuwa na mada. 
Mas'ala 45: 
Kizingatiwacho katika kuto najisika maji yatiririkayo ni kuungana kwake na mada 
(asili kama chemchem au kuungana na bomba), kwa mfano lau kama mada au asili ya 
kutiririka kwa  maji hayo iko juu, na mada  yenye kutiririsha au 
kunyunyiza maji hayo itakuwa  ni chini ya kuri moja maji hayo yatanajisika, 
ndio ikiwa sehemu inayo nyunyiza au asili ya maji hayo itagusana na najisi maji 
hayo hayatanajisika. 
Mas'ala 46: Maji 
yaliyo tuwama na yaliyo ungana na maji yenye kutiririka hukumu yake ni sawa na 
maji yenye kutiririka katika  hukumu ya kuto najisika kwake kwa kugusana au 
kuingiwa na najisi au kitu kilicho najisika, kwa mfano hodhi lililo ungana na 
mto kwa ajili ya umwagiliaji, maji yake hayanajisiki kwa kugusana na najisi, 
vile vile kingo za mto hata kama maji yake yametuwama na 
hayatiririki. 
Mas'ala 57: Ikiwa 
baadhi ya sehemu ya maji yenye kutiririka itabadilika na sehemu nyingine 
isibadilike, sehemu ya maji hayo iliyo ungana na mada hainajisiki kwa 
kuungana  au kuingiwa na najisi hata kama maji yake ni machache, na upande 
mwingine hukumu yake ni sawa na hukumu ya maji yaliyo tuwama ikiwa maji ya 
sehemu hiyo yatabadilika, laa sivyo yatahesabiwa yamenajisika kiwango kilicho 
badilika pekee, kwa kuungana  yale mengine na mada. 
 
 KIFUNGU CHA NNE 
 
 
  
MAJI  YALIYO  TUWAMA  NA HUKUMU ZAKE 
Mas'ala 48: Maji 
yaliyo tuwama bila kuungana na mada ikiwa kiwango chake hakifikii kuri moja 
hakika maji hayo yananajisika kwa kuingiwa na najisi, tofauti na ikiwa yanafikia 
kuri moja, hakika yakiwa ni kuri moja hayanajisiki kwa kuingiwa au 
kukutana  na najisi isipokuwa yatakapo badilika moja kati ya sifa zake 
tatu. 
Mas'ala 49: Kiwango 
cha kuri kwa uzito ni sawa na huqqa ya istambuli 280, ama ukubwa wake ni sawa na 
shibiri 34 kasoro moja ya tatu, na kwa lita ni sawa na lita 377 
takriiban. 
Mas'ala 50: Maji 
yakiwa ni chini ya kuri moja hata kama ni kwa kiasi kichache hukumu yake ni sawa 
na hukumu ya ya maji kidogo. 
Mas'ala 51:Ikiwa 
najisi itaangukia kwenye kuri na haikujulikana ya kuwa imeangukia humo kabla ya 
kufika kuri au baada ya kukamilika kuri, maji hayo yatahukumiwa kuwa ni twahara, 
isipokuwa ikiwa itafahamika tarehe ya kuangukia kwake humo na tarehe ya kufikia 
kwake kuri haikujulikana. 
 Mas'ala 52: 
Ikiwa imefikia kuri lakini haikujulikana ya kuwa ni maji mutlaq (ni maji halisi) 
au mudhaaf, na yakaingiwa na najisi,  maji hayo hayata hukumiwa kuwa ni 
najisi, isipokuwa itakapo kuwa  hali yake ya mwanzo ilikuwa ni mudhaaf na 
kukawa na shaka ya kuwa bado ni mudhafu. 
 Na ikiwa 
kunakuri mbili moja ni mutlaq na nyingine ni mudhaaf, na ikafahamika kuingiwa na 
najisi moja kati ya kuri hizo mbili  lakini haijulikani kuwa ni ipi kati ya 
kuri hizo,  zote mbili zitahukumiwa kuwa ni twahara pia.  
 
KIFUNGU CHA TANO 
  
MAJI YA MVUA NA HUKUMU ZAKE 
 Mas'ala 53: 
Hukumu ya maji ya mvua wakati ikinyesha ni sawa na hukumu ya maji yenye 
kutiririka, hayata najisika kwa kugusana na najisi ikiwa hayajabadilika moja 
kati ya sifa zake,  hata kama  mvua hiyo ni kidogo, sawa maji hayo 
yatiririke kwenye mifereji au juu ya ardhi au laa, la muhimu ni kuthibiti kuwa 
ni maji ya mvua, na ikiwa yatakusanyika sehemu moja na kikaoshewa ndani  
yake kitu kilicho najisika  kitu hicho kitatwahirika hata kama maji yale 
yatakuwa ni madogo.  
Haya yote ni wakati 
mvua ikiendelea kunyesha, na ikiwa mvua itakatika na kuacha  kunyesha 
hukumu yake ni sawa na hukumu ya maji yaliyo tuwama.  
Mas'ala 54: Nguo 
iliyo najisika  na zulia lililo najisika ikiwa vitu viwili hivi 
vitanyeshewa na mvua na maji kuingia ndani ya vitu hivyo basi vitu  hivyo 
vyote vitatwahirika, na haihitaji kukamua au kuosha kwa mara kadhaa, na 
ikiwa  maji yatafika kwenye baadhi ya sehemu na hayakuenea sehemu zote 
itatwahirika sehemu zilizo fikiwa na mvua hiyo  na si vinginevyo. Na hukumu 
hii inahusika tu ikiwa hakuna najisi yenyewe kwenye vitu hivyo, laa sivyo 
havitwahiriki isipokuwa vitakapo nyeshewa tena baada ya kuondoka najisi yenyewe 
kwenye vitu  hivyo. 
Mas'ala 55: Ardhi 
iliyo najisika hutwahirika kwa kunyeshewa na mvua kwa sharti kwamba mvua hiyo 
iinyeshee moja kwa moja kutoka mawinguni  hata kama ni kwa kupeperushwa na 
upepo,  ama ikiwa mvua hiyo itanyeshea juu ya kitu kingine – kama ambavyo 
maji hayo yatatiririkia juu ya ardhi baada ya kuangukia mahali pengine na 
kuingiwa na najisi- katika hali kama hii haita twahirika.  
Ndio  ikiwa mvua 
hiyo itanyesha juu ya ardhi kisha maji yake yakatiririkia juu ya paa basi sehemu 
hiyo itatwahirika. 
Mas'ala 56: Ikiwa 
maji ya mvua yataangukia kwenye najisi yenyewe kisha yakadondokea kwenye kitu 
kingine, kitu hicho hakita najisika ikiwa maji hayo hayakuwa na chembe chembe za 
najisi ndani yake na hayakubadilika kwa najisi. 
Mas'ala 57: Mchanga 
ulio najisika hutwahirika kwa kunyeshewa na mvua ikiwa mvua hiyo itaingia hadi 
ndani ya mchanga huo na kubadilika kuwa udongo. 
Mas'ala 58: Jamvi 
lililo najisika linatwahirika kwa kunyeshewa na mvua, vilevile zulia lililo 
tandikwa juu ya ardhi, na ardhi iliyopo chini ya zulia hilo ikiwa ni najisi 
hutwahirika  ikifikiwa na maji ya mvua. Ndio ikiwa jamvi au zulia havikuwa 
juu ya ardhi au kukawa na utengano, hapo kuna ishkaali katika hukumu ya 
kutwahirika kwake kwa kunyeshewa na mvua, kwanza kwa kunyeshea mvua juu ya jamvi 
au zulia kisha maji hayo yakadondokea juu ya ardhi.  
Mas'ala 59: Chombo 
ambaacho nbi  najisi kinatwahirika ikiwa maji ya mvua yatafika sehemu zote 
zenye najisi katika chombo hicho isipokuwa ikiwa kimenajisika kwa kuliwa na mbwa 
ndani yake, katika hali kama hiyo kutwahirika chombo hicho kwa kunyeshewa na 
mvua tu bila ya kukisugua au kukiosha kwa mchanga kuna ishkaali, lakini ikiwa 
kitanyeshewe na mvua baada ya kukisugua au kukiosha kwa mchanga wakati huo 
kitatwahirika bila ya kuhitajia kuosha mara kadhaa. 
  
 KIFUNGU CHA SITA 
 
 
 
MAJI YA BAFUNI NA HUKUMU YAKE 
Mas'ala 60: Maji ya 
bafuni ni sawa na maji yenye kutiririka kwa sharti kuwa yawe yameungana na mada, 
kwa mfano maji yaliyoko kwenye mahodhi madogo ikiwa yataungana na mada 
hayanajisiki kwa kuingiwa na najisi ikiwa maji yaliyoko kwenye hodhi pekee au 
kwa kuyaunganisha na yaliyomo kwewnye mada yanafikia kuri. 
Mas'ala 61:Ikiwa maji 
yaliyomo kwenye mahodhi madogo yatanajisika yanatwahirika kwa kuungana na mada 
kwa sharti kwamba maji ya mada yawe ni kuri na yachanganyike pia. 
  
 
KIFUNGU CHA SABA 
  
MAJI YA KISIMA NA  HUKUMU  ZAKE 
Mas'ala 62: Hukumu ya 
maji ya kisima yenye kuchimbuka ardhini ni sawa na hukumu ya maji yenye 
kutiririka katika hukumu ya kuto najisika isipokuwa kwa kubadilika moja kati ya 
sifa zake, sawa yawe ni kiasi cha kuri moja au chini ya hapo, na ikiwa 
yatabadilika  kisha ubadilikaji huo ukaondoka na kutoweka wenyewe maji hayo 
yatatwahirika kwa sababu yana mada na yamechanganyika na maji yatokayo kwenye 
mada kama chemchem. Ama yakiwa hayana mada yenye kuchimbuka basi itazingatiwa 
kiasi cha kuri katika hali ya  kutonajisika kwake hata kama kitaitwa 
kisima, kama mfano wa visima ambavyo hukusanyika ndani yake maji yasiyo 
chimbuka  ardhini. 
Mas'ala 63: 
Maji  najisi yaliyo tuwama sawa maji hayo yawe ni kuri au  
kidogo  yanatwahirika kwa kuungana na maji ya kuri yaliyo twahara au kwa 
kuungana na maji yenye kutiririka au maji yenye kuchimbuka ardhini hata kama 
hayatiririki na kuchanganyika na maji hayo, na pia hutwahirika kwa kukutana na 
kuchanganyika na maji ya mvua,  na kauli ya ahwat ni kuwa kutazingatiwa 
kuchanganyika kwa maji hayo. 
Mas'ala 64: Birika 
lililo jazwa maji yaliyo najisika ikiwa litazamishwa kwenye hodhi  
hutwahirika baada ya kuchanganyika maji hayo, na si wajibu kuyamwaga maji yake 
na kuliosha birika hilo. 
 
KIFUNGU CHA NANE   
 
MAJI YALIYO TUMIKA YAKIWA NI MACHACHE 
Mas'ala 65: Maji 
yaliyo tumika  kutawadhia ni twahara na yanatwahirisha hadathi na khabathi, 
vile vile maji yaliyo tumika katika ghusli ya sunna, ama maji yaliyo tumika 
katika ghusli ya hadathi kubwa pamoja na kuwa mwili hutwahirika hakuna ishkaali 
katika utwahara wa maji hayo na juu  uwezekano wa kuyatumia kuondolea 
khabathi, na kauli yenye nguvu zaidi ni kuwa inajuzu kuyatumia kuondolea hadathi 
pia japokuwa kauli ya ahwati ni kuwa nivema kujiepusha na maji hayo.  
Ama maji yaliyo 
tumika kuondoa khabathi tofauti na maji yaliyo tumika kustanji haijuzu kuyatumia 
katika udhu na ghusli, na kauli yenye nguvu zaidi ni kuwa maji yatumikayo 
kuondolea najisi yenyewe ni najisi, bali hata maji yaliyo tumiwa kuoshea yasiyo 
ondoa najisi, ama  maji ya kustanjia  hukumu yake itafuatia. 
 
Mas'ala 66: Hakuna 
ishkaali katika matone ambayo hudondokea kwenye chombo wakati wa kuosha hatakama 
tutasema ya kuwa haijuzu kutumia maji yaliyo oshewa hadathi kubwa. Na maji 
yanayo bakia kwenye nguo baada ya kukamuliwa nguo hiyo ni twahara, ikiwa maji 
hayo yatatoka baada ya nguo hiyo kukamuliwa hayata ambatanishwa na hukumu ya 
maji yaliyo oshewa. 
 Na mkono 
hutwahirika kwa kufuata kitu kinacho twahirishwa baada ya kukitwahirisha kitu 
hicho, kwa hivyo hakuna haja ya kuiosha mikono hiyo, pia chombo ambacho hutumika 
kuoshea nguo na mfano wa hivyo. 
 
KIFUNGU CHA TISA 
 
 
  
HUKUMU YA MAJI  YENYE  KUTILIWA  SHAKA 
Mas'ala 67: Maji 
ambayo hutiliwa shaka ya kuwa ni najisi au twahara maji hayo ni twahara ikiwa 
haikujulikana ya kuwa hapo kabla yalikuwa ni najisi, ama maji ambayo hutiliwa 
shaka ya kuwa ni mutlaq au hapana hayahukumiwi maji hayo kuwa ni mutlaq 
isipokuwa ikiwa hapo kabla yalikuwa ni mutlaq.  
Ndio, ikiwa maji hayo 
ni kuri moja na yakaingiwa na najisi hayatahukumiwa kuwa ni najisi isipokuwa 
ikiwa hapo kabla yalikuwa ni maji mudhaaf, ama maji ambayo yanatiliwa shaka ya 
kuwa ni mubaha au hapana (maji halali) maji hayo hukumu yake ni kuwa ni mubaha, 
aisipokuwa ikiwa hapo kabla yalikuwa ni milki ya mtu mwingine au yalikuwa katika 
milki ya mtu mwingine ambae kuna ihtimali kuwa ni maji yake. 
Mas'ala 68: Ikiwa 
mukallaf atafahamu kwa sura ya ujumla ya kuwa mojawapo  kati ya vyombo 
viwili ni najisi  na kingine ni twahara haitajuzu kutumia chombo moja wapo 
kuondolea khabathi au hadathi. 
Mas'ala 69: Chombo 
kinacho shukiwa kuwa sehemu moja wapo ya chombo hicho imenajisika  hakita 
hukumiwa kuwa ni najisi isipokuwa  hali ya sehemu  hiyo ya hapo kabla 
itajulikana kuwa ilikuwa ni najisi, lakini kauli ya ahwat inasema kuwa ni bora 
kujiepusha na utumiaji wa chombo hicho. 
Mas'ala 70: Ikiwa 
maji mutlaq yatafanana na mudhaaf itajuzu kuyatumia maji hayo kuondolea khabathi 
kwa kutumia moja wapo kati ya maji hayo na kuoshea kwa kutumia maji mengine, 
vile vile katika kuondoa hadathi. 
Mas'ala 71: Ikiwa 
itafahamika kwa sura ya ujumla ya kuwa maji haya ima ni najisi au  
ni mudhaaf inajuzu 
kuyanywa maji hayo, lakini haijuzu kuyatumia kutawadhia, vile vile ikiwa 
itajulikana ya kuwa ima maji hayo ni mudhaaf au ni maghsuub (ya kunyang'anya). 
 
Ama ikiwa 
itajulkikana ya kuwa maji hayo ni najisi au ni ya kunyang'anya haitajuzu 
kuyanywa, kama ambavyo  haitajuzu kuyatumia kutawadhia. 
Mas'ala 72: Ikiwa 
sehemu au pande zitiliwazo shaka au zenye shubha hazijulikani kidhati, katika 
hali kama hii inajuzu kuyatumia maji hayo bila kipingamizi. 
 
 
KIFUNGU CHA KUMI
HUKUMU ZA  MAJI  MUDHAAF
Mmas'ala 73: Maji 
mudhaaf, kama maji ya uwa waridi ni twahara ikiwa hayakuingiwa na najisi, lakini 
maji hayo si yenye kutwahirisha hadathi,  vilevile si yenye kutwahirisha 
khabathi hata katika hali ya dharura. 
Mas'ala 74: Maji 
mudhaaf yana najisika kwa kuingiwa tu na najisi sawa yawe mengi au kidogo, 
isipokuwa yakiwa ni yenye kuchupa  kwa nguvu juu ya najisi, hata kama 
yanatoka chini kwenda juu kama maji yatokayo kwenye bomba lenye 
kunyunyizia  na mfano wa hiyo, katika hali kama hii itahukumiwa kuwa ni 
najisi sehemu ile tu iliyo gusana na najisi, na haivuki na kuelekea 
juu. 
Mas'ala 75: Ikiwa 
maji mudhaaf yatanajisika hayatatwahirika isipokuwa kwa kuyaweka kwenye 
kuri  au kwenye maji yenye kutiririka na kutoweka hali ya kuwa kwake maji 
mudhafu. Na kutwahirika  kwa maji mudhaaf  yaliyo najisi kwa 
kuyachemsha ( au kuongeza kiwango cha maji hayo) kuna ishkaali. 
  
 
 KIFUNGU CHA 
KUMI NA MOJA 
MABAKI YA 
CHAKULA 
Mas'ala 76: Mabaki ya 
chakula yote ni twahara isipokuwa mabaki ya mnyama alie najisi (najisul aini) 
kama mbwa Nguruwe na mushrik (kafir) , hakika mabaki yao ni najisi. 
Mas'ala 77: 
Nimakuruhu kula mabaki ya mnyama asie liwa isipokuwa mabaki ya Muumini na paka 
kutokana na kauli ya baadhi ya mujtahidiin. 
 
SEHEMU YA PILI: HUKUMU ZA CHOONI 
  
PIA KUNA VIFUNGU KADHAA 
  
  
KIFUNGU CHA KWANZA 
 
 
  
HUKUMU ZA KWENDA CHOONI 
Mas'ala 78: Ni wajibu 
wakatio mtu anapokwenda chooni au katika hali ya kujisaidia haja kubwa bali hata 
katika hali nyingine tofauti kusitiri uchi (sehemu za siri) – nazo ni sehemu ya 
mbele na nyuma na peke mbili- kwa muonaji mwenye kuheshimiwa, isipokuwa mtoto na 
mwenda wazimu wasio weza kupambanua, na mke na mume na alie milikiwa kwa mmiliki 
wake na alie halalishwa kwa alie halalishiwa, hakika kwa watu hawa inajuzu kwa 
kila mmoja wao kuangalia uchi wa mwenziwe.  
Mas'ala 79: Hakuna 
tofauti katika uharamu wa kuangali kati ya uchi wa  Muislaam au kafiri 
kutokana na kauli ya ahwat. 
Mas'ala 80: Si wajibu 
kusitiri mapaja mawili wala matako wala nywele ziotazo pembezoni mwa sehemu za 
siri (mavuzi). Ndio, ni sunna kusitiri sehemu zilizoko kati ya kitovu na 
magoti. 
Mas'ala 81: Haijuzu 
kuangalia uchi wa mtu mwingine kwa kutumia kioo na mfano wa hicho, wala kwa 
kutumia kioo cha kujitizamia  na wala haijuzu kuangalia kwa kutumia maji 
yaliyo safi.   
Mas'ala 82: Ikiwa mtu 
itamlazimu kuangalia uchi wa mtu mwingine kama katika hali ya kumtibu mgonjwa, 
kauli ya ahwat ni kuwa ataangalia kupitia kioo kilicho wekwa mbele yake ikiwa 
kufanya hivyo kutatosheleza na kuondoa dharura hiyo, laa sivyo hakuna 
tatizo  kuangalia. 
Mas'ala 83: Ni haramu 
kwa mwenye kujisaidia haja kubwa – wakati wa kujisaidia- kuelekea Qibla na 
kukipa mgongo Qibla kwa kuielekeza sehemu ya mbele ya mwili wake  kwenye 
Qibla hata kama uchi wake atauelekeza sehemu au upande mwingine tofauti na 
sehemu hizo mbili, na kauli ya ahwat ni kuwa ataacha  kukielekezea  
uchi wake pekee hata kama sehemu za mbele za mwili wake zitaelekea  sehemu 
hizo mbili, na makusudio ya sehemu za mbele za mwili ni kifua tumbo na magoti 
mawili, na ikiwa italazimika kufanya moja wapo atakuwa na hiari japokuwa kauli 
ya ahwat ni kuwa atakipa mgongo, na akiwa itamlazimu kufanya kitendo kimoja 
wapo  kati ya mambo mawili hayo na kuto jisitiri pamoja na kuwepo 
muangaliaji mwenye kuheshimiwa itawajibika kwake kujisitiri. 
Mas'ala 84: Kauli 
yenye nguvu ni kuwa si haramu kukielekea au kukipa mgongo kibla katika hali ya 
kufanya istibraa na katika hali ya kustanji japo kuwa kutofanya hivyo ni ahwat 
(bora zaidi). Ndio ikiwa atafahamu ya kuwa mkojo utatoka  kwa kufanya 
istibraa kauli ya ahwat ni kuwa itawajibika kuacha kukielekea au kukipa mgongo 
Qibla. 
Mas'ala 85: Lau kama 
mukallaf atapatwa na shubha katika kukipambanua Qibla hukumu ya kutumia dhanna 
haiko mbali pamoja na kuto kuwepo uwezekano wa kukitafuta na kufanya uchunguzi 
wa sehemu ya Qibla, na ikiwa kuichelewesha sala kutamsababishia 
matatizo. 
Mas'ala 86: Ni haramu 
kujisaidia haja kubwa kwenye milki ya mtu mwingine isipokuwa kwa idhini yake, 
vile vile ni haramu kujisaidia kwenye makaburi ya waumini ikiwa kufanya hivyo ni 
kuvunja heshima yao. 
Mas'ala 87: Ni haramu 
kujisaidia haja kubwa kwenye mashule na mfano wa hayo ikiwa haikufahamika kuwa 
sehemu hizo zimewekwa waqfu kwa ajili ya watu wote, na inatosha idhini ya 
msimamizi wa waqfu hizo, na kauli iliyo dhahiri ni kutosheka na ada ya 
watu  ikiwa kufanya kwao kutakupa matumaini ya kuwa ni sehemu ya matumizi 
ya watu wote, vile vile hali ni hiyo hiyo kwenye matumizi mengine ya vitu hivyo 
vya waqfu. 
KIFUNGU CHA 
PILI 
 
 
KUSTANJI 
Ni wajibu kuosha 
sehemu ya kutokea mkojo kwa maji, na inatosha kuosha mara moja japo kuwa kauli 
ya ahwat ya sunna ni kuosha mara kadhaa, na haitoshelezi kitu kingine tofauti na 
maji, na sehemu ya haja kubwa ikiwa haja itavuka mahali pake na kutapakaa hapo 
italazimika kutumia maji pekee kama najisi nyingine, na ikiwa hakikuvuka mahali 
pake mukallaf anahiari ya kuosha kwa maji hadi kusafike mahali hapo, na kati ya 
kupangusa kwa  kutumia mawe au kitambaa au mfano wa hivyo kati ya vitu 
vyenye kuondoa najisi, na maji ni bora zaidi, na kutumia vyote  ndio 
ukamilifu wa twahara. 
Mas'ala 88: Je 
kupangusa kwa mawe na mfano wa hilo inasababisha kutwahirika mahala hapo au 
kusamehewa kwenye sala pekee? Katika kupangusa kuna ishkaali, na kauli ya ahwti 
ni ya pili (  yaani ni sababu ya kusamehewa kwenye sala) 
Mas'ala 89: Katika 
kupangusa huzingatiwa kutumia mawe matatu au mfano wa hayo, au kutumia pande 
tatu za jiwe moja na mfano wa hilo japo kuwa kuna uwezekano wa kusafika kwa 
kutumia chini ya mawe matatu, na kama hapakusafika mahala hapo kwa mawe matatu 
ataongeza mpaka pasafike mahali hapo. 
Mas'ala 90: Ni wajibu 
mawe yatumikayo au mfano wake yawe twahara. 
Mas'ala 91: Ni haramu 
kustanji kwa kutumia vitu vyenye kuheshimiwa, vile vile ni haramu kutumia mifupa 
na kinyesi. Na lau kama mtu atastanji kwa  kutumia vitu hivyo atazingatiwa 
kuwa ameasi, na kutwahirika au kusameheka kwa kutumia vitu hivyo kuna 
ishkaal. 
Mas;ala 92: Ni wajibu 
katika hali ya  kuosha kwa maji kuondoa najisi yenyewe na athari zake kwa 
maana kuwa kuondoa chembe chembe ndogo ambazo hazionekani na kwa kawaida 
haziondoki isipokuwa kwa kutumia maji, na si wajibu kuondoa rangi na harufu, na 
inatosha katika upangusaji  kuondoa najisi yenyewe, na si wajibu kuondoa 
athari za najisi, na ikiwa haja kubwa itatoka ikiwa na najisi nyingine isiyo 
kuwa hiyo kama damu au mahali pa haja kubwa pakagusana na najisi nyingine kutoka 
nje  haitatosheleza kuitwahirisha sehemu hiyo ispokuwa kwa kutumia maji, na 
lau kama atatia shaka ya kuwa imetwahirika sehemu hiyo au laa atajengea ya kuwa 
haikutwahirika na hapa atakuwa na hiayari kati ya kutumia maji  mawe na 
mfano wa vitu viwili hivyo. 
 
KIFUNGU CHA TATU 
 
ADABU ZA KWENDA CHOONI 
Ni sunna kwa mwenye 
kujisaidia haja kubwa kujitenga na watu au kwenda sehemu ya mbali ambayo 
hatoweza kuonekana, na katika haja ndogo atafute sehemu yenye muinuko, kama 
ambavyo ni sunna kwake kufunika kichwa na kufunga kitambaa shingoni, na kufunika 
kicha na nyingo kwa kilemba au kitambaa  kunatosheleza kufunika kichwa, na 
ni sunna kutanguliza mguu wa kulia wakati wa kutoka, na kufanya istibraa, na 
kujitegemeza kwenye  mguu wake wa kushoto – wkati wa kukaa- na kupanua mguu 
wa kulia, na ni makruuhu kujisaidia barabarani, njiani,  chini yamiti ya 
matunda, na sehemu za kulaaniwa, kama kwenye milango ya majumba na mfano wa 
sehemu hizo kati ya sehemu ambazo mwenye kujisaidia sehemu hizo anakuwa 
amejisababishia watu kumlaani, na sehemu zilizo andaliwa kwa ajili ya vituo vya 
misafara, na kulielekea jua au mwezi kwa utupu wake, na kula na kunywa katika 
hali ya kujisaidia, na mengineyo kati ya mambo yaliyo tajwa na maulamaa radhi za 
mwenyezi mungu ziwe juu yao, japo kuthibiti kwa baadhi ya mambo yaliyo tajwa 
kuwa ni ya sunna au makruuhu kuna ishkaali. 
Mas'ala 93: Maji ya 
kustanjia ni twahara hata kama yamestanjiwa sehemu ya kutokea mkojo ikiwa 
yatatimia masharti haya yafuatayo:  
1- Kuto badilika rangi, 
ladha na harufu ya maji hayo kwa najisi. 
2- Kuto ingiwa na najisi 
nyingine kutoka nje tofauti na mkojo. 
3- Kuto vuka najisi 
itokayo kwenye sehemu yake ya kawaida. 
4- Haja kubwa na ndogo 
isitoke pamoja na najisi nyingine  kama damu, isipokuwa ikiwa itatoka 
lakini si yenye kuonekana katika hali hiyo hakuna tatizo. 
5- Kusiwe na chembe 
chembe za haja kubwa zenye kuonekana kwa kauli ya ahwat. 
Kwa kukamilika 
masharti haya maji ya kustanjia yanakuwa ni twahara na yanaweza kutumika 
kuondolea khabathi, lakini haijuzu kuyatumia kuondolea hadathi wala  
kuyatumia kwenye udhu wa sunna na ghusli ya sunna. 
 
 
 
KIFUNGU CHA 
NNE 
 
 
 
 
 ISTIBRAA 
Namna ya kufanya 
istibraa ya mkojo ni kama ifuatavyo, kwanza uta pangusa kuanzia kwenye makalio 
(yaani mwanzoni mwa sehemu itokeapo haja kubwa) hadi mwanzoni mwa kiungo cha 
kiume mara tatu, kisha uta anzia mwanzoni mwa kiungo cha kiume hadi kwenye 
kichwa cha uume mara tatu, na mwisho utakikamua kichwa mara tatu. 
Na faida ya istibraa 
huonekana pale utakapo  kuhukumiwa kuwa ni twahara unyevu nyevu 
utokao baada ya kufanya istibraa unao shukiwa kuwa ni mkojo au laa, na umaji 
maji huo ukitoka si wajibu kutawadha, na lau kama utatoka umaji maji unao 
shukiwa kuwa ni mkojo kabla ya kufanya istibraa – hata kama mukallaf aliacha 
kufanya istibraa kutokana na dharura na kutoweza kufanya hivyo- atajengea kuwa 
ni mkojo, na itawajibika kujitwahirisha kwa kutoka umaji maji huo na  
kumlazimu kutawadha. 
Na huambatanishwa na 
istibraa katika faida zilizo tajwa muda wote ambao anayakini kuwa hakuna chembe 
chembe zilizo bakia kwenye mirija itoayo mkojo, na mwanamke hafanyi istibraa, na 
umaji maji utokao kwenye sehemu zake za siri unahukumiwa kuwa ni twahara na kuwa 
hautengui twahara ikiwa haikutambulika kuwa ni mkojo. Ndio ni bora zaidi kwa 
mwanamke kusubiri kidogo- baada ya kukojoa – na kukohoa kohoa na kujikamua utupu 
wake (sehemu zake za siri) kwa upana kisha kuiosha kwa maji. 
Mas'ala 94: Faida za 
kufanya istibraa hupatikana katika istibraa hata kama ni kwa kufanywa na mtu 
mwingine kama mkewe au mtu alie milikiwa (mjakazi au mtumwa). 
Mas'ala 95: Ikiwa 
mukallaf atatia shaka ya kuwa amefanya istibraa au amestanji atajengea kuwa 
hakufanya hata kama ni kawaida yake kufanya, na ikiwa atatia shaka mtu ambae 
hakufanya istibraa ya kuwa umetoka umajimaji atajengea kuwa haukutoka hata kama 
atakuwa anadhania kuwa umetoka umajimaji. 
Mas'ala 96: Ikiwa 
atafahamu ya kuwa amefanya istibraa au amestanji na akatia shaka ya kuwa 
amefanya istibraa au amestanji sawa sawa au laa atajengea kuwa ni 
sahihi. 
Mas'ala 97: Ikiwa 
mukallaf atafahamu ya kuwa ametokwa na madhii na hakufahamu ya kuwa madhii hayo 
yalifuatana na chembe chembve za  mkojo au hapana atajengea kuwa ni twahara 
hata kama hakufanya istibraa, isipokuwa ikithibiti kuwa ni umajimaji unao tiliwa 
shaka, na shaka yenyewe iwe katika hali ifuatayo ya kuwa umaji maji huu 
uliodhihiri je yote ni madhii au  ni mchanganyiko  kati ya madhii na 
mkojo.  
 |