Home Page
Maisha Ya Shekh
Vitabu Vyake
Hukumu Na Fat’wa
Wito na fikra za shekh
Vitabu Vya Mwanae
Maktaba Ya Kituo
Picha
Wasiliana Nasi


Affiliate Websites
Affiliate Websites

   E-Mail Listing:


 

MUKHTASARI WA MAISHA YA KIONGOZI WA JUU WA KIDINI AYATULLAHIL UDHMAA SHEIKH MOHAMMAD FAADHIL LANKARANI (MUNGU AMJAALIE UHAI MREFU).

بسم الله الرحمن الرحيم

الذ ين يبلغون رسالات الله ويخشونه ولا يخشون أحدا إلا الله وكفي بالله حسيبا

Tunamshukuru  Mwenyeezi Mungu ambae amemuumba mwanaadamu na akamfundisha kubainisha, na shukurani ni za Mwenyeezi Mungu ambae alifundisha kwa kalamu, na mfundisha mwanadamu mambo asiyo yajua. Na rehema na amani ziwe juu ya mbora wa viumbe vyake na hitimisho la mitume wake Mohammad na Aali zake walio wema na  watakatifu wenye kuongoza na wenye kubarikiwa.

 Nilikuwa na matamanio makubwa yalioje – yakuwa na mimi nipewa jukumu la kuandika kuhusiana na maisha ya mwanazuoni kati ya wanazuoni wa kiislaam, na marjiu[1]  mtukufu kati ya marajiu wa madhehebu ya kishia , na kuhusiana na  mwalimu mkubwa kati ya walimu wa Hawza (shule) ya kielimu ilioko mji  mtukufu wa Qum- basi tusitosheke katika kuyazungumzia maisha ya kundi fulani la  maulamaa wetu na wanafiqhi wetu katika kuelezea juu ya maisha yao tu na kuwataja majina  yao na nasabu (koo) zao au  kuizungumzia sehemu ya elimu yao na athari zao, bila ya kuvuka mipaka hiyo na kuzungumzia yanayohusiana na maisha yao  kiimani na juhudi walizozifanya wakiwa wakwelika  katika kujijenga kiroho na kitabia au kimaadili, na hatua zao za kielimu na mwenendo wao binafsi na ufahamu wao wa kijamii na kisiasa.

Na kwa hakika nimegundua ya kuwa historia za wengi wao- radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- zilikuwa zimejawa na mazingatio mengi na faida nyingi, na zikiwa zimejitosheleza kutokana na athari walizoziacha, zikiwemo sifa njema na mambo mengi ya fakhari waliyo yaacha,

na juhudi kubwa walizo zitoa na ushupavu mkubwa waliouonyesha na misimamo ya kishujaa waliyokuwa nayo, na kujitolea muhanga waliko kufanya katika njia  yenye miba mikali na huku wakikwaruzana na mashetani  wa zama zao, na wakisimama kidete kwenye rai zao, wakipigana jihadi kupinga upotovu wa aina yoyote ndani jamii yao,  wakiamini ya kuwa  maisha ni Itikadi na jihadi, laa sivyo ni udhalili na aibu duniani na udhalili katika Akherah, kwa hivyo basi hakika maisha yao yanafaa kuwa ni masomo yenye kutoa faida na kutunufaisha sisi na yawe ni Ardhi safi kwa kilimo na utoaji wa mavuno mengi.

Kwa hiyo basi ikiwa tutawazungumzia maulamaa wetu kwa mtizamo kama huo , basi kuyaelezea maisha yao haitokuwa  sawa na  kukielezea kitu kilicho kifu na kuandika mistari tu na mukhtasari au ishara fupi za maisha yao, bali ni jitihada ya uwekaji wazi na upekuzi wenye faida kuhusiana na matokeo ya  maisha yao kwa kupekua kila kipengele,  tunafanya hivyo huku tukiangalia kwa makini sababu za kuchipuka kwao na malezi yao, malezi ambayo yameunda watu wema na wanazuoni wenye kumuelewa  Mwenyeezi Mungu (wacha Mungu), bila ya kusahau au kughafilika na kuto zitaja sababu za kupea kwao kielimu na kimaarifa katika majaribio yao yenye juhudi kubwa za hatua kwa hatua za kuzifichua elimu za qur’an  elimu za Qur ani pamoja na urithi wetu mwingine, sawa uwe  urithi huo ni wa kielimu au riwaya au rijaali[2] au historia, ukiongezea mambo ambayo zama zao zilipambika  nayo na tamaduni zao ambazo zilikuwa katika zama zao na matukio mbali mbali na fikra tofauti na athari nyingi nyengine, bali matatizo yaliyo kuwepo ambayo yalikuwa yakihitajia misimamo ya kisheria isiyo tetereka na yenye kuhitaji ushupavu na misimamo ya sawa.

 Na hatua hii itakuwa ni yenye kusisitiza na kutilia mkazo zaidi ikiwa tutafahamu ya kuwa  faqihi (mwanazuoni aliyebobea katika elimu ya fiqhi) anapo beba jukumu na kuchukua cheo cha marjiu, hawi ni mufti tu aulizwae kuhusiana na hukumu za kisheria na kujibum tu, na kumfuata yeye (kumfanyia taqliid) hakuwi ni kule tu mukallaf[3] kuchukua risala amaliyyah (kitabu cha fatwa) na kuirejelea pindi anapo ihitajia au kutatizwa na jambo, bali taqliid (kumfuata mwana chuoni katika hukumu za kidini) imekuwa ikielezea mfumo mwingine uelezao namna ya kuwa sambamba na kuwa bega kwa bega na mfumo wa marjiu (mwanachuoni aliyefikia daraja ya ijtihadi) yule na kuufuata mwenendo wake, na kujifunga na kufuata si tu fat’wa zake bali ni kuzifuata rai zake na misimamo yake katika nyanja zote sawa iwe ni katika uwanja wa kiimani au kijamii.

Na sitakuwa nimevuka mipaka  ikiwa nitasema ya kuwa: Hakika maisha ya mukallaf  yamekuwa ni yenye kuchukua sura ya sera na mfumo wa maisha ya anayemfanyia takliid (anayemfuata) na wakati huo basi mahitajio yanakuwa ni makubwa zaidi na ya dharura zaidi katika kuwa sambamba na maisha ya marjiu wa takliid (marjiu anayefuatwa) ili picha ya maisha yake iweze kubainika  kwa muqallid (wafuasi wake na wapenzi wake) na kuwa rahisi kumfanya kuwa ni kigezo chema katika maisha yao ya kidini na kijamii, na awe ni dalili na msaidizi wa kuyajenga maisha hayo kulingana na misimamo yake na fikra zake.

Kwa hivyo basi sisi tuko mbele ya faqihi aliyebobea katika elimu, na mwanazuoni mkubwa kati ya wanazuoni wa fiqhi na wanazuoni wa madrasa ya Ahlul bayti wa mtume (s.a.w.w), ambae amekuwa akinywa  na kuchukua kwenye neema ya elimu zao zilizo pana na chemchem ya maarifa yao mpaka akafikia kiwango cha juu na kupaa kwenye anga  lake la kielimu na kiroho, na hivi leo akawa ni mwanazuoni mkubwa na mwalimu menye nafasi ya juu na marjiu mmoja wa juu  wa kidini kati ya marajiu wa takliid katika zama zetu hizi.

MAKUZI YAKE.

Baada ya  baba wa sheikh Faadhil Lankarani (Mwenyeezi Mungu amtakase) ambae ni mwanazuoni mkubwa wa Fiqhi, kuhama kutoka Qafqaaz, alihamia na kukaa miaka kadhaa katika mji mtukufu wa Mash’had na katika Hawza ya kielimu ya mjini Zanjaani, kisha akuhamia kwenye mji mtukufu  wa Qum baada  Ayatullahi Shekh Abdul kariim Al-haairiy – radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kusimama na kuanzisha Hawza ya kielimu yenye baraka, ili aendelee na harakati zake  za elimu   ya fiqhi kwenye mji huo na vilevile kuendeleza harakati zake za ualimu au ufundishaji.

Basi mnamo mwaka 1350 Hijiria Shamsia. Alizaliwa mheshimiwa shekh Mohammad Faadhil katika mji mtukufu  wa Qum katika familia ya wanazuoni na katika nyumba moja wapo kati ya nyumba za watu wema na wachamungu na akiwa chini ya malezi ya baba yake mtukufu, ambae alikuwa akimpa umuhimu maalum na uangalizi wa aina yake mpaka alipo maliza masomo yake ya elimu ya msingi, na alikuwa ni mwenye kipaji cha hali ya juu katika hatua zote za masomo yake, na hakuwa akiwapita marafiki zake tu  kimasomo katika madrasa, bali wanafunzi wote wa mji  mtukufu wa Qum.

Mhesimiwa Shekh hakuendelea na masomo yake ya sekondari baada ya kumaliza masonmo yake ya elimu ya msingi, bali alikuwa akiuelekeza muelekeo wake na mtazamo wake kuielekea kwenye Hawza ya kielimu ilioko mji wa Qum, mji ambao yalifahamika mapenzi ya mwanazuoni huyu kuuelekea mji huo na shauku yake ya kupata elimu iliyoko kwenye mji huo, na akajiunga na Hawza ya mji huo, na kwa kufanya hivyo basi ndiyo akawa ameianza safari yake ya kielimu, nae akiwa na umri wa miaka kumi na tatu, na yeye katika mji huo alikuwa ni mwanafunzi mzuri wa kupigiwa mfano na ni mwenye mipangilio madhbuti katika fikra zake,  mwenye kufuatilia vyema masuala yake ya kielimu.

Mheshimiwa Shekh alifahamika kwa udadisi wake na umakini wake na juhudi zake na kupenda kwake masomo yake, kwa kiwango kile kile cha akili alicho kuwa akisifika nacho, uwezo wake mkubwa na wa kiwango cha juu katika mfumo wa matendo yake ya Hawzah na harakati zake za kifikra na ufuatiliaji wake wa mambo ya kielimu, kitu kilicho mfanya kupea na kuwa na nafasi ya juu kuliko wengine na kuwapituka wengine na kumaliza kwa haraka daraja zake za masomo, ingawaje daraja hizo zilisifika kwa ugumu na matatizo makubwa, na akaweza kuzitimiza kiukamilifu na kwa umakini mkubwa, na kukusanya nyenzo zote zihitajikazo kwenye Hawza, hali ya kuwa ameyafahamu vyema masomo  hayo ya Hawza, na alikuwa ni mwanafunzi aliyenufaika na ni mwalimu aliye wanufaisha wengi.

Na alikuwa sifa ambazo alisifika nazo na kusifiwa nazo shakhsia yake na kumpambanua na wengineo kati ya marafiki zake  walio kuwa kwenye zama zake, sawa sifa ambazo alizipata kwenye malezi yake ya nyumbani yaliyo  patikana kutokana na juhudi kubwa za malezi ya dhati aliyopewa na mzazi wake, au aliyoyapata katika kujizatiti kwake kwenye nafsi yake, hali akiishi kwenye mwenendo wa masomo yake na akihudhuria kwenye masomo ya maulamaa wakubwa  wa Hawzah kati ya maulamaa walio julikana  si tu kwa wingi wa elimu yao, bali kwa malezi yao mazuri, kwa wanafunzi wao na uadabishaji mzuri wa wanafunzi wao.

Sifa hizi zilikuwa zikifuatana na maisha ya Shekh wetu mtukufu tangu akiwa mwanafunzi mdogo katika Hawzah ya kielimu na akipasua na kupambana na hatua zake zilizo kuwa ngumu kwa neema alizo mpatia Mwenyezi Mungu mtukufu za kiakili yenye nguvu na ufahamu ulio wazi na uzingatiji wa hali ya juu, mpaka akafikia hatua ya kukwea na kukaa kwenye kiti cha ufundishaji akizungukwa na kundi la wanazuoni wakubwa wa  Hawzah ya kielimu na watu wenye fadhila kwenye Hawza hiyo, wakifaidika kutokana na utafiti wake na rai zake huku wakijipamba na tabia zake na mwenendo wake.

Mheshimiwa Shekh alifuatana katika masomo yake ya Hawzah na rafiki yake marehemu  Shahiid Ayatullah al-haji sayyid Mustafa  al-khomainiy, mtoto mkubwa wa mheshimiwa imamu Khomainiy (Mwenyezi Mungu autakase utajo wake mtukufu), kwani yalikuwa yakiwaunganisha mahusiano  madhubuti yaliyo kuwepo kati yao na urafiki mkubwa wa kidhati.

Na walibaki kwa muda mrefu  wakikumbushana na kusoma pamoja masomo yao ya Hawzah na wakifanya bahthi pamoja kwenye Hawzah hiyo kwa kwa miaka mingi.

Mheshimiwa Sheikh Faadhil kuhusiana wenye baraka anasema: (Kuwepo kwa rafiki huyu mpenzi, kulikuwa na athari kubwa na yenye nguvu, nguvu ambayo ilikuwa ikinifunga kwenye njia ambayo niliamua kuifuata , hakika tulikuwa ni marafiki wawili wenye kusaidiana tukikumbushana masomo yetu na kufanya bahthi pamoja kwenye masomo hayo).

 Na kwa hakika hii ilikuwa ni sababu moja wapo ambayo ilimhamasisha mheshimiwa Sheikh kuendelea na masomo yake ya Hawzah, na miongoni mwa saababu nyengine ni msimamo wa baba yake ambae ndiye mlezi na msimamizi wake na ambae ndiye aliye kuwa akimtilia umuhimu wa aina ya pekee na akimpa nafasi na umuhimu mkuwa kuliko ndugu zake wengine watatu, na hasa hima hiyo ilizidi baada ya kugundua kuwa ni kijana mwenye uwezo  na mwenye mapenzi makubwa ya masomo ya Hawzah, kwa hiyo akazidisha ile hali ya kumfuatilia na kumlea au kumpatia malezi maalum na kumfundisha, na yote haya yalikuwa na athari kubwa katika  kuielekea kwake Hawzah na kuzidi kung’ara katika marafiki zake na waliyo kuwa wakiishi katika zama zake.

Kama ambavyo kuna sababu mbili muhimu alizo zipata mheshimiwa Sheikh, hakika Mwenyezi Mungu alimneemesha kwa kumpa akili yenye nguvu ya kushika na kuwa na uvumilivu (subira) hizi ni sababu mbili ambazo huzihitajia kila mwanafunzi anaye taka kufikia daraja ya juu ya kielimu na maarifa.

Kwa hivyo akawa anazisoma  elimu za Hawzah kwa umakini na huku akipambana na matatizo yake na akizivuka daraja na kuingia daraja nyingine akifanya hivyo kwa makini na kwa muda mfupi, na akawa anazipanda ngazi za elimu kwa muda mfupi na kwa uvumilivu wa hali ya juu na kwa ufahamu wa hali ya juu pia, jambo lililo washangaza walimu wake na marafiki zake na wenye kumpenda.

WALIMU WAKE:

Baada ya mheshimiwa Sheikh kukamilisha daraja mbili za Muqaddimaat na Sutuuh katika muda wa miaka sita, akiwa ameiandaa nafsi yake kwa ajili ya daraja nyengine nayo ni daraja ya (Bahthul khaarij) bahthi ya nje (haya ni masomo ya juu kabisa katika barnaamiji ya Hawzah) daraja ambayo inakuwa na bahthi za juu kabisa na akiwa na umri wa miaka kumi na tisa.Na alihudhuria bahthi za Fiqhi na Usuul  kwa:

 Mheshimiwa Ayatullah al-udhmaa Assayyid Burujardiy Mwenyezi Mungu amtukuze, akawa akichota elimu yake kutoka kwenye chemchem ya Sayyid huyu alie kuwa na kipaji cha juu kabisa cha akili na mwalimu  aliye mzuri na Marjiu mkubwa, na akihudhuria bila ya kukosa kwenye vikao vyake  vya kielimu, akiandika  mihadhara yake ya Fiqhi na Usuul mpaka  ikafikia mihadhara ile kuwa ni mijalladi mitatu mikubwa na yenye milango mingi  katika sheria za Sala.

Ama kwa hakika alikuwa ni sikio lenye kuelewa na mwanafunzi  mwerevu na mdadisi na aliye kuwa akiuliza kila alisikialo, jambo lililomstaajabisha mwalimu wake, na akapata hadhi ya pekee kwa mwalimu wake na nafasi ya juu, nafasi ambayo hakuificha kwa mwanafunzi wake mwalimu huyo na alimfahamisha mzazi wake bila kificho hali ya mwanawe.

Na hebu tuyasikilize aliyo yasema Mheshimiwa Shekh Mohammad Faadhil nae akielezea historia ya kujiunga na masomo ya sayyid Burujardiy akijiimarisha kwa kuchukua mfumo wa mheshimiwa Shekh sayyid  na bahthi zake za kina:

Katika mwaka 1369 hijiria. Shamsia. Nilikuwa na umri wa miaka kumi na tisa, Mwenyezi Mungu mtukufu alinipa tawfiiq ya kuhudhuria bahthi za mwalimu wetu Burujerdiy, na kwa shauku kubwa na uchangamfu wa hali ya juu na kwa sababu ya nguvu ya akili niliyo kuwa nayo nilikuwa nikiandika tukiwa katika hali ya masomo anwani za bahthi na riwaya zake tu ili nikamilishe kuziandika usiku, na hii ndiyo ilikuwa njia yangu katika kuandika masomo ya sayyid ustaadhi wetu.

Sayyid ustaadhi wetu alikuwa ana sifa ya umakini na udadisi katika ibara zake na mfumo  wa kina, isipokuwa ni kwamba kuingia kwake kwenye bahthi na kutoka kwake lilikuwa ni jambo lisilo kosa ugumu wa utambuzi, na kwa sababu hii  kuandika masomo haya lilikuwa ni jambo zito na gumu pia.

Na vilevile Mheshimiwa sayyid  alikuwa katika masomo yake ni kama hakimu ambaye hubeba pamoja nae mafaili maalum ya kila kesi, kwa hivyo katika kila mas’ala kati ya mas’ala ya Fiqhi akihifadhi faili lake maalum  katika kifua chake, na faili hilo likikusanya au likiwa na riwaya mbali mbali za mas’ala hiyo na kauli mbali mbali za maulamaa wa kisunni (Al-aamah) na kishia (Al-khaaswa) kwenye faili hilo, na rai zao zenye kutofautiana kuhusiana na mas’ala hiyo na kuhusiana na riwaya hiyo moja, na baadae huyabainisha mas’ala hayo yaliyo tajwa kwa uwazi kabisa na mwisho kumalizia kwa kutoa rai yake kuhusu mas’ala hiyo.

Siku moja mheshimiwa Sayyid alihudhuria au alikuja kwenye majlisi ya Azaa ya Ahlul bayti (a.s) iliyo kuwa inafanyika nyumbani kwetu, na baada ya kumaliza majlisi na watu kutawanyika kiasi kwamba hakukubakia nyumbani mtu yoyote isipokuwa sisi, baba yangu akasema kumwambia Sayyid ustaadh: Je mnafahamu ya kuwa mwanangu anaandika masomo na bahthi zako ambazo unazitoa katika masomo yenu nae ni miongoni mwa watu walio pewa tawfiqi ya kuhudhuri kwenye bahthi hizo? Sayyid ustaadhi akajibu: Hapana.

Baba yangu akaniambia: Lete masomo uyaandikayo, na umpatie mheshimiwa Sayyi. Nikayaleta yale niliyo kuwa nikiyaandika  na kuyaweka mbele yake. Nae akamaliza nusu saa  akiyasoma,  kisha akaya tilia ish’kaali juu ya riwaya iliyo nukuliwa kwenye kitabul -wassaila, kisha akanigeukia na akawa akinihamasisha kuendelea na kazi niliyo kwisha anza kuifanya, na  baada ya hapo sikuchelewa katika kuyaandika masomo ya sayyid ustaadhi wetu siku anapo fundisha.

Na kama sikujaaliwa na kupewa tawfiiq ya kuyaandika siku ile ile nilikuwa nikiyaandika usiku ufuatao, na nilikuwa nikimpatia mheshimiwa kila ninacho kiandika nae alikuwa akiyasoma na akinielekeza sehemu zenye kasoro.

Na miongoni mwa bahthi nilizo ziandika ni bahthi ya nguo ya sala yenye kutiliwa shaka na bahthi hii ni miongoni mwa bahthi muhimu sana katika mlango au kitabu cha sala, na ustaadhi  aliyazungumzia mas’ala haya na kuzielezea pande zake zote za kifiqhi na Usuul, na bahthi hii niliiandika kwa ukamilifu wake kwenye karatasi maalum peke yake bila kuichanganya na bahthi nyengine na nilipo maliza nilimpatia mheshimiwa sayyid, na baada ya kumaliza kuipitia akawa ananihimiza na kunitia moyo na kunihamasisha kuendelea na kazi ya kuandika, na alinipatia kwa wakati huo  tumani mia tano na kilikuwa ni kiwango kikubwa na ni pesa nyingi katika zama hizo.

Na nilipo maliza na kuikamilisha juzu ya kwanza nilimpatia na yeye kuisoma kisha akaamuru ichapishwe. Na alifanya hivyo hivyo pia kwenye juzu ya pili nilipo maliza kuiandika, na ilibakia kwake kwa muda wa wiki moja, na baada ya kumaliza kuisoma takriban thuluthi mbili za kitabu hicho. Akaniambia: Sikukuta makosa ndani yake na hakina tatizo lolote.

Nikamwambia: je unaniruhusu kukichapisha? Akasema: Nenda kakichapiche na gharama yake ni juu yangu. Na kitabu hiki kimezungumzia bahthi za sala, na haya ni matunda ya miaka  kumi na moja ya ufundishaji wa sayyid ustadh wetu. Na mwishoni mwa umri wake mtukufu alisomesha baadhi ya kitabu cha utoaji hukumu (Kitabul - qadhaa).     

Na kwa hakika sayyid ustadhi wetu alikuwa akikitilia umuhimu wa aina yake kitabu hiki. Na ninakumbuka ya kwamba yeye katika majlisi moja  iliyohudhuriwa  na watu wawili au watatu alisema, na kulipita   mazungumzo kadhaa kuhusiana na kitabu hiki:Akasema Sisi tunatoweka na kuihama dunia na hakuna kinacho bakia kwetu isipokuwa kitabu ambacho kimetungwa kwa jina letu, nacho ndicho kinacho bakiza jina letu likiwa hai.

Nyenzo za uchapishaji kwa wakati huo hazikuwa ni nzuri, na hazikuwa kama nyenzo zipatikanazo kwenye zama zetu hizi ambazo ni maridadi na ni nyingi, kwa hivyo nilikiandika kitabu changu hiki mara tatu, mara ya kwanza kikiwa katika hatua ya kwanza na mara ya pili kikiwa kimesahihishwa, na chapa ya tatu kilichapishwa kila ukurasa upande mmoja, na kukipeleka kwa ajili ya uchapishaji.

Na kazi hii ilikuwa ni kazi nzito sana, pamoja na kuwa ilinitaabisha sana, lakini ni kazi niliyo kuwa nikiifurahia kutokana na kuwa ni matunda ya aina yake aliyo tupa ustadhi wetu, na kwa usaidizi wa Mwenyezi Mungu na tawfiqi yake  kimekamilika na kumalizika uchapishaji wake.

Na mimi ninaishukuru kamati ya kielimu katika kituo cha Fiqhul aimmatul at’haar (a.s) ambacho kimeandaa kitabu hiki kwa jili ya chapa mpya, kwa hiyo ni huduma bora na nzuri kwa Fiqhi ya Ahlul bayti (a.s), nina muomba Mwenyezi Mungu mtukufu awazidishie baraka katika juhudi zao hizo na awaneemeshe kwa kuwapa tawfiq na usaidizi.

Yamemalizika mazungumzo ya Sheikh. Na  mazungumzo  haya yote nimeyataja kwenye kitabu nilicho kiandika kuhusiana na maisha ya sayyid Buruujardiy na maisha ya Shekh Faadhil mwanzoni mwa juzu ya kwanza ya kitabu kiitwacho Nihaaayatu taqriir cha mheshimiwa Ayatulla Shekh Alfaadhil, na nimeyanukuu hapa kutokana na ulazima ulio kuwepo       na kwa ajili ya faid yake.

Ustaadhi sayyid Buruujadiy amesema kuhusiana na mheshimiwa Shekh baada ya kuona masomo ya ustadhi wake  aliyo yaandika na akiwa ameyaandika kwa lugha safi ya kiarabu: ( Sikuwa nikidhani ya kuwa katika umri mdogo kama huu kuna mtu anae weza kufahamu  alama zilizo fichika na mambo maalum yaliyoko kwenye masomo yetu, na kuyaandika kwa ibara za kiarabu kizuri na chenye kufahamika).

Kama ambavyo kuna kauli nyingine  ya mheshimiwa sayyid Buruujerdiy, iliyosimuliwa na mmoja kati ya wanafunzi wake aliyekuwa akihudhuria masomo yake amsema ya kuwa  siku moja sayyid Buruujerdiy alisema akimuashiaria Shekh Faadhil:

(Hakika huyu ni mujtahid)  na kauli hii ilikuwa ni kauli  iliyowastaajabisha wengi na kuwatahayarisha wengine hasa tukiangalia katika umri wake nae akiwa ni kijana mdogo na barobaro ambae hajavuka miaka ishirini na tano ya umri wake mtukufu.

2- Mheshimiwa Ayatullah al-udhumaa Imam Khomainiy  Mwenyezi Mungu autakase utajo wake.

Baada tu ya sayyid Imam Khomainiy kuanza kutoa bahthi zake za kielimu watu wengi  kati ya wapendao kuwepo kwake na wapendao elimu yake wakaanza kwenda mbio kuhudhuria mlolongo wa darsa zake, wakichota na kujikusanyia kutoka kwenye elimu yake iliyo kuwa ni nyingi na kubwa na fikra zake zilizo nyingi na rai zake zenye kuamsha watu na vipaji vyake vya kiroho  na vya hali ya juu.

Na mheshimiwa Shekh Mohammad Fadhil ni miongoni mwa watu wa mwanzo na wanafunzi wa mwanzo kuhudhuria kwenye masomo yake, na akamaliza miaka saba akiwa mbele ya sayyid Imam akihudhuria darsa zake na akiwa amehitimisha duru (round) kamili ya usuul katika bahthi za (Alfaadh) matamko na bahthi za kiakili. Kama ambavyo alivyokuwa akihudhuria duru nyingine ya Fiqhi aliyo kuwa akitoa sayyid imam pamoja na masomo yake ya Usuul.

Na miongoni mwa mambo Aliyo sifika nayo na  kuwapita wenziwe Shekh Faadhil ni kuhudhuria kwake  kwenye masomo kusiko katika, na alikuwa akiandika masomo yote aliyokuwa akihudhuria na alikuwa akiandika kwa umakini mkubwa na kwa ufahamu wa hali ya juu mpaka masomo yale yakafika kuwa ni vitabu viwili vikubwa vyenye kukusanya milango tofauti na mingi  ya fiqhi.

3- Mheshimiwa Ayatullah sayyid Mohammad Hussein Twaba twabaiy Mwenyezi Mungu autakase utajo wake.

Pamoja na kuhudhuria masomo yake ya fiqhi na Usuull Shekh  Mohammad Faadhil aliendelea na kupokea masomo mengine, lakini mara hii alikuwa akiyachukua kutoka kwa Allaamah na mwanazuoni mtukufu sayyid Twabatwabaiy muandishi wa Tafsirul miizan, na alisoma kwa mheshiwa sayyid Mwenyezi Mungu autukuze utajo wake masomo ya Tafsiri na Falsafa na Hekima, na alibahatika kusoma sehemu ya kitabu Al-Mandhuumah cha Sabziwariy na Asfaar cha Mullah Swadraa Shiiraziy, ukiongezea kushiriki kwake  kwenye mlolongo na bahthi zingine za Akida na Akhlaaq.

Hakika mheshimiwa Shekh Faadhil aliumaliza muda wake mrefu wa umri wake akihama kwenye vikao vya walimu wake watukufu, ambao ni mheshimiwa Ayatulla al-udhmaa Buruujardiy, na mheshimiwa Ayatullah al-udhmaa Imam Khomainiy, na mheshimiwa Ayatullah Allaamah Twabatwabaiy, na kujichotea kwenye chemchem za elimu yao iliyo kuwa ni nyingi, na wakimpa na kumwagia  mambo mengi kutokana na mifumo yao ya kielimu na kimalezi, kwa hakika ilikuwa ni mito ya salsabiil  hakuwahi kuonja kinywaji kilicho kuwa safi na chenye kukata kiu yake kuliko kinywaji hicho, mpaka kipindi hiki kilicho jawa na faida katika maisha yake kuwa ni nguzo za kielimu na kiroho zilizopata mahala pake kwenye nafsi yake na katika shakhsia yake, na ikaanza kuota mizizi tabia nzuri na mifumo mizuri na sera thabiti na tabia yenye manufaa, mambo yaliyo zisaidia  hatua zake za kielimu na hata za kijamii katika kupasua njia yake kwa kuvumilia mitihani yake, na akifunguliwa katika kila mlango auingiao milango mingine mingi, na kila uwanda au ukingo hujifungua na kuambatana na kingo zingine zilizo kuwa na kina kirefu na zenye manufaa mengi.

 Na hapa mbele yetu kuna sifa za walimu wake na bahthi zao alizo ziandika, na mlolongo wa masomo yake na bahthi zake za kielimu na vitabu vyake alivyo vitunga na ambavyo  mara nyingi akitoka nje ya rai za walimu wake, na akawa akizihoji baadhi ya rai hizo kwa roho ya kielimu na kwa hoja madhubuti, hakika hiyo ni dalili juu ya sifa alizokuwa akisifika nazo mheshimiwa Sheikh kuwa ni mwenye uwezo wa aina ya pekee,  na ufahamu wa masomo ulio madhubuti , na uchangamfu wa hatua kwa hatua na hakueleweka kwa uchovu na uvivu  kwani hakuwa akifahamu kulegea wala kushikwa  na uvivu. 

Na jambo livutialo hapa ni kuwa mheshimiwa Sheikh kipindi ambacho alikuwa akijishughulisha na masomo yake kwa wanazuoni hawa wakubwa na kwa wengineo katika Hawzah ya kielimu wakati huo huo alikuwa akijishughulisha na pia kufundisha, kwa mfano alipokuwa na umri wa miaka kumi na tano alikuwa ni mwanafunzi alie kuwa amewapita wenzake na kuwazidi kama ambavyo kipindi hicho hicho alikuwa ni mwalimu mzuri, na hili ni jambo ambalo ni marachache kupatikana na hupatikana kwa watu wachache tu kati ya wanazuoni wa Hawzah na waheshimiwa wa Hawzah au as’haabul fadhiila. 

Na masomo yake yalikuwa yakihudhuriwa na kiasi cha wanafunzi thamanini  wa Hawzah na walio kuwa wakilingana naye kwa umri, mpaka harakati zake za kielimu  zikaamsha na kuwazindua wengi  walio kuwa wakimshuhudia, na haikomei hapo bali darsa zake zilikuwa zikihudhuriwa na kundi kubwa la watu wazima walio wakubwa kiumri kuliko kijana huyu mwenye elimu na fat’wa zake na ufahamu wake ulio mpana na uwezo wake wa kufundisha wa kisasa na wa aina ya pekee na ulio bora.

Na alipofikia umri wa miaka kumi na tisa darsa zake zikapanuka zaidi na wahudhuriaji wa darsa hizo kuvuka mamia ya wanafunzi. Na mheshimiwa  baadae akaendelea na ufundishaji wa kitabu  Kifayatul Usuul cha Muhaqiqi al-khorasaaniy na hicho ni kitabu cha mwisho kisomeshwacho kwenye daraja ya Sutuuh na kilicho kigumu  katika daraja hiyo. Na kwa hakika alifundisha kitabu hiki na kukikamilisha  mara sita kama ambavyo alifundisha kitabu Al-makaasib pia cha Al-muhaqiq Al-answariy mara tano.

Na hivi ndivyo maisha yake yalivyo kuwa kwa muda wote akiendelea na harakati zisizo koma na juhudi za kielimu zisizo simama mpaka akachaguliwa kuwa marjiu na kupewa cheo hicho na kuwa marjiu taqliid, na kuanzia hapo akawa ni miongoni mwa maraajiu taqliid walio wakubwa wa madhehebu ya Ahlul bayti na mmoja wapo kati ya wanazuoni wake, kama ambavyo alivyondelea na kazi ya kufundisha tangu muda mrefu juu ya mimbari ya masomo ya bahthul khaariji (masomo ya juu kabisa kwenye Hawzah) kama Fiqhi na Usuul, na masomo yake yakihudhuriwa na kundi kubwa la wanazuoni na watu wenye elimu, kama ambavyo idhaa ya jamhuri ya kiislaam ilivyokuwa akiviweka vipindi vya masomo yake  ili walio mbali na mji wa Qum waweze kufaidika na ambae hakupata nafasi ya kuhudhuria masomo ya mheshimiwa Shekh Mwenyezi Mungu amhifadhi na ampe umri mrefu.

Na baada ya kufariki sayyid Imam Khomainiy Mwenyezi Mungu autakase utajo wake- ambae alikuwa akitilia mkazo kuwepo kwa mheshimiwa Shekh  Mohammad Faadhil kwenye Hawzah ya kielimu, na akisisitiza juu ya ulazima wa watu  kufaidika na kuwepo kwake- waumini wengi walirejea na kuhamia kwake katika taqliid. Na baada ya kufariki Ayatullah al-udhmaa Shekh Arakiy Mwenyezi Mungu amrehemu hapo Shekh Faadhil alitambulishwa na kupendekezwa rasmi na jopo la Jaamiatul mudarrisiina la Hawzah ya kielimu  kwa anwani ya kuwa ndiye mtu wa kwanza kati ya maraajiu wakubwa wa taqliid wa umma wa kiislaam.

 Mheshimiwa Shekh - pamoj na haya ni kuwa- alikuwa akisifika na sifa njema na nzuri, na miongoni mwa sifa ya wazi kabisa aliyo sifika nayo ni mapenzi yake ya ndani na ya kweli aliyo kuwa nayo na kumtawalisha kwake mtume (s.a.w) na Ahlul bayti wake walio safi na elimu zao na tabia zao, kama ambavyo alivyokuwa  akisifika na usafi wa nafsi, na kupenda kwake elimu na wanazuoni, na kunyenyekea kwake kwa waumini, na kutilia kwake umuhimu wa masuala yote yanayohusiana na waislaamu wote kwa ujumla na hasa hasa madhehebu ya shia, na juhudi zake alizokuwa akizifanya za kutatua haja na matatizo ya watu na kuwasaidia kwake wanyonge na wenye matatizo (mafukara).

VITABU VYA  MHESHIMIWA AYATULLAH AL-UDHMAA SHEKH MOHAMMAD FAADHIL LANKARANIY

Miongini mwa mambo ambayo inapaswa kujipamba nayo mwanafunzi au mtafutaji wa elimu ni kukuza uwezo wake wa kuandika, ili aweze kutunga vitabu na kuandika  matokeo ya elimu   yake, kwa mfano historia na mwenendo wa maulamaa wetu walio wengi ni kuwa wao waliandika yale waliyojifunza na kuyajua na hawakuficha jambo lolote, na walifanya kazi kubwa na nzuri, kwa hivyo kuficha elimu ni jambo lililo kemewa, na Mwnyezi Mungu anasema:

( إن الذين يكتمون ما أنزلنا من البينات والهدي من بعد ما بيناه للناس في الكتاب أولئك يلعنهم الله ويلعنهم الللآعنون)  سورة البقرة: 159

(Hakika wale ambao wanaficha ukweli  na uongofu tulio uteremsha baaada ya kuubainisha kwa watu  katika kitabu hao wanalaaniwa na mwenyezi mungu na wanalaaniwa na wenye kulaani).

(من كتم علما نافعا عنده ألجمه الله يوم القيامة بلجام من النار) 

(Na  mwenye kuficha elimu yenye manufaa aliyo nayo au aliyo ipata Mwenyezi Mungu atamfunga midomo yake siku ya kiama kwa kamba ya moto).

(ومن كتم علما فكأنه جاهل به)

( Na mwenye kuficha elimu ni kana kwamba yeye ni jahili si mwenye kuijua elimu hiyo).

Na ili isithibiti kwa mwenye kuitafuta elimu au mwanafunzi na mwanazuoni ya kuwa ni mwenye kuificha elimu, ni juu yake kufanya kila njia na juhudi za kuisambaza na kuieneza kwa wengine kwa nyenzo yoyote anayo weza kuitumia kwa kauli au kuandika na kuihifadhi kwa kuiandika  ili  kizazi kijacho kiweze kufaidika nayo.

Na huu ni urithi wetu wa kielimu ambao tumeurithi  kutoka kwa maimamu wetu na wanazuoni wetu ni ushahidi bora, na urithi huo bado upo na utaendelea kuwa ni msingi wa elimu zetu zote, kwa hivyo basi umma hauwezi  kuishi bila ya kuangalia yaliyo achwa na wengine kwa ajili ya umma huo.

Na kila umma unahitajia wanazuoni wake wabakie wakiwa hai kati yao na wawe ni wenye kuishi milele na milele, na inafahamika ya kuwa wao wenyewe na viwili wili vyao huharibika na kutoweka, kwa hivyo tuishi nao kwa fikra zao na rai zao na misimamo yao, na yote haya hayawezi kubakia bila kuhifadhiwa na kuandikwa.

Wanafikra wana maisha mengine ( Maulamaa na wanazuoni ni wenye kubakia kwa muda wote wa kubakia kwa dunia) na ninaweza kuyaita maisha ya pili ya kidunia, lakini mara hii huishi kwa urithi wao wa kielimu na maarifa si kwa viwili wili vyao. 

( Hafi mwenye kuihuisha elimu), na hili ndio jambo liwapambanualo maulamaa na wanazuoni   na watu wengine( Ipateni na itafuteni  elimu yatakupateni maisha), kwa hivyo wale ambao hawajui maisha yao ya kidunia  humalizika kwa kufariki kwao na huwa kama jiwe lililo kuwa juu ya ardhi kisha likawa chini yake.

  Na hapa kuna tashbihi  iliyo nzuri ya baba wa balagha na Faswaha  na ubainifu ambaye ni Amirul muuminiin Imam Ali ( a.s), hakika yeye amemfananisha mjinga ya kuwa yeye( ni sawa na jiwe kubwa ambalo halitoi maji, na mti ulio mkavu usio chipua, na ardhi isiyo mea majani)!

Na maana ya maneno haya - kwa mafhumu yake -ni kuwa mwana zuoni yuko kinyume na vitu hivyo, yeye ni jiwe lile ambalo hupasuka na kutoa maji au kutiririsha mito ya maji, na yeye ni sawa na ule mti ambao watu hujikinga kwenye kivuli chake na kunufaika kwa matawi yake....., na kututolea matunda yenye rangi tofauti, na pia yeye ni sawa na ile ardhi ambayo imefufuka na kumea na kuotesha kila aina ya mimea.

Kwa hivyo matendo ya maulamaa na athari zao na vitabu vyao manufaa yake ni ya watu wote, na matunda yake au faida zake ni nyingi sana, hubakia na kuhama kutoka kizazi kwenda  kizazi kingine ili waweze kunufaika nazo kizazi hadi kizazi kingine, na nyoyo kuyapokea kwa ajili ya kujiadabisha kupitia elimu hiyo, na mikono kupokezana kwa kupeana elimu hiyo ili waweze kunufaika na elimu hiyo mpaka imalizike ardhi na wote waliomo kwenye ardhi hiyo.

Haya ukiachilia mbali faida na manufaa yapatikanayo ya kidunia kutokana na elimu au urithi huo nafasi tukufu na malipo mema na makubwa, ( kwa hivyo mwanazuoni ambae watu hunufaika na elimu yake ni bora kuliko ibada ya watu sabini elfu wenye kufanya ibada),  hadithi inasema:(  utapimwa wino wa kalamu za wanazuoni na damu za mashahidi, na wino wa wanazuoni utakuwa ni bora zaidi juu ya damu za mashahidi).

Kwa ajili ya haya na mengineyo tunawaona wanazuoni wetu - Mwenyezi Mungu awalipe mema juu ya juhudi zao- ni kwa kiasi gani wamekiandalia kizazi kijacho urithi wa kielimu, walikesha usiku kucha kwa ajili yake mpaka wakatupatia urithi huo ukiwa umeandaliwa kwa ajili yetu, kwa hivyo basi ni juu yetu tuwe ni warithi wao walio wema kwa kuuhifadhi urithi huo, bali ni juu yetu kuuzidisha na kuuongeza na kuukabidhi kwa kizazi kijacho ili kiweze kunufaika na urithi huo, na kiweze kizazi hicho kunywa kwenye mito yao ya rahiiq  na maji yao yaliyo safi.

Na Shekh Faadhil ni mmoja wapo kati ya watu hao ambao waliendelea usiku na mchana wakiwa wamekunja magoti yao na huku wakifanya juhudi zisizo koma, na akawa akitoa zaka ya elimu yake si kwa wale waishio kwenye zama zake tu bali kwa wajao pia baada yao, na kwa kufanya hivyo akieneza na kuusambaza ujumbe wake ambao ni ujumbe wa Ahlul bayti wa mtume walio watwaharifu (a.s), kama mwanazuoni mkubwa na Faqihi mwenye elimu naye bado anafundisha na anaelimisha na anaandika na kutunga na kufanya uhakiki kwa kalamu iliyo wazi na ubainishaji  ulio safi ambao watu wote hufaidika nao,naye alikuwa na bado nimwenye kuendelea na jambo hilo, na athari zake zimekuwa zikipokelewa na mikono mbali mbali maalum ya watafutaji wa elimu ya kidini katika Hawzah ya kielimu, ili waweze kufaidika kutokana na urithi huo na waweze kufaidika na rai  makini na madhubuti zilizomo na mifumo yake isiyo tetereka katika Fiqhi na Usuul....

mpaka vitabu vyake  mheshimiwa vikafikia mujallad 40 au zaidi ya hapo, vikiwa vimejawa na fikra madhubuti na elimu kubwa na isiyo na kifani kutokana na ubainifu mzuri na wa wazi.

Na vifuatavyo ni vitabu vyake:

         VITABU VILIVYO ANDIKWA NA SHEKH:

             1- NIHAYATU TAQRIIR  FI MABAAHITHIS SWALAAT

Kitabu hiki kina mijalladi mitatu: 1- Juzu ya kwanza inakurasa 516, na katika utangulizi wake kuna historia ya maisha ya imam sayyid Burujardiy Mwenyezi Mungu autukuze utajo wake, na mukhtasari wa maisha ya muandishi wake  mheshimiwa ayatullah al-udhmaa Shekh Mohammad Faadhil lankaraniy Mwenyezi Mungu amrefushie umri, kisha baadae unafuatia utangulizi wa muandishi, na sehemu ya kwanza ya kitabu hiki inahusiana na utangulizi wa sala. 

2- Juzu ya pili ina kurasa 532, na kitabu hiki kime elezea sehemu ya pili:  Sehemu hii inahusiana  na matendo ya sala, kisha sehemu ya tatu: Inahusu mambo yakatayo na kubatilisha sala, na sehemu ya nne: Inazungumzia kasoro zijitokezazo kwenye sala.

3-Juzu ya tatu, inakurasa 424, na shekh kwenye sehemu hii  anakamilisha sehemu ya nne na baada ya kuikamilisha anahamia kwenye sehemu ya tano: Inayo husiana na kulipa sala (kadhaa), kisha sehemu ya sita: Inayohusu sala ya jamaa.

Baada ya yote haya ameweka vyanzo na masaadir alizo zitegemea kwenye uandishi na uhakiki wake na mtiririko wa yaliyomo kwenye juzu tatu za kitabu hiki.

Na kitabu hiki ndiyo kitabu cha mwanzo kati ya vitabu vilivyoandikwa na mhesimiwa  ayatullah al-udhmaa   Shekh Faadhil, na vitabu hivyo ni tahriri ya masomo ya mheshimiwa Ayatullah al-udhmaa sayyid Burujardiy katika bahthi za faradhi ya sala, aliyo yatoa kwa muda wa miaka kumi na moja aliyo ihudhuria Shekh Faadhil kwa mheshimiwa Sayyid Burujardiy.

Na Sayyid mwenyewe alikuwa akifahamu kuandikwa kwa masomo haya kama tulivyoelezea hapo kabla.

Hakika mheshimiwa Shekh alipata hadhi kubwa ya kusifiwa na Sayyid huyu kutokana na kazi aliyo ifanya na juhudi kubwa alizozitoa kwa kufanya kazi hii naye akiwa katika umri huo wenye baraka, na elimu yake hii iliwastaajabisha wengi kati ya watu waliokuwa wakiishi kwenye zama zake au walio kuwa wakihudhuria masomo ya Sayyid.

Na kituo cha Fiqhul aimmamtul at'haar (a.s) kimesimamia kuzihakiki juzu hizi tatu na chapa yake ya tatu ilitolewa mwaka 1420 Hijiria.

2- TAFSWILU SHARIIAH: ( Uchambuzi wa sheria)

Hiki ni kitabu cha Fiqhi kilichoelezea mambo ya kifiqhi  kwa upana na kwa kutoa dalili, na kitabu hiki ni sharhu  au ufafanuzi wa kitabu Tahriirul wasiilah cha mheshimiwa Ayatullahil udhmaa Sayyid imam Khomainiy mwenyezi mungu autukuze utajo wake, na ufafanuzi wa istidlaliy ( kutoa ushahidi na dalili) wa misingi yote ya Usuuli na Kifiqhi ambayo alikuwa akiitegemea mheshimiwa Sayyid imam katika vitabu vyake huku akiiipinga baadhi  na kubakisha na kuikubali mingine.

Na jambo la kuvutia hapa ni kuwa waheshimiwa hawa wawili yaani muandishi asili wa kitabu na muandishi wa sharhu wote wawili waliandika vitabu hivi wakiwa ukimbizini na huku wakivumilia matatizo  na machungu ya ukimbizi, kwani kila mmoja alianza kazi yake yenye manufaa na faida kubwa akiwa mafichoni, kwa mfano Sayyid imam- radhi za mwenyezi mungu ziwe juu yake- alianza kutunga kitabu Tahriirul wasilah akiwa ukimbizini katika nchi ya Uturuki, baada ya utawala uliokuwa ukiitawala Iran na wanachi wake walio dhulumiwa kumfukuza, na mheshimiwa ameyataja hayo kwenye mujjalladi wa kwanza au juzu ya kwanza ya kitabu chake Tahriirul wasilah.

Wakati ambapo msheshimiwa Shekh Faadhil- Mwenyezi Mungu amlinde - alianza kuandika sharhi ya Tahriirul wasilah  iitwayo ( Tafswilu shariiah) naye akiwa ukimbizini kwenye mji wa Yazdi, mji ambao alipelekwa na utawala muovu ulio kuwepo, na haya ndiyo aliyo yataja mheshimiwa Shekh lankaraniy katika utangulizi wa kitabu Al-ijtihadi wa taqliid.

Na kitabu hiki juzu zake nyingi zimechapishwa na zilifikia juzu ishirini, na huenda zikafikia arobaini ikiwa Mwenyezi Mungu ataurefusha umri wa Shekh Faadhil, wakati ambapo juzu nyengine ziko tayari kwa ajili ya kuchapishwa. Na kati ya hivyo vilivyo chapishwa ni kama vifuatavyo:

   4- AL-IJTIHAAD WAT TAQLIID:

Na hii ni athari moja wapo kubwa na yenye thamani kubwa, aliyo isherehesha mheshimiwa Shekh Faadhil siku ambazo alikuwa ametolewa na   utawala dhalimu na kupelekwa kwenye mji wa Yazdi akiwa kama ni mkimbizi wa kisiasa. Na alibainisha mas’ala mbali mbali za Taqliid na hukumu za Ihtiyaat ya mutlaq. Na kitabu hiki kina kurasa 303. Na Shekh alikimaliza kukiandika siku ya ijumaa tarehe 25 ya mwezi wa Rabiul awal  mwaka 1394 Hijiria.

5- ALMIYAAHU: (Maji)

Kitabu hiki kinaanza kwa kuelezea mgawanyiko wa maji na mas’ala mbali mbali  yahusianayo na maji pamoja na kubainisha hali mbali mbali ikiwa yatachaganyika na  Najisi. Na kinakurasa 276. Na kitabu hiki ni kama kilicho tangulia kwani Shekh alikisherehesha na kukifafanua katika muda alio kuwa mafichoni au ukimbizini kwenye mji wa Yazdi. Na kitabu hichi kilikamilika tarehe 17 ya mwezi wa Muharram mwaka 1395 Hijiria.

6- AHKAAMUL WUDHUU WAT TAKHALLIY:
( Hukumu za udhu na hukumu za chooni).

  Mheshimiwa Shekh alikitunga kitabu hiki akiwa kwenye mji wa Yazdi mji ambao alipelekwa kama ni mkimbizi. Na ametaja kwenye kitabu hiki mambo yote au mas’ala yote yahusianayo na mas’ala ya udhu na istibraa, istinjaa na udhu wa pio pio (Bandeji), kwa misingi yake na fikra zake za kifiqhi ambazo zilielezewa na mheshimiwa sayyid imam Khomeiniy Mwenyezi Mungu autukuze utajo wake. Na kitabu hichi kina kurasa 432. Na alimaliza mheshimiwa Shekh kukisherehesha kitabu hichi mwishoni mwa mwezi wa dhul hajji mwaka 1390 Hijiria.

7-ANNAJAASAATU WA AHKAAMUHA: (Najisi na hukumu zake)

 Kitabu hichi kinahusu hukumu za Najisi na namna vitu vinavyonajisika, kama abavyo kivyonaelezea  sehemu za najisi zilizosamehewa katika sala. Na kitabu hichi kina kurasa 492. Na kilimalizika tarehe 18 ya mwezi mtukufu  wa shaabani mwaka 1397 Hijiria. Na kituo cha Fiqhul aimmatul at’haar kinasimamia jukumu la kukichapisha kwa mara nyingine kikiwa kimefanyiwa uhakiki.

8-GHUSLI YA JANABA, TAYAMMUM, NA VITU VITWAHIRISHAVYO:  

Kitabu hichi kina kurasa 723. Na mheshimiwa Shekh  Mwenyzi Mungu amhifadhi alimaliza uandishi wa kitabu hiki mnamo tarehe 18 ya mwezi wa dhul qaadah mwaka 1398 Hijiria. Na mheshimiwa aliashiria mwishoni mwa kitabu hiki matatizo wanayokumbana nayo wananchi na waislaam wa Iran na mambo yaliyo fanywa na utawala ulio wakalia kwa mabavu, na matendeo yake ya kidhalimu kumhusu yeye na kuhusu mali zake na vyanzo vyake vya kiuchumi, na mheshimiwa aliashiria tukio lililo fanyika kwenye msikiti uitwao Masjidul jaamiu wa Kirmaan tukio la kushambuliwa na vibaraka wa utawala ule dhalimu na mashambulizi yaliyo fanywa kwa kundi la watu walio kuwa wamekusanyika kushiriki kwenye maombolezo ya arobaini ya mashahidi waliouliwa Tehraan, kwani waliuwawa kwenye mashambulizi hayo idadi kubwa ya walio kuja kuomboleza, ukiongezea tukio la kuchomwa msikiti na maktaba na vyote vilivyo kuwamo kama Qur’ani tukufu……

9- ASSALATU: (Sala)

Na tayari imekwisha chapishwa juzu moja ya kitabu hiki, ambacho kina kurasa 687, nacho kinazungumzia utangulizi wa sala;  utangulizi wa kwanza unahusu idadi ya faradhi na nyakati zake na sunna zake, utangulizi wa pili unazungumzia Qibla, wa tatu unahusu kisitiri na chenye kusitiriwa yaani nguo ya kusalia, na mwishoni mwake ameelezea nguo yenye kushukiwa, wa nne unahusu sehemu ya kusalia, wa tano unahusu Adhana na iqamah. Na alimaliza mheshimiwa kukiandika kitabu hiki tarehe 26 ya mwezi wa Rajab mwaka 1400 Hijiria.

10-AL-HAJJU: ( Hijja)

Juzu ya kwanza, inakurasa 523, Shekh katika kitabu hiki alizungumzia umuhimu wa ibada ya Hajji katika uislaam na maana yake ya kilugha na kiistilahi na dalili za kuwa kwake wajibu na masharti yake …. Na hijja ya Nadhiri,  Ahadi, na yamini au kiapo.

Na mheshimiwa Shekh alimaliza kuandika kitabu hiki Jumaatatu  tarehe 13   ya mwezi wa  Jamadul Aakhir mwaka 1411 Hijiria.

11- Juzu ya pili, inakurasa 448, na katika juzu hii amesherehesha ndani yake kumhijia mtu au kuhiji kwa niaba ya mtu na kuusia kufanyiwa hajji, na masuala mengine yahusianayo na hijja ya sunna, kisha akazungumzia Umrah na wajibu wa kufanya Umrah na mgawanyiko wake. Na baada ya hayo alizungumzia mgawanyiko wa hajji kwa upana zaidi na hajji ya tamatuu ambayo ni moja kati ya aina za hajji.

Na alimaliza kuandika kitabu hiki tarehe 22 mwezi wa dhul qaadah mwaka 1412 Hijiria.

12- Juzu ya tatu, inakurasa 472, kitabu hiki kimezungumzia vituo vya kuvalia ihraam (mawaaqiit) na hukumu zake, na Ihraam na namna ya kuvaa ihraam, kisha akafafanua mambo yaliyo haramu na yasiyo tendwa baada ya kuvaa ihraam.

Na Shekh alimaliza kukiandika kitabu hiki tarehe 13 mwezi wa Jumadul Aakhir mwaka 1414 Hijiria.  

13- Juzu ya nne, inakurasa 448, mtunzi alipata nafasi katika kitabu hiki kufanya bahthi kwa upana zaidi juu ya mambao mengine yaliyo haramu, na baada ya hayo akahamia na kuzungumzia Twawaf na mambo ya wajibu kwenye twawafu na masharti yake na hukumu zake.

Na juzu hii ilikamilika na kumalizika siku ya Jumaa mosi tarehe 27 ya mwezi wa dhulhajji mwaka 1415 Hijiria.

14- Juzu ya tano, inakurasa 480, katika juzu hii Shekh alizungumzia: Saa’yi, kupunguza nywele, na visimamo viwili vya Arafah na muzdalifah, kisha akahamia kwenye bahthi ya mambo ya wajibu katika Minaa, na mambo yaliyo wajibu baada ya kumaliza matendo ya Minaa, kisha akazungumzia maudhui ya kulala Minaa na kutupa mawe kumpiga shetani (Ramyul jimaari Athallth). Na mwishoni alizungumzia maana ya

( Aswadd wal Hasri na hukumu ya kila moja kati ya mas’ala hayo).

Na alimaliza kukiandika kitabu hiki katika kumbukumbu za arobaini ya imam Hussein (a.s) yaani tarehe 20 ya mwezi wa Safar mwaka 1418 Hijiria.

15- AN-NIKAAH  (Ndoa):

Kitabu hiki kina kurasa 656, na kinazungumzia kanuni za ndoa au Aaadabun nikaah na sababu za kuharamishwa kuoa na mgawanyiko wa nikaha na hukumu zake, pia hukumu za watoto na matumizi. Na alimaliza kukiandika kitabu hiki tarehe 23 ya mwezi wa Ramadhan mwaka 1419 Hijiria.

16- AT-TALAAQ WALL MIIRAATHI: (Talaka na mirathi)

Na kitabu hiki kina kurasa 535. Na kimeelezea masharti ya talaka na mgawanyiko wa talaka na hukumu zake…… Na mambo yanayo wajibisha urithi  vizuizi vya kurithi, na mafungu ya urithi na hukumu zake….

Na alikikamilisha kitabu hiki tarehe 7 ya mwezi wa Rabiuth thaniy mwaka 1420 Hijiria.

17-  AL-QADHAA WA SHAADAAT:  (Utoaji hukumu na ushahidi)

Kitabu hiki kina kurasa 560, na sehemu ya Kadhwa au utoaji hukumu imeelezea masuala mbali mabli ya kifiqhi kama: sifa za kadhi, namna ya kutoa hukumu, shahidi na kiapo…. Na bahthi hizi zimechukua kiasi cha kurasa 387, na kilikamilika kitabu hiki katika mwezi wa Shaaaban mwaka 1419 Hijiria.

Ama kitubu shahaadaati au sehemu ya ushahidi kimechukua kurasa zilizo bakia za kitabu hiki kilicho tajwa, na kinaelezea sifa za mtoa ushahidi au shahidi, na mgawanyiko wa haki, kisha mengineyo, na kilimalizika kitabu hiki katika mwezi wa Safar mwaka 1420 Hijiria.

Na vitabu hivi vitatu vya mwisho  chapa yake ya mwanzo ilisimamiwa na Markazul fiqhil aimmatul at’haar (a.s) kituo ambacho kilisimamia kuvihakiki na kuvichapisha na kuvisambaza.

18- ALQISWAAS (Kisasi):

Kitabu hiki kina kurasa 463. Kilichapishwa kwa mara ya kwanza mwaka 1407 Hijiria, na hii ni chapa yake ya pili, na  kilihakikiwa na kuchapishwa  na kusambazwa na Markazu fiqhul aimmatul At’haar (a.s).

19- AL-HUDUUD:

Kitabu hiki kiliunganishwa na ufafanuzi wenye kutosheleza wa kila mas’ala ambayo yanahusiana na kanuni za sheria au (Huduud) na Adhabu za kiutawala, na alimaliza shekh kukiandika kitabu hiki  na kukisherehesha mwaka 1406. Na kinakurasa 735.

Na markazu fiqhil aimmatil at’haar  inasimamia tena kuchapishwa kwa kitabu hiki kwa mara ya pili baada ya kukamilika uhakiki wake na kupangwa upya bahthi zake.

20- ADDIYAAT: ( Faini)

Kitabu hiki kina kurasa 344, na Shekh alimaliza kukiandika siku ya ijumaa tarehe 16 ya mwezi wa Jumadal uula mwaka 1418 Hijiria. Ama kuhusu bahthi zake ni kama zifuatazo: Mgawanyiko wa uuaji, na kiwango cha faini, na mambo yawajibishayo kubeba dhamana…

21- AL-IJAARAH: ( Kukodi)

Ndani ya kitabu hiki kuna mas’ala yanayohusiana na kukodi au kukodisha na hukumu zake,  na mwishoni mwa kitabu hiki mheshimiwa Shekh hakuacha kuelezea matukio ya umwagaji damu yaliyotokea mwaka 1357 Hijiri Shamsia, na hiyo ni dalili ya kutilia kwake umuhimu mambo na matukio yampitiayo  na mambo mazito, na kitabu hiki kina kurasa 441.

MUUTAMADUL  USUUL:

Kitabu hiki ni uandishi wa masomo yaliyo kuwa yakitolewa na mheshimiwa sayyid imam Khomainiy Mwenyezi Mungu autukuze utajo wake kwa kalamu ya mheshimiwa Shekh Faadhil Mwenyezi Mungu amrefushie umri, na kilichapishwa kwenye kumbukumbu za kumalizika miaka mia moja tangu kuzaliwa kwa imam Khomainiy- Mwenyezi Mungu amuwie radhi -  kilichapishwa na kituo cha (Tandhiim wa Nashri aathari imam Khomaini) mwaka 1420 Hijiria na kitabu hiki kina juzu mbili:

22- Juzu ya kwanza imechapishwa, na inakuras 529 na katika kurasa hizo kumezungumziwa mambo mbalimbali: kama Al-awaamir wa An-nawaahiy, na Al-aam wal mutlaq.. na hukumu za Al-qat’u na Adhannu na Aslul baraa’a. Haya ni yale yahusianayo na juzu ya kwanza.

23- Ama juzu ya pili, imeelezea Tanbiihaatul baraa’a, na Usulul amaliya zingine, na bahthi zingine kama Taadul wa tarjiih, na Ijtihaad na Taqliid, na kikombioni kuchapishwa baada ya kukamilika uhakiki wake kwa usimamizi wa kituo cha aimmatul at’haar (a.s).

24-AL-AHKAAMUL WAADHWIHA:

Hiki ni kitabu cha mas’ala ya fiqhi au kwa jina lingine ( risaalatul amaliyyah) kilicho andikwa kwa lugha ya kiarabu. Na kitabu hiki kina kurasa 488, na kina mas’ala 2042 katika milango tofauti ya fiqhi.

25- RISALATU TAWDHIIHUL MASAAIL:

 Kitabu hiki kimeandikwa kwa lugha ya kifarisi (kiajemi). Na kina kurasa 623, kitabu kimezungumzia mas’ala 2883 ya kifiqhi na mas’ala mengi  yawapatayo  mukallafiin katika ibada  na muaamalaati (uuzaji na ununuaji). Na mwishoni mwake kuna muujam (kamusi) wa istilahi za kifiqhi, na kimechapishwa kitabu hiki mara sitini na hiyo ni dalili ya kuhitajika kwa kitabu hicho.

26- RISAALATU AHKAAMU SHAR’IYYAH TAKHTASU BI SHABAAB:

Kitabu hiki kimekusanya hukumu zinazo wiana na umri wa vijana katika milango tofauti ya fiqhi: kama vile Twahara na vitu vinavyo twahirisha, Udhu, Ghusli, na Tayammam, Sala za wajibu na Sunna, Funga, Khumsi, Zaka, na Muaamalaati ( ununuaji na uuzaji), Vyakula na Vinywaji, na hukumu za ndoa na mas’la mengineyo. Na kinakurasa 216  na katika mwaka 1376 ilitoka chapa ya nne ya kitabu hiki.

27- AL-HAWWASHI ALAA Al-URWATUL WUTHQAA:

     Cha Ayatullahi Sayyid Mohammad Kaadhi Twabatwabaiy Al-yazdiy.

Mheshimiwa Shekh Mohammad Faadhil lankaraniy aliandika ufafanuzi wa kitabu hicho ufafanuzi ambao ulikuwa ukipinga baadhi ya mambo  na uliokuwa na utafiti wa undani, na kitabu hiki kina kurasa 313 kulingana na utaratibu wa kitabu Al-ur’watul wuthqaa. Na  chapa yake ya tatu ilitoka mwaka 1316 Hijiria.

28- MANAASIKIL HAJJI: ( Kwa lugha ya kiajemi)

Na kitabu hiki kimekusanya maswali 1088 yanayo husiana na faradhi  ya hajji na matendo ya ibada, ambayo anayahitaji mwenye kwenda hijja kwenye sehemu  na mahali patakatifu kwa kulingana na maono na fat’wa za mheshimiwa Shekh Faadhil Lankaraniy.

29- MADKHALUT TAFSIIR:

 Na hiki ni kitabu kizuri sana kinacho elezea kuhusu  tafsiri ya Qur’ani tukufu na kuwa kwake ni muujiza na usomaji wake na misingi ya kuitafsiri kwake, na kwamba hakuna ugeuzaji wa aina yoyote uliomo au ulio ifika Qur’ani. Na kina kurasa 296 chapa ya pili ilitoka mwaka 1418 Hijiria.

30- AYATU TATHIIR  RUAYATUN MUBTAKIRATUN:

 Kitabu hiki kimeandikwa na mashekhe wawili watukufu Ayatullah Lankaraniy na Ayatullah Mungu amrehemu Ishraaqiy mkwewe sayyid Imam Khomeiniy- Mwenyezi Mungu autukuze utajo wake- na asili ya kitabu hiki kilikuwa kwa lugha ya kiajemi, kisha kikatafsiriwa kwa lugha ya kiarabu, na ndani yake kuna dalili za wazi juu ya kuwa aya hii iliteremka kwa ajili ya Ahlul bayti (a.s), ambao walifunikwa na kisaa (Shuka) peke yao na si wengineo.

Na kwa hivi sasa markazul fiqhil aimmatul at’haar inafanya maandalizi ya kutoa chapa nyingine mpya na iliyo hakikiwa ya kitabu hiki.

31- AIMMATUL AT’HAAR HAFADHATUL WAHYI FIL QUR’ANI:

Kitabu hiki   kiliandikwa  kwa lugha ya kiajemi na kalamu ya kila mmoja kati ya mashekh hawa wawili, Shekh Faadhil na Ayatullah Ishraaqiy, na kitabu hiki kinatetea utawala au wilayah na uimamu  kwa dalili za kielimu na zilizo wazi. Chapa ya nne ilitoka mwaka 1376 na kinakurasa 455.

32- ATTAQIYATUL  MUDAARATIYYAH:

Kitabu hiki kidogo kimeandikwa kwenye maudhui haya kwa kutegemea  misingi yenye manufaa  ya kifiqhi ya imam Khomainiy, na hasa katika umma wetu wenye madhehebu ya aina tofauti na mengi, na kilitoa athari kubwa  na kuzivutia nyoyo nyingi kati ya wapenzi wa madhehebu haya, baada ya siasa kufanya kazi yake na kuacha cheche zake na alama zake katika tofauti hizi, na aina hii ya taqiyyah ikawa ni jambo la lazima bali hata kufikia kuwa wajibu, kwa ajili ya kuhifadhi umoja wa waislaam.

33- AL-QAWAAIDUL FIQHIYYAH:

Kitabu hiki – kilicho chapishwa katika mwezi mtukufu  wa Muharram mwka 1416 Hijiria kikiwa na kurasa 550- kinazungumzia kanuni ishirini muhimu katika  fiqhi au sheria ya kiislaam na  kuzihakiki. Na kanuni zenyewe ni kama zifuatazo:

1-Qaaidatu adamu dhamaanul amiin illa ma’a taadiy wat tafriit. Kanuni ya kutochukua dhamana alie wekeshwa amana isipokuwa ikiwa atafanya uchokozi na kuzembea.

2-Qaaidatul itlaaf . Kanunim ya kuharibu mali ya mtu.

3-Qaaidatul iqraarul uqalaa alaa anfusihim jaaiz. Kanuni ya kuwa wenye akili kukiri juu ya nafsi zao ni jambo linalo faa.

4-Qaaidatu alal yadi maa akhadha hatta tuaddaa.

5-Qaaidatul ilzaam.

6-Qaaidatu man malaka shay’an malakal iqraau bihi.

7-Qaaidatu Al-maghruuri yarjiu ilaa man gharrahu.

8-Qaaidatu nafyus sabiil.

9-Qaaidatul jubbi.

10-Qaaidatul ihsaan.

11-Qaaidatul ishtiraak.

12-Qaaidatul ishtiraakil kuffar ma’al muuminina fit takliif.

13-Qaaidatu adamushartiyyatul bulugh fil ahkaamil wadh’iyyah.

14-Qaaidatu mashruuiyyatu ibaadatu swabiiy wa adamihaa.

15-Qaaidatu amaariyyatul yad.

16-Qaaidatul qur’aah.

17-Qaaidatu hurmatul iaanatu alal ithmi.

18Qaaidatu hujjiyyatul bayyinah.

19Qaaidatu hujjiyyatu suuqul muslimiin.

20-Qaaidatu akh’dhi ujrata alaal waajibi.

34- KITABU TWAHARAH:

Kitabu hiki ni tahriiri ya masomo ya imam Khomeiniy na kiko mbioni kuchapishwa.

JAAMIUL MASAAIL: (Kitabu hiki ni juzu mbili)   

35- Juzu ya kwanza: ina kurasa 640 pamoja na mas’alala 2248.

36- Juzu ya pili: inakurasa 496 na mas’ala 1307. Na kila juzu ina fat’wa zilizo chaguliwa kati ya fat’wa nyingi zielekezwazo kwa mheshimiwa Shekh Faadhil  pamoja na majibu yake.

37- AL-ISTIFTAA  AATI  HAWLAL HAJJI WAL UMRAH:

Kitabu hiki kinakurasa 144, na kimekusanya maswali yaliyo elekezwa kwa mheshimiwa Shekh Mwenyezi Mungu amuhifadhi, na majibu yake juu ya maswali hayo.

38- AHKAAMUL HAJJI MIN KITAABI TAHRIIRUL WASIILAH:

Kitabu hiki ni ufafanuzi wa mheshimiwa Shekh Faadhil – Mwenyezi Mungu amlinde - wa kitabu Tahriirul wasiila cha Sayyid imam Khomeiniy –Mungu autukuze utajo wake-  wa sehemu ya hajji, na kina kurasa 144 na kina mas’ala mbali mbali kuhusu faradhi hii tukufu, na hadi sasa imekwisha toka chapa ya tatu, na kituo cha Fiqhu aimmatul at’haar ndicho kilicho simamia kuchapishwa na kusambazwa kwa kitabu hiki.

39- AL-FATAAWAL WAAFIYAH:

Juzu ya kwanza, inakurasa 600 na kiko mbioni kuchapishwa. Na kimekusanya mswali mbali mbali ambayo huelekezwa kwa mheshimiwa Shekh Faadhil Mungu amlinde pamoja na majibu yake.

40- MANAASIKUL HAJJI: (Kwa lugha ya kiarabu)

Kitabu hiki kuna kurasa 386.

41- AHKAAMUL UMRATUL MUFRADAH. ( Kwa lugha ya kiajemi)

Kitabu hiki kina kurasa 256 na kimechpishwa mara sita.

IFUATAYO NI MIHADHARA YAKE  SHEKH   ILIYO  ANDIKWA.

1-TIBYAANUL  USUUL:

Na hiki ni tahriri ya mihadhari  au masomo ya Shekh Faadhil –Mwenyezi Mungu amhifadhi- kwa uandishio wa mmoja wapo kati ya wanafunzi wake, aliyokuwa akiyatoa, na kwenye kitabu hicho  kuna masuala ya Al-qat’i wadhanni, Al-imaaratu wal- usuulul amaliyyah. Na kwa hivi sasa juzu ya tatu tu ndiyo yenye kupatikana, na kina kurasa 354, chapa yake ya kwanza ilikuwa mwaka 1414 Hijiria.

Na mheshimiwa Shekh amesema kuhusu kitabu hiki: Nimekikuta kikiwa ni chenye kutosheleza malengo bila ya kuzidisha wala kurudia rudia kunako chosha wala si mukhtasari  wenye upungufu.

2- DUSTUURUL IDAARAH INDAL IMAM ALI (A.S).

Madhumuni ya kitabu hiki ni kufafanua na kusherehesha usia ulio andikwa na imam Ali kwenda kwa Maalik Al-ashtari walii wake kwenye nchi ya Misri. Na kimeandikwa kwa kalamu ya mmoja kati ya wanafunzi wake na ni tahriri ya bahthi ya mheshimiwa Shekh. Na chapa yake ya kwanza ilitoka mwaka 1366 Hijiria Shamsia, kisha kikachapishwa tena mpaka ikafikia chapa ya saba mwaka 1379, na kina kurasa 206, kitabu hiki  kina bahthi nzuri na makini sana.

3-7- IIDHWAAHUL KIFAAYAH:

 Mheshimiwa Shekh Faadhil alisomesha daura kamili katika sutuuh kitabu Kifaayatul Usuul. Na dauru ya mwisho imerekodiwa, na mmoja kati wanafunzi wake aliiandika na kuichapisha kama kitabu kwa jina la IIDHWAHUL USUUL.

 Na kina mijjalladi mitano, na kitabu hicho ni miongoni mwa sharhu mash’huri na iliyo makini kati ya sharhu za Kifaayatul usuul kwa lugha ya kifursi.  Na juzu zote hizi tano zinakurasa 2560.

8- 23- ASSAYRUL KAAMIL FII USUULIL FIQHI: (Asili yake ni kiajemi)

Kitabu hiki ni daura kamili ya bahthi za Shekh Faadhil Mungu amlinde alizo kuwa akizitoa kwenye bahthi za kharijii (masomo ya juu ya Hawzah) kwa muda wa miaka kumi, na kina mijjalladi 16 iliyo chapishwa hadi hivi sasa.

Kila mujjalladi mmoja una kurasa 640, tisa kati ya mijjalladi hiyo inazungumzia bahthi za Al-faadhi (maneno au Lafdhi), wakati ambapo mijaladi mingine inazungumzia bahthi za Al-qat’u wa Adhannu na Ijmaau na Hujjiyyatu khabarul waahid, kisha  bahthi za Ussulul amaliyyah.

24-28- TASHRIIHUL USUUL:

Vitabu hivi ni sehemu nyingine ya tahriri ya masomo ya Shekh Faadhil katika Usuulul fiqhi, kwa uandishi wa wanafunzi wake wawili walio kuwa wakihudhuria darsa zake, mijalladi mitano iko tayari kwa ajili ya chapa, na tunataraji itafikia mijalladi kumi.

29-30- KITAABUL HUDUUD: (Kwa lugha ya kiajemi)

Kitabu hiki kina juzu mbili, juzu ya kwanza inakurasa 670, na juzu ya pili inakurasa 757, nacho kiko mbioni kuchapishwa.

VITABU VYA SHEKH  VISIVYO CHAPISHWA

1-Tafsiru suuratul hamdu. Na hii ni tafsiri bora kabisa ya aya za sura hii tukufu.

2- Ufafanuzi wa baadhi ya bahthi za Tahriirul wasiilah.

3- Kitabul ijaarah, na hiki ni tofauti na kitaabul ijaara fii sharhi Tahriirul wasiilah.

4-Qaaidatu laa dharara, na hii ni tahriiri ya bahthi za sayyid imam Khomeiny.

5- Risaalatun fii swalaatil jum’ah.

6- Al-khumsi, ni tahriir ya masomo ya Sayyid Burujardiy.

7- Al-khumsu min mawsuuah, kutoka kwenye kitabu (Tafsswiilu shariiah fii sharhi tahriirul wasiilah).

8- Ufafanuzi wa kitabu ( Atwaharah) kutoka kwenye kitabu Misbaahul faqiih cha marhuum Al-muhaqiqul Hamadaniy Mungu amrehemu, na huyu ni miongoni mwa maulamaa wakubwa walio pita. Na kitabu chake hiki kimezungumzia mas’ala ya twahara kwa tahkiki ya Ayatullah Shekh Mohammad Faadhil Lankaraniy.

9- Kitabu swaumu.

Mwanzoni mwa mwezi mtukufu wa Ramadhani mwaka 1405 Hijiria mheshimiwa Shekh  Faadhil alianza kukiandika kitabu hiki, na ame elezea bahthi nyingi  zinazo husiana na funga na bado hakijakamilika.

10- Al-masaailul mustahdathah.

   Kitabu hiki ni miongoni mwa tahriri ya bahthi au masomo ya sayyid Khomeiniy. Na kitabu hiki kime elezea baadhi ya bahthi mpya, kama dhamana na mikataba ……………….

11- Kitaabul qadhaa.

Kitabu hiki kimeandikwa na yeye Shekh mwenyewe, na msingi wa kitabu hiki ni masomo ya  mheshimiwa Ayatullah sayyid Burujardiy  katika utoaji hukumu (Al-qadhaa), na jambo la kusikitisha ni kuwa mauti hayakumpa firsa ya kuweza kukikamilisha kitabu chake hiki.

12- Ufafanuzi wa kitabu Atwahara kutoka kwenye kitabu Sharaaiu cha muhaqiqi Al-allamah al-hilliy Mwenyezi Mungu autakase utajao wake. Na kitabu hiki kilicho andikwa kwa hati za mkono kina kurasa 135, na sharhu yake imekamilika hadi kwenye mas’ala ya kurudia kupaka ( Tikraarul mas’hi).

13- Ufafanuzi wa Fuuruu’ul ijtihaad wa taqliid kutoka kwenye kitabu  Al-urwatul wuthqaa. Shekh Faadhil alianza kukisherehesha kitabu hiki katika mwezi wa Jumaadul uulaa mwaka 1384 Hijiria, na kime elezea mas’ala sitini na nane kati  ya mas’ala husianayo na bahthi ya ijtihadi na taqliid ambayo yametajwa kwenye kitabu kiitwacho (Al-ur’watul wuthqaa) cha Sayyid  Twabatwabaiy Al-yazdiy Mungu autukuze utajo wake.

14- Risaalatun fii ahkaamis swalaat fii libaasil mashkuuk.

Kitabu  ni tahriri  ya mheshimiwa Shekh Faadhil ya bahthi za sala zilizo tolewa na mheshimiwa Ayatullah  al-udhmaa Sayyid Buruujardiy, na alianza kukiandika tarehe 22 mwezi wa Safar mwaka 1371 Hijiria.

15- Ismatul anbiyaa.

Hiki ni kitabu kilicho andikwa kwa lugha ya kiajemi kinacho thibitisha Ismaa ya mitume kulingana na aya za Qurani tukufu.

16- Al-qawlu fil mushtaqq.

 Ni tahriiri ya masomo ya sayyid Burujardi.

17- Al-qawlu fil awaamir.

 Pia ni tahriiri za masomo ya Sayyid Biruujardiy mungu amrehemu.

18- Al-qawlu fii shuhratil fat’waaiyyah.

 Pia ni tahriiri ya bahthi na masomo ya Sayyid Buruujardiy.

19- Risaalatun fii qaaidati ( laa haraj)  ya kifiqhi.

20- Ufafanuzi wa kitabu Al-mudwaarabah wal muzaara’a wal musaaqaat kutoka kwenye kitabu Tahriirul wasiilah.

        HARAKATI  ZA SHEKH ZA  KISIAS

Wakati ambao nchi ya iran ilikumbwa na balaa la kutawaliwa na tawala mbaya na dhalimu na watawala madikteta  waovu na mutakabbirina kwa muda mrefu wa historia ya nchi hiyo, na wa mwisho katika utawala huo akiwa Mohammad Ridhaa pahlawiy na utawala wake muovu, na aliyekuwa akifuata madola  makubwa na jeuri  ulimwenguni  yakiongozwa na Amerika, kutokana na tukio hili lenye kuumiza na lenye kutesa watu kulijitokeza na kuamka harakati za ukombozi na zenye kuelewa mambo vyema na vikajitokeza vikundi vya kuendesha mapambano makali, na baadhi ya watu mashuhuri walio jitolea kwenye njia ya Mwenyezi Mungu kupambana na utawala ule,  na kupinga mambo  ya kuhuzunisha na kusikitisha yaliyo wekwa na utawala ule dhalimu na yaliyo acha kwenye nchi hii kilio na masikitiko makubwa pia kilio cha muda mrefu kisicho koma kwa wananchi na watoto wa waislaam wa nchi hii walio kuwa wakipigana kuondoa utawala huu, kutokana na sababu hii maulamaa wengi na wanafikra wengi wa nchi hii  walipatwa   na misukosuko mingi kama kuuwawa na kuadhibiwa na kuteswa na kutiwa jela, pia kufukuzwa  na kulazimishwa kwenda mafichoni, kwa sababu wao walikuwa ndio kundi la vijana lililo kuwa na uelevu na ufahamu wa mambo haya ya kisiasa na kundi lenye imani na lenye kupigana jihadi katika uwanja huu na malumbano haya ya kisiasa na kiutawala yaliyo makali na upambanaji uliokuwa mkali, na kati ya kundi hilo la maulamaa walio kuwa wakiendesha harakati hizi ni mheshimiwa Shekh Mohammad Faadhil Lankaraniy, ambae alikuwa akitoa misimamo yake   mikali ya kisiasa dhidi ya utawala wa Shaha  na uendeshaji wa harakat,  pia misimamo yake ya kisiasa ilikuwa ikitoa na kuonyesha pia kutoa mchango wa aina ya pekee na nguzo ya msingi kabisa katika maisha yake ya kijamii na kisiasa na kijihadi, mpaka misimamo hiyo ikamfanya achukue hatua madhubuti na awe na msimamo madhubuti na hatari kuuelekea utawala, na njia zake na mipango yake ya haraka ilikaribia kumlazimu kutoa maisha yake.

Tangu mheshimiwa Sayyid imam Khomainiy alipo anza  kwenye zama zetu hizi kufanya maandalizi yake na kujiandaa yeye mwenyewe na wafuasi wake na wapenzi wake kupambana na utawala  fasidi ulio wakalia watu kwa mabavu, na kuondoa dhuluma na taabu kwenye umma huu wa kiislaam ulio dhulumiwa na wenye kupigana jihadi,  na kukata mikono ya madhalimu kwenye mali ya watu wa nchi hii walio kandamizwa na kukaliwa kwa mabavu, na kuupiga vita ukafiri wa kiulimwengu ambao unajiona kuwa ndio wenye haki kutawala pakee na utawala wa kidikteta na ambapo shaa alie zikwa alikua ni sehemu moja wapo ya kufru hiyo, na alikuwa ni mwenye kupita kwenye mzunguko huo na mwenye kufuata mkia wa miundo yake na mikakati yake ya uovu.

Mheshimiwa Shekh Mohammad Faadhil ambae alikuwa  ni miongoni mwa wanafunzi wa imam waliokuwa mstari wa mbele na  akiwa ni kati ya watu wampendao kidhati  na kiuhakika na walio kuwa  tofauti na wengine, alikuwa akimfuatilia ustadhi wake katika kila hatua za kijihadi na alifanya hivyo kutokana na imani aliyokuwa nayo  ya usahihi wa misimamo yake na usahihi wa mwenendo wake na umakini pia umadhubuti wa rai zake zisizo tetereka na zilizo simama juu ya msingi wa maarifa na ufahamu kamili wa mambo, misimamo na ufahamu ambao ulitokana na jukumu la kisheria alilo bebeshwa  na kupewa, Mungu amwie radhi.

Mheshimiwa Shekh akawa ni miongoni mwa wale ambao waliungana naye na kuto muacha katika mapambano yake yale ya kijihadi na ni miongoni mwa watu walio simama imara na thabiti kwenye mfumo wake imam.

Na akaendeleza  mapambano yake ya jihadi  yaliyo kuwa makali na kuumiza,  sawa akiwa peke yake au akiwa ameungana na ndugu zake wengine na wakiwa wameunda kikundi chenye kuitilia shindikizo serikali tawala, na yeye alikuwa ni miongoni mwa jopo la Jamaaatul mudarrisiin  jopo ambalo  lilikuwa na  harakati na nashati kubwa zilizoamsha ghadhabu ya utawala ule.

Na wakati utawala ule ulipo  waamrisha vibaraka wake kumkamata Imam, na baada ya kazi hiyo kufanyika aliwekwa jela mpaka itakapo kamilika kazi ya kumhukumu,  maulamaa kumi na mbili wa hawzah  na wanafunzi wao – na Shekh Faadhil akiwa ni mmoja wao - walitoa tamko wakiutaka utawala na viongozo wake kumuachia huru  Sayyid imam Khomainiy, na wakautaka  kuto mhukumu, kwani yeye ni miongoni mwa mamujtahidi wakubwa, na katiba ya nchi hairuhusu kumuhukumu mwanazuoni au aalimu alie fikia kwenye daraja hiyo.

Na pindi utawala ulipo hisi hatari inayo jengeka kwa kuwepo mheshimiwa  Shekh ilitoa amri ya kukamatwa na kupelekwa mafichoni na kumweka sehemu ambayo huhesabiwa kuwa ni sehemu mbaya zaidi katika Iran, na  alipelekwa kwenye sehemu iitwayo ( Bandar langeh) kiasi kwamba joto la sehemu hiyo ni la hali ya juu sana, na alimaliza muda wa miezi minne kwenye sehemu hii ya mbali.

Mheshimiwa anasema kuhusiana na sehemu hii: (Hakika miezi hii mine ilikuwa ni sawa na miaka arubaini kutokana na machungu yake na mitihani iliyo kuwa huko).

Kisha utawala ukamhamishia kwenye mji wa Yazdi pia mji huo uko mbali na mji mtukufu wa Qum na Hawza ya kielimu ambayo alikuwa akiipenda, na alimaliza kwenye mji huo muda wa miaka miwili na nusu kati ya umri wake mtukufu akiyavumilia matatizo na machungu ya mji huo.

Pamoja na matatizo na machungu au maudhi yaliyokuwamo kwenye mji huo isipokuwa ni kuwa mheshimiwa alikuwa akijishughulisha na kufanya tahkiki na utafiti wa kielimu na uandishi, na akifaidika na nafasi hii ya kuwa faragha ambayo alilazimishwa kuwamo kwa nguvu. Na hali hii ni katika upande mmoja.

Na kwa upande mwingine alipokuwa Yazdi alijishughulisha na kujenga mahusiano madhubuti kwa njia ya siri pamoja na shahidi wa mihraab Ayatullah Swaduuqiiy, na walikuwa pamoja na kundi la waumini wakiwaandaa watu na wakiandaa njia ya kufanya mapinduzi dhidi ya utawala dhalimu.

Na kutokana na juhudi zao hizo watu wawili hawa na kutokana na ufahamu wa kina ulio enea kwenye mji wa Yazdi ukianza na wale watu wa mwanzo walio itikia wito wa mapinduzi na kutoa mashahidi wengi, kwani walikuwa wakipigana na utawala na askai wake kwa nikono mitupu wakiwa hawana silaha na wakipambana na silaha zao kwa nyoyo na vifua vlivyo jawa na imani na kupenda kufa shahid, mpaka Mwenyezi Mungu akawathibitishia wao na wananchi wa Iran walio waislaam ushindi na kuweza kusimamisha dola la kiislaam dola ambalo  kwa muda mrefu walikuwa wakiliota wote kwa pamoja.

UTAMBULISHO  WA KITUO CHA FIQHUL AIMMATUL AT’HAAR ( A.S)

Kutokana na kufahamu kwa mheshimiwa Ayatullah Al-udhumma Shekh Mohammad Faadhil Lankaraniy Mwenyezi Mungu amlinde, umuhimu uliopo na faida nyingi, pia manufaa mengi yapatikanayo kwenye  taasisi  na vituo vya kielimu, ni dalili ya kupevuka na kuwa na ufahamu mkubwa, kama ambavyo hiyo ni dalili na muongozo wa kila mfanya utafiti mwenye kufanya juhudi na mwenye kutafuta elimu akiwa na nia safi    ( Mukhlis) na mtu mwenye fadhila na mkweli.

 kutokana na maswaadir na vyanzo na za rejeo (referene)za kifiqhi na harakati za kielimu, ukiongezea na mazingira uwanja unaoandaliwa  na vituo hivyo vya kielimu pamoja na utafiti na tahkiki mambo ambayo hayapatikani  isipokuwa kupitia taasisi hizo, basi haiwezekani Hawzah ya kielimu kujisahaulisha  na kujitosheleza na kuufumbia macho umuhimu  na ulazima wa taasisi hizo, na hasa ukizingatia kuwa ni kituo kilicho sifika na sifa ya kuwa ni kituo cha kisasa na cha takhassusi katika ulimwengu ambao maarifa  na elimu zimepanuka na rai  pia fikra mbali mbali kudhihiti  na kudhihiri  waziwazi,  takhassus  ikawa ni jambo la muhimu sana ikiwa hatukusema kuwa nila wajibu.

 Kwa ufahamu wa Shekh wa mambo haya na mengineyo, mheshimiwa Mungu amlinde  akachukua jukumu kwa kupitia juhudi za kundi fulani la waaumini wenye ikhlas kati ya watu wenye kufahamu umuhimu wa kuyabeba majukumu haya , na kuanzisha vituo vya kielimu vya takhassus.

Vituo ambavyo - pamoja na  vitabu mihimu vilivyomo kwenye vituo hivyo na vyanzo mama vya kila madhehebu – vituo hivyo vina  harakati nyingine za kiutafiti, na vimekuwa vikianzishwa na kundi la wanafunzi wake wakubwa, na walio na kiwango cha juu kabisa ambao walipata kiwango kikubwa cha elimu na wakawa makini huku wakifanya juhudi za kufuatilia masomo yao ya Hawzah, na pembezoni mwao kukiwa na wafanyao utafiti na bahthi, na kukiwa na wahakiki watiliao umuhimu suala la bahthi  katika urithi wa kifiqhi na Usuul na ambao wamesifika na kupambika na sifa ya uvumilivu na kuto kata tamaa katika kazi na wasio acha kufanya kazi hizo, hata kama juhudi zao zitatoa matunda na faida ndogo katika muda huu mfupi ispokuwa matarajio ni kwamba - kutokana na tawfiqi ya Mwenyezi Mungu – juhudi hizo zitazalisha na kutoa matunda au faida yenye manufaa .

Nataraji sintakuwa nimezidisha katika kusifia-ikiwa nitasema ya kuwa: Hakika kituo  hiki cha kifiqhi kinahesabiwa kuwa ni kituo moja wapo cha pekee na cha aina yake katika uwanja huu, pamoja na tuliyo yabainisha hapo kabla na haya yafuatayo, kinasifika kuwa ni kituo cha kisasa katika utaratibu wake na mfumo wake, bali pia malengo yake yaliyo mema.

Na hatuta kuwa mbali na ukweli ikiwa tutasema: hakika kituo hiki kinafanya utafiti kuhusiana na fiqhi iliyo sambamba na zama hizi na misingi ya kufanya ijtihadi, kikizingatia kwa makini kabisa zama hizi na matatizo yake, kikifaidika na urithi wote wa fiqhi ya kiislaam na milango yake na bahthi zake zilizo nyingi kulingana na madhehebu zake tofauti, na kikifanya juhudi kubwa kuyachukua yaliyo sahihi au kuzichukua riwaya zilizo sahihi na kuziacha zilizo dhaifu na zilizo pandikizwa, kwa kutumia dalili za kielimu zenye nguvu na imara na  zilizo  mbali na taasubi (mapenzi tu yasiyo na dalili) yenye kuchukiza na ujizuiliaji ulio pofu na wenye kufuata madhebu, na wenye kuchukia  kuupima urithi wa kielimu kwenye vipimo vya kielimu pekee na si vinginevyo, kikiitetea fiqhi na ufaqihi ambao unasifika na sifa ya usafi na kuto kuwa na shubha ndani yake na unaochambua mas’ala kwa undani kabisa,  na ambao msingi wake unakuwa ni kitabu kitukufu na sunna sahihi na rai za maimamu wakubwa wa waislaam na mafaqihi wenye ikhlaasi, kikitoa neno zuri na fikra iliyo safi, na kinafanya hivyo ili kuunda familia zenye uwezo wa kubeba majukumu na kizazi chenye kufahamu majukumu yake ya kiislaam na kikiufanya umoja wa kiislaam kuwa ndio lengo lake lenye kutarajiwa kufikiwa.

Na ni uzuri ulioje wa kazi hii na juhudi hizi zenye kushukuriwa za kuchambu na kuchekechwa  urithi huu, ili kupata urithi usio na kasoro  na uchafu ndani yake, na kuyatupilia mbali yanayo udhuru mwendo wa umma, umma ambao mwenyezi mungu (ameuweka kati ili uwe shahidi juu ya watu na mtume awe shahidi juu yenu)!

Kwa ajili ya sababu hizi na malengo haya na huenda kukawa na malengo mengine yasiyo kuwa haya, kituo hiki kiliimarisha nguzo zake kikifaidika na ushauriwa na maelekezo ya mheshiomiwa Ayatullah al-udhmaa Shekh Faadhil Lankaraniy mwenyezi mungu amlinde, na kikaweza  kituo hiki tangu miaka mitatu iliyo pita na huu ukiwa ni muda mfupi,  kusimamia na kutekeleza baadhi ya mambo machache na kufanya juhudi za kielimu huku kukitaraji harakati hizo kupanuka zaidi na kuzama na kuwa ni zenye manufaa zaidi na zenye athari kubwa, kwa tawwfiq na usaidizi kutoka kwake subhaanahu.

VITENGO VYA KITUO HIKI.

Katika kituo cha Fiqhul aimmatul at’haar (a.s) kuna vitengo vitano, na kila kitengo kina majukumu maalum na mas’uliyya kiyatekelezayo.

KITENGO CHA KWANZA: KITENGO CHA TAALUMA

 Katika kitengo hiki kuna nyanja na harakati mbalimbali za kielimu:

a- jopo la masuala ya Qadhaa utoaji hukumu au uhakimu.

b-Jopo la masuala ya Hajji.

c- Jopo la uchumi wa kiislaam ( ukodishaji)

d- Jopo la Usuulul fiqhi.

e- Jopo la kanuni za kifiqhi.

Na kila jopo moja wapo kati ya majopo haya kina wanafunzi watano walio bora  na walio chini ya uangalizi wa mwalimu mwenye uzoefu na mwanazuoni mwenye fadhila.

Na washiriki wote katika vitengo hivi, jukumu lao ni kuzitafuta rai na kuzifanyia utafiti na kuzijadili kwa dalili za kielimu. Na mpaka sasa wamemaliza mwaka wa tatu katika kazi hii, na tunataraji juhudi zao hizi zitatoa matunda yenye kuwanufaisha watu wote, na Kitabu (Qaaidatul qur’ah) kilicho andikwa na mheshimiwa hujjatul islaam wal muslimiina Al-haji Shekh Hussein Kariimiy mwalimu wa jopo mojawapo kati ya majopo haya, ni  matokeo na matunda ya utafiti huu, na kilikamilika mnamo mwezi wa ramadhani mwaka 1419 Hijiria.

KITENGO CHA PILI:  UTUNGAJI WA VITABU

Hakika majukumu ya  utendaji kazi wa kitengo hiki ni Fiqhi na Usuul, na kitengo hiki kina idadi kadhaa ya wanazuoni wa Hawzah, ambao wanasifika kwa elimu na uvumilivu na ustahamilivu katika kazi yao, na majukumu yao ni kama yafuatayo:

1-kuandika daura kamili katika maudhui ya Ussulul Fiqhi kwa lugha ya kiajemi wakitumia mifumo ya bahthul khaariji katika elimu ya Usuul ya shekh Ayatullah Al- udhmaa Faadhil Lankaraniy na hadi sasa daura hiyo imevuka mijalladi kumi, na hadi hivi sasa mijallad mitano imekwisha kamilika nayo iko mbioni kuchapishwa na kwa kuzingatia kuwa hakuna kitabu hadi sasa kwenye bahthi hii na kilicho zungumzia kwa upana katika lugha ya kiajemi.

2- Kuandika daura kamili katika Usuulul fiqhi kwa lugha ya kiarabu kwa kujitegemeza au kwa kutumia mifumo ya bahthi ya khariji katika elimu ya Usuulul fiqhi ya Shekh Ayatullah Al-udhmaa Faadhil Lnkaraniy.

3- Kufanya bahthi ya kupingana kati ya Al-asli na Adh-dhaahiri, na haya ni miongoni mwa maudhui muhimu katika elimu ya Usuul, na bahthi hii inafanya uhakiki na utafiti katika sehemu za kupingana kati ya Al-asli na Adh-dhahiir, na kazi hii imekamilika na kitabu chake kikombioni kuchapishwa.

4- Kuandika Mawsuuatu ahkaamu swibyaan.

 Hiki ni kitabu  cha fiqhul muqaarin  kinacho elezea  kwa upana na kukusanya hukumu za madhebu zote za kiislaam, zinazohusiana na watoto ambao hawaja balee, zinazo husu malezi yao, ibada zao, ufanyaji biashara wao,  na haki zao… na kinazungumzia hukumu zote kwa ujumla zinazo husiana na wao.

Na kazi hii imekabidhiwa kwa watu sita kati ya wanazuoni wakubwa wa Hawzah ya kielimu, na juzu ya kwanza ya mausuua hii, ambayo tunataraji kuwa itakuwa ni mijalladi kumi, iko kwenye hatua ya kuchapishwa.

5- Kitabul huduud kwa lugha ya kiajemi, na kitabu hiki ni tahriiri ya masomo ya khaariji katika fiqhi ya mheshimiwa muasisi wa kituo hiki, na kina mujalladi mbili.

6- Kuandika kwa lugha ya kiarabu juzu ya kwanza ya kitabu Jaamiul muasisi, na ambacho kina maswali mbali mbali yaelekezwayo kwa mheshimiwa  Shekhe muasis, na kitabu hicho kina jina la ( Al-fataawaa Al-waafiyah) na kiko tayari kwa ajili ya chapa.

     KITENGO CHA TATU:  UHAKIKI NA USAHIHISHAJI

Hakika majukumu ya kitengo hiki yana hatua tatu:

Hatua ya kwanza: kutoa hadidi za rejea.

Hatua ya pili: Kusahihisha na kuzitathmini dalili (Nusuus).

Hatua ya tatu: Kuziangali na kuzisahihisha.

Na baada ya kumalizika hatua hizi tatu huanza kazi ya kuchapishwa kitabu. Na hadi sasa imekamilika kazi ya kuchapishwa vitabu vifuatavyo:

1- Nihaayatut taqriir, kitabu hiki kina juzu tatu. Na kitabu hiki ni tahriiri ya masomo ya khaariji ya mheshimiwa Ayatullahil udhmaa sayyid Burujardiy mungu amrehemu kwa uandishi wa mheshimiwa Ayatullahil udhmaa Shekh Faadhil Lankaraniy- Mwenyezi Mungu amzidishie umri- kwa muda wa miaka  11 aliyo imaliza akihudhuria kwenye masomo ya mheshimiwa sayyid Ayatullah al-udhmaa Burujerdiy.

2- Q aaidatul qur’pah.

Kitabu hiki kimekamilika kwa juhudi za kundi la wanafunzi wa kituo hiki.

3-Na kuna bitabu vingine vya mheshimiwa Shekhe muasis, ambavyo kazi ya kurejea maswaadir  na usahihishaji wake umekamilika  kwa juhudi za kundi mojawapo  la wanafunzi wa kituo hiki, na baadhi tiyari vimekwisha chapishwa navyo ni kama vifuatavyo:

1-Kitaabul qadhaa.

 2- Kitaabush- shahaadaat.

3-Kitaabul qiswaas chapa ya pili.

4-Kitaabu twalaaq wal mawaariithi.

5-Kitaabun nikaah.

Na vitabu hivi vitano vimeandikwa na Shekh muanzilishi na muasisi wa kituo hiki na ukiwa ni ufafanuzi wake juu ya kitabu Tahriirul wasiilah cha mheshimiwa Ayatullah Al-udhmaa sayyid imam Khomainiy mungu amrehemu.

Na kunavitabu vingine vya Shekh muasisi ambavyo viko njiani kwa ajili ya uhakiki, uchapishaji na usambazaji.

KITENGO CHA NNE: MAKTABA YA KIFIQHI

YA TAKHASSUS

(فيها كتب قيمة)

Katika ulimwengu ambao kila uwanja wa kielimu kitamaduni na kiamali unajifunga kwenye mfumo wa takhassusi, hakika maktaba ya takhassus inajikuta kwamba nafasi yake ina umuhimu mkubwa katika nyanja hizo na inaulazima mkubwa wa kuwa hivyo, haiwezekani kwa harakati zozote za kielimu kujitosheleza na kutolitilia umuhimu  jambo hilo, kwa hivyo kukianzisha kituo hiki ni kazi moja muhimu na iliyo elewa vyema umuhimu huu na iliyo hisi mahitajio kama hayo  hasa kwenye jamii yetu ya Hawzah.

Kwa sababu hii ndio maana ikaanzishwa maktaba hii kwa mara ya kwanza kabisa katika Hawzah ya kielimu ya Qum, na  maktaba hii ikafanywa kuwa ni maalum kwa ajili ya Fiqhi na Ussul za madhehebu zote za kiislaam:  Fiqhi ya kishia, Fiqhi ya shafiiy, Fiqhi ya Hanbaliy, Fiqhi ya Hanafiy, Fiqhi ya Maalikiy, na Fiqhi ya madhehebu zingine kama Zaidiyya na Dhaahiriyyah… Usuulul fiqhi ya shia, Usuulul fiqhi ya Ahlu sunnah, Uluumil qur’ani na ayaatul ahkaam kwa mashia na Ahli sunnah, historia ya Fiqhi, Historia ya wapokezi wa hadithi kwa mashia  na Ahli sunnah, hadithi za shia na Ahli sunna, Al-fiqhul jadiid, Al-fiqhul muqaarin katika madhehebu za kiislaam,  jarida la kifiqhi, na lugha.

Na mheshimiwa Ayatullah al-udhmaa Shekh faadhil Lankaraniy aliamuru ya kuwa milango ya maktaba hii ya takhassusi iwe wazi kwa watu wote wenye kufanya tahkiik na wafanyao utafiti.

Na maktaba imebeba jukumu la kuandaa vitabu vya rejea kadri ya uwezo wake, sawa iwe ni ndni ya Jamhuri ya kiislaam ya Iran au nje ya jamhuri kwa ajili ya kuitumikia elimu na maulamaa na wafanya utafiti.

KITENGO CHA TANO: KITENGO CHA COMPYUTER

Jukumu la kitengo hiki, pamoja na kuandaa maalumaati (elimu) ya lazima kwa ajili ya wafanyao tahkiki, pia kinajukumu la kuandika na kuvitoa vitabu kwa njia ya kifani, kitengo hiki kinahifadhi maalumati yote na maandishi yote kwenye (cd) ili yabakie kwa ajili ya wale watakao taka kufaidika nayo na kwa ajili ya kizazi kijacho.

KITENGO CHA SITA: KITENGO CHA SAUTI NA PICHA

Katika kitengo hiki huhifadhiwa kanda zote  za audio na vidio za masomo ya mheshimiwa Shekhe muasisi, ili waweze kufaidika nazo wafanya bahthi na wanafunzi na kila mwenye kutaka kufaidika nazo…..  Na mheshimiwa Shekh anacho kituo kwenye internet chenye vitabu vyote vilivyo andikwa na shekh na kituo hiki  hupokea maswali na istiftaa ati kupitia kituo hiki na majibu yake huwekwa kwenye kituo hiki.    


[1]- Marjiu : ni mwanachuoni ambae amefikia daraja fulani ya kielimu ijulikanayo kwa jina la    IJITIHADI ,  inawezekana  mwachuoni akafikia daraja hiyo lakini bado asiwe MARJIU kwa sababu neno MARJIU maana yake ni (mwenye kurejewa katika mambo yanayohusiana na dini) kwa hiyo ili watu waweze kumrejea mwanazuoni katika mambo yao ya kidini ni lazima awe ameandika kitabu kinachofafanua mambo hayo na kitabu hicho hua kinaiitwa RISAALTUL-A’MALIYYAH, kwa hio kila mwanachuoni aliyefikia daraja ya IJITIHADI  akawa hajaandika kitabu hicho hua anaitwa MUJTAHID na siyo MARJIU.
[2] RIJALI : ni elimu ambayo inafanya kazi ya kuwasoma wapokezi wa hadithi, au kwa kauli nyengine tutasema kuwa elimu hii inafanya kazi ya kukupa wewe mtizamo mzima wa maisha ya wapokezi wa hadithi.
[3] MUKALLAF:ni mtu aliyefikia umri wa balegh  na  akawa   hajitoshelezi kielimu katika masuala yanayohusiana na ibada au dini  kwa ujumla  bali akawa anamhitajia mwanazuoni fulani  ili  amfuate.